Pre GE2025 Vyama vya siasa nchini havina usawa, kuna dhaifu na vyenye nguvu. Hali hii inaweza kusababisha uchaguzi usiwe huru na wa haki

Pre GE2025 Vyama vya siasa nchini havina usawa, kuna dhaifu na vyenye nguvu. Hali hii inaweza kusababisha uchaguzi usiwe huru na wa haki

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Genius Man

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2024
Posts
1,012
Reaction score
2,317
Katika uhalisa ndani ya taifa letu chama tawala ndio chama chenye nguvu kuliko vyama vingine ambapo Mgawanyiko huu wa sehemu mbili yani dhaifu na nguvu unaweza kuondoa demokrasia, usawa na haki.

Hii ni tofauti na vyama vya siasa vilivyopo Marekani, ambapo huko vyama. Vyote vina usawa hata kama kimoja kikiwa madarakani vyote vina nguvu na sauti kwenye taifa hali inayopekea kila chama kupata haki na usawa hata kwenye chaguzi za nchi lakini hii ipo tofauti hapa Tanzania.

Katika uhalisia Tanzania chama tawala ndio kina nguvu kuliko vyama vingine hali inayoweza kuchangia kusiwepo na usawa ikiwemo kwenye chaguzi.

Kwa hiyo Ili tupate uchaguzi wa haki na wa kidemokrasia tunahitaji kwanza kutafuta usawa wa vyama vya kisiasa haijalishi kipo madarakani au hakipo madarakani hii ni muhimu kwa afya ya demokrasia yetu na hii ndio haki.
 
Poor analysis!! Lack of evidence, fallacy of generalization 🤔🤔🤔
 
Poor analysis!! Lack of evidence, fallacy of generalization 🤔🤔🤔
labda hujaelewa Ushahidi ndio huo "nguvu na dhaifu" hapa unaona kuna usawa kwenye hivi vitu viwili,

je, chama tawala nchini ndio kinanguvu kuliko vingine ? kama ni ndio hii inaweza kupelekea kusiwe na haki kwenye masuala mbali mbali ikiwemo chaguzi sijui umenielewa ?
 
Katika uhalisa ndani ya taifa letu chama tawala ndio chama chenye nguvu kuliko vyama vingine ambapo Mgawanyiko huu wa sehemu mbili yani dhaifu na nguvu unaweza kuondoa demokrasia, usawa na haki.

Hii ni tofauti na vyama vya siasa vilivyopo Marekani, ambapo huko vyama. Vyote vina usawa hata kama kimoja kikiwa madarakani vyote vina nguvu na sauti kwenye taifa hali inayopekea kila chama kupata haki na usawa hata kwenye chaguzi za nchi lakini hii ipo tofauti hapa Tanzania.

Katika uhalisia Tanzania chama tawala ndio kina nguvu kuliko vyama vingine hali inayoweza kuchangia kusiwepo na usawa ikiwemo kwenye chaguzi.

Kwa hiyo Ili tupate uchaguzi wa haki na wa kidemokrasia tunahitaji kwanza kutafuta usawa wa vyama vya kisiasa haijalishi kipo madarakani au hakipo madarakani hii ni muhimu kwa afya ya demokrasia yetu na hii ndio haki.
Mkuu una kitu cha ziada usipuuzwe.. Ulichosema kina ukweli mkubwa. Chama tawala kipo juu ya mamlaka zote.. Za nchi upinzani ni kama wanafanya drama...
 
Chama kinajichotea mapesa hazina, chama kinajimilikisha viwanja, majengo, nk. Chama kinajinunulia mabasi ya mabilioni na kuhonga wasanii mabilioni, kutumia nguvu ya serikali(polisi), kung'ang'ania katiba mbovu, kutumia madaraka kukandamiza na kutisha wapinzani, Leo hii kinawezaje kutoka madaakani kwa haki? Kimsingi tunapaswa kuvipongeza sana vyama vya upinzani kufanya kazi katika mazingira hayo! Pamoja na yote wanahitahidi mno!
 
Back
Top Bottom