Nafaka
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 12,154
- 31,246
Bagamoyo inauzwa mamba wa kufugwaSijawahi lkn nikionaga picha za nyama yake namtamani. Siku nitapoikuta nyama yake lzma nile.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Bagamoyo inauzwa mamba wa kufugwaSijawahi lkn nikionaga picha za nyama yake namtamani. Siku nitapoikuta nyama yake lzma nile.
Ukibahatika kumla panya hata ww hutoacha.[emoji28][emoji28][emoji28]Kwahyo mkuu panya unapiga fresh kabsa saizi na kuwasifia juu yaani
Wanabanika hapohapo? Nikionaga nyama yake iliyobanikwa aisee inaonekana si mchezo hiyo kitu.Bagamoyo inauzwa mamba wa kufugwa
Yah ukitaka unabanikiwaWanabanika hapohapo? Nikionaga nyama yake iliyobanikwa aisee inaonekana si mchezo hiyo kitu.
Nakumbuka nlipiga hii pichaNlikuwa bangalore masomoni, siku moja tumeenda study tour Goa, ni mji kama bagamoyo kwa huku. Ila ji mbali kama 1300km toka goa hadi bangalore. Tulivofika tukaingia kula. Mi nikaagiza fried rice ndo wali kidogo unafanana na wa kwetu ila mbaya balaa na kingfish, kuletewa nikawekewa na bakuli lingine pembeni, basi bwana ilikuwa usiku kwenye ka mwanga hafifu hivi saa nne za usiku mm nikamimina mchuzi wa samaki na filet ya samaki. Nikachukua na mchuzi mwingine nikamimina sasa wakati nakula namalizia nikawa nimemaliza nyama ya samaki, nikaenda kwenye lile bakuli dogo nile na kilichomo. Nlikutana na konokono wamejaaa. Nikatamani kujitapsha. Nikawamind balaa wenye hoteli. Pasi wakaomba msamha ila jamaa yangu kutoka malawi alikula konokono wale
Machizi tu hawa, wao aanakufa kama kumbikumbi halafu watusaidie sisi. Ama ndo wanataka kutuambukizaNakumbuka nlipiga hii pichaView attachment 1716520
Bila shaka ushakula.Yah ukitaka unabanikiwa
Story yako inatufundisha nini ?Nlikuwa bangalore masomoni, siku moja tumeenda study tour Goa, ni mji kama bagamoyo kwa huku. Ila ji mbali kama 1300km toka goa hadi bangalore. Tulivofika tukaingia kula. Mi nikaagiza fried rice ndo wali kidogo unafanana na wa kwetu ila mbaya balaa na kingfish, kuletewa nikawekewa na bakuli lingine pembeni, basi bwana ilikuwa usiku kwenye ka mwanga hafifu hivi saa nne za usiku mm nikamimina mchuzi wa samaki na filet ya samaki. Nikachukua na mchuzi mwingine nikamimina sasa wakati nakula namalizia nikawa nimemaliza nyama ya samaki, nikaenda kwenye lile bakuli dogo nile na kilichomo. Nlikutana na konokono wamejaaa. Nikatamani kujitapsha. Nikawamind balaa wenye hoteli. Pasi wakaomba msamha ila jamaa yangu kutoka malawi alikula konokono wale
khaa sio kweli mkuu duuhKuna nikikumbuka nachekaga sana,,, miaka hiyo utotoni songea uko kuna mdau wetu mmja kwao walikua wapo kama wanne ivi wanaosoma sasa kuna siku wenzake wamewai kuludi toka shule wakala ugali mboga wakamaliza alaf ukabakia ugali tupu sasa muhuni kaludi kakuta ugali tupu yaani jamaa akapenga kamasi akala na ugali yan ukimkumbusha mbak leo jamaa anachukia kinoma Dadek
😃😃😃 Kweli kabisa Mkuu jamaa alikula ugali na kamasi ila ulkua utoto tu itakuakhaa sio kweli mkuu duuh
Aaah Mzee wa kibao. Ulienda tena kwa Mzee kupata kingine? Maisha haya yana mengi ya kujifunza ikiwemo na vyakula vya aina tofautitofauti"Hata Nguruwe huwa ana swih mbele ya njaa ya kufa"
Hii kauli niliwahi kumsikia Fid Q kwenye moja ya nyimbo zake, kitambo kidogo.
Muda huo nakula ugali wa kengele, yani dereva wa sahani break mkeka.
Nilipo kuwa nausikia mstari huu, kila siku nilikua najisea kua hata iwe vipi sintokuja kula nguruwe, sababu jamii yangu, dini yangu hairuhusu kula nguruwe.
Miaka mingi imepita, ule ugali wa kengele umeota mbawa, nasasa ni mwendo wa asie fanya kazi na asile, yani ni Jitegemee sio makongo tena.
Katika kujitafutia mwenyewe riziki ndipo sasa nakubaliana na msemo wa fid q " hata nguruwe huwa anaswih mbele ya njaa ya kufa" baada ya kukutana na nyakati ngumu za utafutaji riziki (hususan chakula)
Leo nataka niwashirikishe, ama niwahabarishe vyakula vya ajabu nilivyo wahi kula, ambavyo sikutegemea kama nitakuja kula kwenye maisha yangu.
1- PANYA
Ebwana eh, Mndengereko ukitaka akunyime maji basi atambue kua wewe ni mla panya.
