Sijui kama wengine mlikuta mambo haya,chakula kilikuwa kinagawiwa kwa mtu aliye na foodcard.hiyo foodcard ilikuwa inatolewa kwa mtu aliyesomba maji ya kupikia ndoo kadhaa.Ole wako uende dining Hall(DH) bila foodcard halafu mlangoni ukutane na kiongozi wa DH aitwaye Mwakalindile A.K.A Never look,hapo siku hiyo itakuwa imekula kwako.Uji wenyewe ulikuwa unagawiwa saa kumi za usiku,kuna watu toka bweni la shabani Robert walikuwa mabingwa wa kuamka mapema. wakishamaliza uji jikoni ndio wanapiga kengere ya kuamsha watu waende kwenye uji.Pale wanakutana na surprise mpisha anaosha sufuria la uji.Mnakumbuka pia pale ARTIST CORNER?,pale ilikuwa mwisho wa maneno ,hasa katuni ya KAMJINGIJINGI.