LoyalTzCitizen
JF-Expert Member
- Sep 15, 2010
- 2,241
- 940
wadau karibuni uwanja wa taifa kuona mechi kali tangu mwaka 2015 uingie vijana wa unyamani simba sc watakipiga na kinara wa ligi kuu Azam fc wana lambalamba, vijana wa simba chuo cha soka Tanzania wameahidi kutoa dozi kulingana na hali ya mgonjwa kwa kupiga mpira mwingi ili kupata points 3 muhimu, simba itakuw inawategea vijana waliokwiva kama nahodha isihaka hassani, jonas mkude, saidi ndemla, ramandani singano, okwi(mtoa roho), saimon serenkuma, uku Azam fc ikiwategemea kipre tchetche, domayo, kavumbagu, bocco na brian majegwa.
Karibuni wadau wote mtapata update hapahapa jf.
Mechi itaanza saa kumi kamili jioni
Team today
1. MWADINI ALI
2. SHOMARI KAPOMBE
3. ERASTO NYONI
4. AGGREY MORIS
5. PASCAL WAWA
6. BOLOU MICHAEL
7. MUDATHIR YAHYA
8. FRANK DOMAYO
9. DIDIER KAVUMBAGU
10. KIPRE TCHETCHE
11. HIMIDI MAO
AKIBA
1. KHALID MAHADHI
2. SAID MORAD
3. GADIEL MICHAEL
4. KELVIN FRIDAY
5. KHAMISI MCHA
6. AMRI KIEMBA
7. JOHN BOCCO
Azam hana madhara kwenu wakati anaitafuta pointi ya 23 wakti nyinyi mna 18?
Ama kweli mtu aliyekata tamaa utamjua tu.
Weka na kikosi cha mnyama ili tutoe tathmini.
Weka na kikosi cha mnyama ili tutoe tathmini.
Azam naichukia, Simba nayo siipendi. Sijui leo niwe upande upi! Azam akishinda bado hana madhara kwetu. Simba naye hata akishinda bado si lolote na si chochote.
Leo niko neutral, matokeo yoyote na yaje tu. Mwenyezi Mungu aitendee haki kila timu kwa kuvuna ilichopanda.
bora hata kisipowekwa maana kinahuzunisha sana.
makoye Leo hakuna visingizio vya taulo wala gloves.Leo hakuna uchawi.Leo ni mpira tu
subirini mkija kushituka tulishapita kama mshale.
Mkuu naomba nikukumbushe kuwa niliwahi kupost hapa jamvini kuwa Yanga ndio tageti la uchawi katika soka. Kila kitimu kinachoanzishwa kinataka kuifunga Yanga kwani ndiyo SI unit katika soka la bongo (usibishe!). Sina lengo la kushabikia uchawi maana ni aibu hata kuutaja tu kwa jina lake ingawa kweli uchawi upo. Kwa Yanga muda wote iko cautious kweli kweli!
Ngoja nirudie kwa manufaa ya wengi:
DOUGLAS Muhani, beki wa zamani aliyepata kuchezea klabu kadhaa za Tanzania pamoja timu ya taifa, Taifa Stars, anakumbuka siku ambayo yeye na wachezaji wenzake walipokesha makaburini wakiroga ili kupata ushindi.
Hii ilikuwa ni mechi ya Ligi ya Taifa Tanzania katika kituo cha Mwanza mwaka 1978, wakati akiichezea Sigara (sasa Moro United) na mechi hiyo ilikuwa inaikutanisha timu yake na Yanga.
"Tuliambiwa na mtaalamu wetu kutoka Tanga kwamba lazima tufanye ndumba kwa sababu mechi ingekuwa ngumu. Mganga wetu, ambaye tulikuwa naye tangu mwanzo wa mechi zetu, alituambia kwamba tungeshinda, lakini mwenzetu mmoja angedondoka uwanjani.
"Tuliamriwa kutomgusa wala kumsogelea, kwa sababu kufanya hivyo kungemaanisha kwamba angepoteza maisha," anakumbuka. "Na kweli, kabla hatujafunga bao, mchezaji mwenzetu, John Mlebo, alianguka na kuzimia. Tulimtazama tu mpaka alipochukuliwa kwenye machela. Tulifunga bao, na wakati tulipodhani tumeshinda, Omar Hussein akaisawazishia Yanga zikiwa zimesalia dakika nane tu."
Muhani anasema katika maisha yake ya uchezaji, akiwa amechezea klabu kadhaa kama Sigara, Coastal Union, Maji Maji na Bandari Mtwara, amekumbana na matukio mengi ya ushirikina kuelekea mechi za soka.
Anasema kuchanjwa chale kwenye vifundo vya miguu, kujifukiza ubani, kuoga maji yaliyowekwa talasimu pamoja na kuvalishwa hirizi ni mambo ya kawaida aliyokumbana nayo na ambayo anasema yanaendelea kufanyika kwa siri katika timu nyingi za soka, siyo Tanzania tu, bali Afrika kwa ujumla.
Source: Imani za uchawi zinavyoangamiza soka, nini kifanyike kwa sasa? - Fikra PevuFikra Pevu
mimi ni mshabiki wa mnyama. ila leo ningependa AZAM washinde ili wasogee mbele na kuipa YANGA wakati mgumu zaidi kipoint. Simba tumejitoa kwenye kombe hili maana halina faida sana kama la nani mtani Jembe.lile lina pesa nying zaidi kuliko hata VPL. so leo hata AZAM Wakishinda sitajisikia vibaya sana kwa kuwa YANGA hawatakuwa na amani. na mimi ninachotaka ni YANGA kutokuwa na furaha maisha yao yote. TEAM YA WASHIRIKINA KAMA YANGA ilipaswa ifungiwe lakini naona TFF inawatizama tu.
Mchawi mara nyingi asipofanikiwa kitu cha kwanza kuona ni kwamba anafanyiwa uchawi, wewe unafikiri wachezaji na mashabiki na viongozi pia kama sio wachawi hizo akili za kwenda kuchukua taulo, kuchukua gloves na kwenda kufukua fukua uwanjani wanazitoa wapi?
Baba yetu uliye mbinguni nakuomba uwajalie azam ushindi katika mechi hii dhidi simba, ili mtumishi wako niwe na amani siku ya leo.... AMEN
Hivi Yanga iliwahi kuwa na mwenyekiti anaitwa Bamchawi vile?
Makoye Matale acha kupaka rangi upepo.anayeamini ushirikina ni mshirikina
Mkuu nimesema Yanga tuko cautious muda wote! Hebu angalia mwaka 1978 kabla Azam wala Mtibwa hazijazaliwa Yanga tayari walikuwa wanarogwa, kwa nini wasichukue tahadhari?
Wewe mwenyewe unajua Gamboshi jinsi inavyoshikilia 'balimi' kibao waliofariki kimiujizamiujiza, kitu gani Mkuu kinakufanya ushangae vijiuchawi vidogovidogo uwanjani?