Ukweli ni kwamba vyuo vya private vipo ambavyo vinawaanda wanFunzi vizuri kabisa lakini jamii ya kitanzania kwa upande wa elimu ya juu wana imani na vyuo vya serikali zaid kuliko vya private. Tofauti na ilivyo kwa elimu ya sekondari.
Wanafunzi wa sekondari za private waliofaulu ni nadra sana kumkita chuo cha private ndio ujiulizesekondar mzazi alipambana mwanae asisome govt bt chuo vice versa. Mfumo wa upataji walimu wa chuowanabebwa the best je skondari ikoje?
hoja hii sikutaka kuichambua kwa sababu ya kuchosha wasomaji, ninaelewa mambo mengi sana katika misingi ya hoja nyingi ambazo nyingi hazizungumzi ukweli bali ni imani.
nitaeleza kwa kifupi sana ila nikilazimika naweza kutoa maelezo ya kina kwenye hoja yako.
1.kwanza watanzania wengi ni maskini na hakuna anayependa kuendelea kuwa maskini.
2.pili wazazi wengi wanaosomesha watoto wao shule za binafsi si watu tajiri ila wengi wana maisha ya kati kama walimu,manesi,wakulima,wafugaji nk. ila tofauti ni kwamba hawa wanakuwa wanaelewa umuhimu wa mtoto kusoma shule nzuri. na wazazi wengi sana wanajitahidi sana kutumia nyenzo zote ili angalau mtoto afikie kidato cha sita na baada ya hapo mzazi anajua mtoto wake atapata kusomeshwa na serikali chuo kikuu na hivyo mzazi hatakuwa na mzigo tena.
kwa taarifa tu ni kwamba wapo wazazi wengi sana wanafilisika kisa kumsomesha mtoto O level peke yake na akishindwa kufaulu kwenda serikalini wazazi haohao wanakuwa hawana tena uwezo wa kumpeleka private mtoto yule kwa sababu kama ni mashamba wameuza yote. wengine wanakuwa na nguvu ya kiuchumi inayoishia form six ambapo familia inakuwa haina tena uwezo wowote wa kuchangia hata kiasi kidogo cha ada ya chuo.
hoja yangu hapa ni kwamba wazazi wengi na hata wanafunzi ni maskini na malengo yao ni kutafuta unafuu wa gharama chuoni ambapo serikali inatoa mkopo na si ubora wa vyuo vya serikali ama ubovu wa vyuo vya private ndio hufanya wazazi wengi waseme mtoto wao akasome udsm, na hapa ndipo nilipinga mfumo wa HELSB kupanga asilimia za mikopo kwa kungalia kama mwanafunzi alisoma private=tajiri ama alisoma serikali=masikini, kuna watu wanasomesha private kwa kujikamua na mpaka mtoto anamaliza shule nyumbani ashakomba kila kitu.
ok, nisitoke nje ya hoja yako.
najua kuwa mikopo inatolewa hata vyuo vya private, but how informed the society is? ukweli ni kwamba jamii kwa kiasi kikubwa haielewi kama na wanafunzi wa private wanapata mikopo, hivyo wanaelewa huko mikopo haitolewi alafu kumbuka hapo wanatafuta unafuu wa gharama, unafikiri choice itakuwa nini?
ukweli mwingine ni kwamba ada za vyuo vya private ni kubwa kwa kiasi kikubwa na inapotokea mikopo si asilimia mia linakuwa tatizo jingine na hapo hata wanaoelewa hivyo vyuo wanavikwepa kwa sababu ya gharama. na kumbuka wengine wamemaliza kila kitu huko sekondari.
kihistoria pia inajulikana tangu zamani kuwa chuo unalipiwa gharama na hivyo wazazi wengi wanajua mtoto wao akienda chuo cha serikali anapata nafuu.
MASWALI KWAK
1.wewe wazazi wako wanaelewa dhana ya ubora wa vyuo vya serikali na dhana ya ubovu wa vyuo vya private? mimi wa kwangu hawaelewi na hakuna hata mmoja alishaona hata chuo kimojawapo kati ya vyuo vya serikali lakini huko waliko wanajua kuna chuo kikukuu kinaitwa MLIMANI, je walipotaka nisome mlimani ilikuwa kwa sababu ya ubora ama kwa sababu ndicho chuo pekee walichokuwa na wamezoea kukisikia toka ujana wao?
2. ni watanzania wangapi leo wamebahatika tu kufika na kuona chuo cha mlimani? iwe wamesoma ama walipita tu kama wanatembea? je kwa mkutadha huo ni wazazi wangapi kati ya wengi wanaopenda watoto wao wasome UDSM wana uelewa thabiti na chuo cha mlimani?
ukiniuliza mimi nitakwambia kuwa pamoja na kwamba ni ukweli usiopingika kuwa wengi wa wazazi wanapenda watoto wao wasome UDSM(na si vyuo vya serikali vyote kama hoja yako) UKWELI ni kwamba wengi kati ya hao wazazi hawaelewi chochote kuhusu dhana ya ubora wa udsm kama wengi tunavyofikiria, ila wanajua hicho ndio chuo kikuu na vingine hawaelewi kama ni vyuo sawa na udsm tena wengine hata ukiwatajia UDOM bado hawakuelewi. pia wapo wengi wanataka watoto wao wakasome mlimani lakini hao wazazi hata Dar es salaam hawakuwahi kufika,SO SHORT NI KWAMBA UDSM IS A POPULAR UNIVERSITY IN TANZANIA DUE TO HISTORICAL REASONS. niishie hapa i am not ok hata kupangilia hoja inakuwa ngumu. ila unaweza kutafakari haya maelezo na kama una hoja zingine just raise japo sitajibu sasa my brain is very tired mana kuichambua rasimu ni kazi ngumu na imechosha sana akili yangu.