KERO Vyoo Vya Umma Kukosa Sabuni na Toilet paper

KERO Vyoo Vya Umma Kukosa Sabuni na Toilet paper

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

povour3

Senior Member
Joined
Dec 11, 2019
Posts
177
Reaction score
638
Hakika ni jambo la aibu,dhihaka,ujinga na kukosa ustaarabu na wakati huo huo tukijiona jamii yenye ustaarabu na Elimu.

Maeneo yenye mkusanyiko mkubwa wa watu,wenye kutafuta huduma au kupatiwa huduma mfano zahanati,vituo vya afya,hospitali(wilaya,mkoa na rufaa), Taasisi za Elimu(shule za msingi, sekondari,vyuo vya ufundi,Kati na vyuo vikuu),Vituo vikuu na vidogo vya mabas,Masoko n.k

Ukibahatika kutembelea maeneo hayo kwa shughuli mbalimbali unaweza kubanwa na haja kubwa au ndogo,hivyo basi lazima uhitaji huduma ya choo iwe ya kulipia au bure.

Kilicho fanya niandike Uzi huu ni hii,sijui niite tabia au desturi ya kipumbavu kabisa ambayo ilipaswa kufanywa na watu wapumbavu,maana mtu mwenye akili timamu hawezi Weka huduma choo iwe ya bure au kulipia alafu akashindwa kuweka Sabuni au toilet paper.

Mfano mtu akijisadia haja kubwa anaweza tumia maji au toilet paper,kiafya inashauri baada ya kukataa gogo,mtu huwa na machaguo mawili atumia maji au toilet paper na baadaye kunawa mikono kwa maji Safi na sabuni.

Sasa inakuaje maeneo ya umma mengi yana vyoo,lakini hakuna Sabuni na Toilet paper ? Na mbaya zaidi Kuna taasisi muhimu zenye jukumu la kutoa matibabu kwa watu,lakini ukienda kwenye vyoo hakuna Sabuni Wala toilet paper na Kuna wakati hata huduma ya maji hakuna kabisa.

Jambo hili hata mwandishi wa habari bwana Denis Mpagaze katika kitabu chake cha "Wasomi Huru Gerezani" anashangaa taasisi kama vyuo vikuu kukosa Sabuni kwenye vyoo.

Jambo hili lina kera na linafanya jamii yetu ionekane kituko kwa jamii zenye ustaarabu.

Rai yangu kwa serikali,umma na mtu binafsi,tubadilike.
 
Usitumie vyoo vya umma.

Hata vikiwa na sabuni na toilet paper SIO SALAMA

Utakuja kunishukuru
Mfano mtu unasafiri na umebanwa na haja unafika kituo Cha mabasi kwa ajili ya kuchimba dawa utafanyaje? Au mgonjwa ambaye yuko hospitali au kituo Cha afya kupatiwa huduma unataka atumie vyoo au choo Cha wapi ?
 
Mfano mtu unasafiri na umebanwa na haja unafika kituo Cha mabasi kwa ajili ya kuchimba dawa utafanyaje? Au mgonjwa ambaye yuko hospitali au kituo Cha afya kupatiwa huduma unataka atumie vyoo au choo Cha wapi ?

TUMIA VYOO VYA KULIPIA

Vina afadhali
 
Hakika ni jambo la aibu,dhihaka,ujinga na kukosa ustaarabu na wakati huo huo tukijiona jamii yenye ustaarabu na Elimu.
Maeneo yenye mkusanyiko mkubwa wa watu,wenye kutafuta huduma au kupatiwa huduma mfano zahanati,vituo vya afya,hospitali(wilaya,mkoa na rufaa), Taasisi za Elimu(shule za msingi, sekondari,vyuo vya ufundi,Kati na vyuo vikuu),Vituo vikuu na vidogo vya mabas,Masoko nk

Ukibahatika kutembelea maeneo hayo kwa shughuli mbalimbali unaweza kubanwa na haja kubwa au ndogo,hivyo basi lazima uhitaji huduma ya choo iwe ya kulipia au bure.

Kilicho fanya niandike Uzi huu ni hii,sijui niite tabia au desturi ya kipumbavu kabisa ambayo ilipaswa kufanywa na watu wapumbavu,maana mtu mwenye akili timamu hawezi Weka huduma choo iwe ya bure au kulipia alafu akashindwa kuweka Sabuni au toilet paper.

Mfano mtu akijisadia haja kubwa anaweza tumia maji au toilet paper,kiafya inashauri baada ya kukataa gogo,mtu huwa na machaguo mawili atumia maji au toilet paper na baadaye kunawa mikono kwa maji Safi na sabuni.

Sasa inakuaje maeneo ya umma mengi yana vyoo,lakini hakuna Sabuni na Toilet paper ? Na mbaya zaidi Kuna taasisi muhimu zenye jukumu la kutoa matibabu kwa watu,lakini ukienda kwenye vyoo hakuna Sabuni Wala toilet paper na Kuna wakati hata huduma ya maji hakuna kabisa.

Jambo hili hata mwandishi wa habari bwana Denis Mpagaze katika kitabu chake cha "Wasomi Huru Gerezani" anashangaa taasisi kama vyuo vikuu kukosa Sabuni kwenye vyoo.

Jambo hili lina kera na linafanya jamii yetu ionekane kituko kwa jamii zenye ustaarabu.

Rai yangu kwa serikali,umma na mtu binafsi,tubadilike.
Nilisha sema before. Kufanya kazi taasisi za umma ni raha sana. Hamna accountability.
 
Kukojoa kichakani ni salama zaid ya kukojoa kwenye vyoo vya umma ..sija zungumzia kukata gogo wadau
 
Kama hauna ulazima we vumilia tu maana utabeba magonjwa kwenye hivyo vyoo utajutia
 
Kama hauna ulazima we vumilia tu maana utabeba magonjwa kwenye hivyo vyoo utajutia
Mkuu jambo hili sio binafsi,bali linamgusa kila mtu,kama halikugusi wewe tambua wazi kuwa Kuna mtu wa karibu y'ako linamgusa.
 
Back
Top Bottom