Vyoo vya kuchuchumaa ni bora kuliko vyoo vya kukalia

Vyoo vya kuchuchumaa ni bora kuliko vyoo vya kukalia

Choo cha kuchuchumaa ni the best.. kiafyA... kwa kuwa unapochuchumaa Utumbo unakaa 90 degree.. ambayo ni nzuri kiafyA..
Kama unajenga/ umejenga nyumba weka choo cha kuchuchumaa kwenye master yako
 
NB: Haihusishi walemavu ambao inabidi wavitumie vyoo vya kukalia.

Kiukweli linapokuja suala la kwenda haja, choo cha kuchuchumaa ni kizuri zadi kuliko cha kukaa..

1. mkao wa Mchuchuma ndio pozi la asili kwajili ya kutoa haja kwa ufanisi wa hali ya juu, njia ya haja linafunguka zaidi pale tunapochuchumaa, na hii ndio sababu kuu ya kwenda haja kwa kuchuchumaa.

2. kuchuchumaa ni zoezi ambalo ni zuri kiafya kulifanya mara moja moja si mbaya kwajili ya nguvu za magoti, kunyoosha mgongo, n.k.

3. Choo cha kukaa, kinyesi huwa kinatua moja kwa moja kwenye tundu lenye maji, kero hapa ni pale kinyesi kikiwa kizito au kikubwa kikitua yale maji huwa yanaruka na kumfikia mtumiaji kwenye sehemu za kutoa haja, hii ni hatari kiafya.

4 choo cha kukalia ni vema ukitumie mwenyewe ama wawili mke na mme kwa kuzingatia usafi na afya, si vizuri kitumike na wengi kwasababu zifuatazo:
  • mtu akikaa kuna ule mgusano wa mapaja na choo unaweza kupelekea magonjwa ya ngozi,
  • mtu anapokaa anaweza kuliacha jasho lake sehemu ya kukaa,
  • mtumiaji akikojoa huwa kuna matone ya mikojo yanaweza kudondokea sehemu ya kukaa,

5. Choo cha kuchuchumaa unaweza kujisafisha kirahisi kuliko choo cha kukaa.
Vyote ni vyoo vizuri tu kulingana na wewe au watumiaji wanavyo kihandle, nina miaka mingi natumia choo cha kukaa sijaona tatizo
 
Nimebakia nacheka tuuu khaaaa mada hiii chibokooo
 
Vyoo vyote ni bora tofauti ni kipi umekizoea ukizoea cha kukaa(European type) basi cha kuchuchumaa( Asian type)kitakupa shida kukizoea cha muhimu nikuzingatia usafi sana cha mwisho kwa mazingira yetu cha kukaa kina itaji watu wawili au mmoja kwa matumizi sio vyema kuwekwa public
Huwa Unajitawazeje Choo cha Kukaa?
 
Back
Top Bottom