Waafrika kwa sasa wanazalisha vyao kwa ajili yao?

Waafrika kwa sasa wanazalisha vyao kwa ajili yao?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Kama ulifanikiwa kusoma hadi Sekondari, na ulikuwa na Mwalimu mzuri wa Historia kama Mwalimu wetu, unaweza ukawa unaikumbuka hii kauli:" We produce what we do not consume and consume what we do not produce". Kwa tafsiri isiyo rasmi inaamisha hivi:"Tunazalisha tusichokitumia na kutumia tusichokizalisha".

Hiyo tulikutana nayo Form Two, kama sikosei. Ni mojawapo ya sababu iliyopelekea kuibuka kwa vuguvugu la kudai uhuru. Waafrika walichoka kuzalisha wasichokitumia, na kutumia wasichokizalisha.

Madhalani, kwa Tanzania, watu walilazimishwa kuotesha mazao ya biashara ambayo hatimaye yalisafirishwa kwenda viwandani Ulaya, na Waafrika wakaletewa bidhaa kama nguo n.k., toka viwanda vya Ulaya.

Kwa hiyo, Afrika ikawa mahali pa kuzalishia "raw materials" na pia kama soko la bidhaa za viwanda vya Ulaya.

Ikiwa ni miaka mingi tangu nchi za Kiafrika zijinasue kutoka katika makucha ya utawala wa Wakoloni, kuna utofauti wowote?

Je! Inazalisha inachozalisha kwa ajili yake au bado ni kwa ajili ya watu wa ng'ambo? Bado ni chanzo cha raw materials na soko la bidhaa za nchi za mabara mengine?

Ni nani anayeconsume "madhahabu" yetu?

Nani anayeyatumia "maalmasi" zetu?

Nani anayeyafaidi "Matanzanite" yetu?

Mbona bado zinaenda kwa watu weupe? Sisi hatujui kuyatumia? Hatuyapendi? Tunayaogopa? Hatuyajui matumizi yake?

Ukiacha mazao ya chakula, ni kipi tunachokizalisha kwa ajili yetu wenyewe? Magari, simu, silaha, madawa, makompyuta, zana za kilimo, n.k., kwa asilimia nyingi zinatoka hukoo!

Pamoja na kuwa nchi zetu ni huru, mbona kama bado tunaconsume what we do not produce na kuproduce what we do not consume?
 
Mchango wako ni upi ukitoa kulalamika? Wewe usha anza kuzalisha nini? Hii nchi kuna vituko saana
Labda sijakuelewa mkuu!

1. Ni wapi nilikolalamika?

2. Uzi unaziongelea nchi za Afrika na si mtu mmoja mmoja. Nijibu kwa niaba ya nchi ya Tanzania au bara la Afrika?
 
"Bajeti hii (mapendekezo ya bajeti kuu ya serikali kwa mwaka wa fedha 2024/25 iliyowasilishwa Bungeni na Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba hivi karibuni) ina maana gani kwa Mtanzania wa kawaida?, je kuanzia mwezi Julai 2024 hali ya maisha ya Watanzania itakuwaje?, serikali imependekeza kuanzisha kodi katika mazao ya kilimo na mifugo serikali imeendelea kuwakamua wakulima na wafugaji kwa kuanzisha kodi katika mifugo na wakulima, serikali imeanzisha tozo ya asilimia 2 kwa wachimbaji wadogo, mbali na malipo mengine wanalipa kodi ya madini (mrabaha) 6%, ushuru wa ukaguzi 1%, ushuru wa huduma 7.3% ambazo zote zinatoka kwenye mauzo ghafi, kwa ujumla bajeti ya mwaka 2024/25 itapelekea maisha ya mwananchi wa kawaida kuwa magumu zaidi kwa sababu gharama za maisha zitaendelea kupanda na kipato kupungua, sera za bajeti zimeshindwa kutazama bajeti kama sera (policy instrument) na badala yake imekuwa nyenzo tu ya kukusanya mapato na kuyatumia"
 
Watanganyika waliambiwa kuwa Mzungu ni mbaya kwa kuwa anatoza Kodi. Matokeo yake, mpaka leo hii ukusanyaji kodi ni kwa mbinde!
Waliaminishwa sababu za kipumbavu kabisa sijui kodi,unyonyaji sijui viboko sasa jitu halitaki kazi linaachwaje sasa lisilambwe viboko.Halafu mzungu hakutegemea kodi kuendesha nchi aliitoza ili watu wafanye kazi.
 
