Vyumaa: Leo nimemuona tajiri anagawana sh elfu tano na familia!

Nichumu Nibebike

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2016
Posts
8,658
Reaction score
15,793
Sikuamini macho yangu.. Huyu jamaa ni tajiri mkubwa mtaani petu.. Sasa kaja na gari lake mpaka dukani, mlango wa mbele ukafunguliwa akashuka binti yake kuja kuomba chenji ya elfu tano dukani ili wagawane; familia ipate pesa ya mboga na baba abakie na pocket money.
Sikuamini macho yangu, nilikuwa na stress za ukata ila ghafla nikajikuta nafarijika...
 
Kwa hiyo umefurahi?
 
Mawazo ya kimaskini haya,ndiyo maana sisi weusi tunadharaulika.huwezi kuwa timamu halafu ukashangilia shida za mwenzako,tuupige vita umaskini wa mawazo kwani unazaa kizazi kisichokuwa hata na huruma.
 
Rekebisha kichwa cha habari mdada,nimekuja mbiombio nikijua jamaa anagawa 5k kitaa ngrrrrrr.
 
Hujiulizi kwanini kachenji hio hela na nani kakuambia ndio the only cash walikua nayo? Mafuta ya gari unawajazia wewe? Sio kila mtu vyuma vimekaza ndugu, tupo kibao tunao ishi vizuri kuliko wakati wowote.
 
nyie ndo mnaofurahia vyuma kukaza eti matajiri watafilisika
ila kumbuka hata huyo tajiri akifilisika hamuwezi kuwa sawa
 
Acha Umbeya Mkuu.
 
Kumesaidia nini kuchunguza maisha ya MTU mwingine?
 
Hongera mkuu kama rais angeongoza vizuri maana yake ungekuwa juu ya hapo.
Hujiulizi kwanini kachenji hio hela na nani kakuambia ndio the only cash walikua nayo? Mafuta ya gari unawajazia wewe? Sio kila mtu vyuma vimekaza ndugu, tupo kibao tunao ishi vizuri kuliko wakati wowote.
 
Hongera mkuu kama rais angeongoza vizuri maana yake ungekuwa juu ya hapo.
Kabisa, kilicho ikost nchi ni kwamba Raisi ana akili kama za huyu mtoa mada, kutamani matajiri waishi kama mashetani, asicho jua ni kwamba ukimbana tajiri, anapunguza uzalishaji na gharama kwa kupunguza wafanyakazi na kupunguza manunuzi ya luxuries, mwishowe wanao isoma namba wanabaki kuwa wale wale wanyonge ambao alidhani anawatetea.... Sasa hivi ardhi vijijini inauzwa bei ya kutupwa, walala hoi wanauza ekari hadi laki tano wakalipe ada za watoto. Mwishowe maskini wanazidi kumaskinika zaidi
 
Mawazo ya mafukara
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…