Vyakula gani sipaswi kula endapo nina tatizo la acid reflux?

Vyakula gani sipaswi kula endapo nina tatizo la acid reflux?

mgagani2014

Member
Joined
Jun 2, 2014
Posts
9
Reaction score
3
Pia naomba kuuliza.
Parachichi
Apple
Ndizi mbivu
Wali
Ugali
Nyama
Maziwa mtindi
Maziwa fresh(boxed like asas and first choice)
Wine.
Mayai ya kukaanga au kuchemsha

Vitu gani Kati ya hivi sipaswi kutumia kabisa?

Maana nasumbuliwa na acid reflux na tumba kujaa ges.

MWENYE UFAHAMU NAOMBA ANIJUZE TAFADHALI.
 
Ndizi mbivu,maziwa mtindi kunywa kwa Kiasi,wali kwa Kiasi,parachichi kwa Kiasi na wine
 
Pia naomba kuuliza.
Parachichi
Apple
Ndizi mbivu
Wali
Ugali
Nyama
Maziwa mtindi
Maziwa fresh(boxed like asas and first choice)
Wine.
Mayai ya kukaanga au kuchemsha

Vitu gani Kati ya hivi sipaswi kutumia kabisa?

Maana nasumbuliwa na acid reflux na tumba kujaa ges.

MWENYE UFAHAMU NAOMBA ANIJUZE TAFADHALI.
Wapi wamajeua kua una hilo tatizo na hawajakupa maelezo jinsi ya kuishi nalo?
........hautakiwi kunywa maji
 
Pia naomba kuuliza.
Parachichi
Apple
Ndizi mbivu
Wali
Ugali
Nyama
Maziwa mtindi
Maziwa fresh(boxed like asas and first choice)
Wine.
Mayai ya kukaanga au kuchemsha

Vitu gani Kati ya hivi sipaswi kutumia kabisa?

Maana nasumbuliwa na acid reflux na tumba kujaa ges.

MWENYE UFAHAMU NAOMBA ANIJUZE TAFADHALI.

Pole sana.

Tatizo la acid reflux (GERD) na tumbo kujaa gesi huwa na visababishi vingi mfano ukiwa na maambukizi ya aina fulani ya bacteria wajulikanao kama H-pylori. Pia aina ya vyakula na mtindo wa ulaji huweza kuchangia hiyo hali kutokea.

Kwa hiyo ukiwa na tatizo hilo ni muhimu kwanza kwenda hospitali ili ukafanyiwe vipimo vya choo ili kama huyo mdudu, H-pylori ataonekana basi upatiwe dawa za kumuua.

Kama vipimo vipo kawaida basi ni muhimu kuepuka au kupunguza kula aina fulani ya vyakula ambavyo husababisha tatizo hilo kutokea baada ya kuvitumia. Hapa ni vigumu kutaja moja kwa moja vyakula vya kuepuka kwa sababu mara nyingi kila mtu kuna vyakula akila hupata/huchochea hiyo hali ya acid reflux (GERD). Kwa hiyo epuka au punguza kula vile vyakula ambavyo wewe mwenyewe unaona kuwa vinachochea hiyo hali ya acid reflux (GERD) kukupata.

Pia epuka kupanda kitandani/kulala muda mfupi baada ya kula. Inashauriwa ulale/upande kitandani walau saa 1 hadi 2 baada ya kula. Mara baada ya kula utumbo huzalisha acid nyingi kwa ajili ya kumeng'enya chakula kwa hiyo kulala mara baada ya kula husababisha acid reflux na hivyo kusababisha vichomi na kiungulia. Kukaa saa 1 hadi 2 baada ya kula huruhusu chakula kumeng'enywa na hivyo kupunguza tatizo la acid reflux.

Kama utafanya vyote hapo juu lakini bado hupati nafuu basi unaweza kwenda hospital kubwa wanapofanya vipimo vingine vikubwa vya kuchunguza mfumo wa chakula mfano OGD ili kubaini matatizo mengine yanayoweza kusababisha hiyo hali ya acid reflux (GERD).

Kila la kheri.
 
Pole sana.

Tatizo la acid reflux (GERD) na tumbo kujaa gesi huwa na visababishi vingi mfano ukiwa na maambukizi ya aina fulani ya bacteria wajulikanao kama H-pylori. Pia aina ya vyakula na mtindo wa ulaji huweza kuchangia hiyo hali kutokea.

Kwa hiyo ukiwa na tatizo hilo ni muhimu kwanza kwenda hospitali ili ukafanyiwe vipimo vya choo ili kama huyo mdudu, H-pylori ataonekana basi upatiwe dawa za kumuua.

Kama vipimo vipo kawaida basi ni muhimu kuepuka au kupunguza kula aina fulani ya vyakula ambavyo husababisha tatizo hilo kutokea baada ya kuvitumia. Hapa ni vigumu kutaja moja kwa moja vyakula vya kuepuka kwa sababu mara nyingi kila mtu kuna vyakula akila hupata/huchochea hiyo hali ya acid reflux (GERD). Kwa hiyo epuka au punguza kula vile vyakula ambavyo wewe mwenyewe unaona kuwa vinachochea hiyo hali ya acid reflux (GERD) kukupata.

Pia epuka kupanda kitandani/kulala muda mfupi baada ya kula. Inashauriwa ulale/upande kitandani walau saa 1 hadi 2 baada ya kula. Mara baada ya kula utumbo huzalisha acid nyingi kwa ajili ya kumeng'enya chakula kwa hiyo kulala mara baada ya kula husababisha acid reflux na hivyo kusababisha vichomi na kiungulia. Kukaa saa 1 hadi 2 baada ya kula huruhusu chakula kumeng'enywa na hivyo kupunguza tatizo la acid reflux.

Kama utafanya vyote hapo juu lakini bado hupati nafuu basi unaweza kwenda hospital kubwa wanapofanya vipimo vingine vikubwa vya kuchunguza mfumo wa chakula mfano OGD ili kubaini matatizo mengine yanayoweza kusababisha hiyo hali ya acid reflux (GERD).

Kila la kheri.
Daah hii OGD jinsi ya kupima asee
 
Daah hii OGD jinsi ya kupima asee

Ni kifaa/mashine maalumu ambayo ina kamera ambayo huingizwa kwenye kinywa na kuanza kumulika kinywa, koo la chakula hadi kwenye utumbo ili kubaini uvimbe, michubuko au madonda kwenye njia hiyo ya chakula. Ina uwezo wa kupiga picha na kuchukua sampuli kama inahitajika.
Ukienda tu hospital ambayo wana hicho kifaa utaona wanavyopima.
 
OGD nakifahamu vizur yan ila namna ya upimaji wake ndio umenishinda yan nilimpelekaga mshua kupima asee ye mwenyewe alishindwa hadi wakampiga sindano ya usingizi 😄. Ngoja nikapime tu bacteria H pyrol
 
Back
Top Bottom