Kwetu panya aliwi kabisaa tena ni kinyaa, lakini mimi nimekula.
Nakumbuka ilikua mwaka 2018, nikiwa nachimba poli la Nacoja (inasomeka nakocha)
Kulikua kuna nyumba moja hivi, ya bibi yangu wa kimakua, huyu alikua mganga, nilikua nikitoka Nanhupo (ninapo ishi) lazima nipite hapo kijijini (Nacoja) kwa huyu bibi, nioge dawa ndio niingie polini (mgodini)
Mazoe hayo yalipelekea pale nyumbani kwa yule bibi nichukuliwe kama mwana ndugu, kwani nilipo kua nafika hapo nyumbani lazima nibebe vijizawadi.
Siku moja, nimetoka zangu polini mida ya jioni, jua lishazama, nikaona kwa muda huu siwezi kupata piki piki ya Nanhupo, nikaamua kulala pale kijijini kwa yule bibi yangu.
Hii si mara yangu ya kwanza kulala hapa. Ni nyumba kubwa yenye wanafamilia wengi, pia kuna mtoto mmoja wapo wa yule bibi ni lika langu, hivyo huyu bibi alikua anani chukulia kama mwanae tu.
Niliingia pele, nikamkuta dada mkubwa yuko jikoni anaandaa ugali, nikamsalimia, nikaingia chumbani kubadili nguo za kazi.
Mara haukupita muda mrefu, nikaitwa kwa ajili ya kula. Sahani yetu ilikua ya watu kama wanne hivi, akiwemo yule mtoto wa kiume wa yule mama na watu walio nizidi umri kama wawili hivi.
Kabla ya kuanza kula yule mshikaji wangu, akaniuliza "unaaliya mavala?" akimaanisha kua ninakula panya, nikamjibu ndio.
Neno mavala mimi nikahisi kaniuliza kama nina kula mbawala, hivyo nikamjibu ndio. Nikawanawa maji na show ikaanza.
Matonge kama manne matano, mara, mmoja wa wale wazee akazama ndani ya bakuli nakutoa kitoeo na kukiweka kwenye sahani, amadi nakuta panya katula, mkia huo.
Kidogo nitapike lakini nikajikaza kisabuni, kwanza nijiuliza kama nitanawa maji, wenyeji wangu wangenichukulia vipi? tena ukizingatia walisha niuliza. Nikaona sio poa, na mimi nika kamata wakwangu nikaweka pembeni. Kwa kweli nilijilazimisha mpaka nikammaliza.
Miaka miwili sasa tangu tukio hilo kupita, cha ajabu nimekua nawapenda panya kufikia mpaka nawalipaga watoto waende wakanichimbie huko mapolini.
Panya ananoga ukimkaanga na Mafuta kisha ukapata kachumbari na pili pili nyingi, mbele yako upo ugali wa muhogo.
Kwa hapa Tete panya anauzwa kwenye sahani kama samaki wa kukaanga, haiwezi pita week bila kula panya. Kiufupi panya ni mtamu na najuta kuchelewa kumjua.
2- CHURA
Hii ilikua huko huko polini Nacoja, tafauti ni kua huku sio kijijini bali ni porini.
Polini kula vitu vya ajabu haishangazi lkn si wote wanaokula vitu vya hovyo.
Binafs nilikua nina kinyaa sana kula vitu vya hovyo lkn kubanwa na njaa usiombe.
Kuna nyakati ufanyaji wetu wa kazi hupitiaga nyakati ngumu sana , hasa kiangazi, tena zaidi ni kuanzia mwezi wa kumi, kumi na moja na mwanzoni mwa mwezi wa kumi na mbili.
Narudi muda si mrefu
Mlipata wapi chanzo cha moto wa kumchoma nyani huyo?Hivi Kwanzaa kabla ya kushusha mistari Tanapa wanapita humu ?
Eeh bwana basi mi na wanangu wa manzese maisha yalitupiga dar wengine wakawa wanatafutwa kwa wizi tukaamua twende pori flani tuanze biashara ya kukamata nyani na kuwauza hii biashara hipo kwenye hicho kijiji halafu kuwashika ni simple tu kikubwa tulikuwa tunawaekea ugoro kwenye ndizi akielewa tunae
Basi bwana siku hiyo katika kukamata askari wanyamapori hao hapo tulikimbia kichizi mwenzangu mmoja alipigwa shaba ya mguu tulikuwa wanne watatu tukaendeleza mbio huku mwanangu mmoja akiwa amembeba nyani mgongoni tunakimbia ule msako ulikuwa mkubwa Sana ilitubidi tuishi kwenye pango kwa siku kadhaa tutulie maana tungetokea vijiji jiran tungeshikwa pia tungetokea ng'ambo nje ya msitu tungeshikwa
Sasa kibarua kinaanza hio sehemu ya pori tuliojificha imefunga Sana (closed canopy) kibaya vinyama vidogo huvioni hata matunda Hakuna mengine yalikuwa rangirangi tukaogopa kula pengine ya sumu basi tulimchuna Yule nyani tukamchoma tukala maana njaa ilizidi sasa
Daah na ile njaa ilitubidi tule nyani
MmmhKeki ya bamia
Nadhani wahuni hawakosi kiberiti Cha kuvutia Cha Arusha..Mlipata wapi chanzo cha moto wa kumchoma nyani huyo?