Kama ulifanikiwa kusoma hadi Sekondari, na ulikuwa na Mwalimu mzuri wa Historia kama Mwalimu wetu, unaweza ukawa unaikumbuka hii kauli:" We produce what we do not consume and consume what we do not produce". Kwa tafsiri isiyo rasmi inaamisha hivi:"Tunazalisha tusichokitumia na kutumia tusichokizalisha".

Hiyo tulikutana nayo Form Two, kama sikosei. Ni mojawapo ya sababu iliyopelekea kuibuka kwa vuguvugu la kudai uhuru. Waafrika walichoka kuzalisha wasichokitumia, na kutumia wasichokizalisha.

Madhalani, kwa Tanzania, watu walilazimishwa kuotesha mazao ya biashara ambayo hatimaye yalisafirishwa kwenda viwandani Ulaya, na Waafrika wakaletewa bidhaa kama nguo n.k., toka viwanda vya Ulaya.

Kwa hiyo, Afrika ikawa mahali pa kuzalishia "raw materials" na pia kama soko la bidhaa za viwanda vya Ulaya.

Ikiwa ni miaka mingi tangu nchi za Kiafrika zijinasue kutoka katika makucha ya utawala wa Wakoloni, kuna utofauti wowote?

Je! Inazalisha inachozalisha kwa ajili yake au bado ni kwa ajili ya watu wa ng'ambo? Bado ni chanzo cha raw materials na soko la bidhaa za nchi za mabara mengine?

Ni nani anayeconsume "madhahabu" yetu?

Nani anayeyatumia "maalmasi" zetu?

Nani anayeyafaidi "Matanzanite" yetu?

Mbona bado zinaenda kwa watu weupe? Sisi hatujui kuyatumia? Hatuyapendi? Tunayaogopa? Hatuyajui matumizi yake?

Ukiacha mazao ya chakula, ni kipi tunachokizalisha kwa ajili yetu wenyewe? Magari, simu, silaha, madawa, makompyuta, zana za kilimo, n.k., kwa asilimia nyingi zinatoka hukoo!

Pamoja na kuwa nchi zetu ni huru, mbona kama bado tunaconsume what we do not produce na kuproduce what we do not consume?
"Let us agreed that Blacks cannot rule themselves, Whites are born in order to rule and Blacks are born to be ruled."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era
 
Waliaminishwa sababu za kipumbavu kabisa sijui kodi,unyonyaji sijui viboko sasa jitu halitaki kazi linaachwaje sasa lisilambwe viboko.Halafu mzungu hakutegemea kodi kuendesha nchi aliitoza ili watu wafanye kazi.
Laiti Wajerumani wangeikalia Tanganyika hadi mwaka 2000, leo hii Tanganyika ingekuwa ya kitofauti! Inawezekana wengi wetu tusingekijua Kiswahili, lakini tungekuwa na faida nyingine nyingi lukuki:
1. Uchapa kazi
2. Uaminifu
3. Mfumo bora wa Elimu
4. Miundombinu ya uhakika
5. Good managerial skills
6. Viwanda vikubwa
7. Mipango miji ya uhakika
8. Treni za umeme, n.k.
 
Laiti Wajerumani wangeikalia Tanganyika hadi mwaka 2000, leo hii Tanganyika ingekuwa ya kitofauti! Inawezekana wengi wetu tusingekijua Kiswahili, lakini tungekuwa na faida nyingine nyingi lukuki:
1. Uchapa kazi
2. Uaminifu
3. Mfumo bora wa Elimu
4. Miundombinu ya uhakika
5. Good managerial skills
6. Viwanda vikubwa
7. Mipango miji ya uhakika
8. Treni za umeme, n.k.
"Let us agreed that Black people cannot rule themselves, Whites are born in order to rule and Blacks are born to be ruled."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era.
 
Back
Top Bottom