Waafrika tujitambue kwenye hizi dini Uislam na Ukristo

Waafrika tujitambue kwenye hizi dini Uislam na Ukristo

Dini ni Imani ya binadamu kuhusu roho na uumbaji, hujumuisha maadili na miiko ya kufuatwa na jamii inayofuata dini husika Ili kujenga jamii bora. Ipi ni dini bora? Hapa uamuzi hutokana na fikira za mtu anayeamua dini bora ni ipi Kati ya zote zilizopo duniani lengo likiwa ni lile lile, kujiweka sawa kiroho.
 
Sahihi mkuu watu wanazungumzia dini za mababu ila hawajui kuwa walichokuwa wakikifanya hao mababu ni uchawi
Wasukuma hio dini hawaiachi nasikia akijenga nyumba inaweza kua kubwa ila kuna kakibanda kanajengwa kwa nje kale kakibanda ndani katikati kinawekwa chungu, ni dini za jadi ni mila ni desturi ni tamaduni
 
Dini ni Imani ya binadamu kuhusu roho na uumbaji, hujumuisha maadili na miiko ya kufuatwa na jamii inayofuata dini husika Ili kujenga jamii bora. Ipi ni dini bora? Hapa uamuzi hutokana na fikira za mtu anayeamua dini bora ni ipi Kati ya zote zilizopo duniani lengo likiwa ni lile lile, kujiweka sawa kiroho.
Dini za jadi zinaonekana local sababu hazina kitabu maalum na hazina kitabu kwa hio zinaonekana km uchawi au ushirikina tu unapewa miiko usifanye hivi na usifanye vile fanya hivi fanya vile kunywa maji kwa wingi nenda ukapigwe risasi kinjeketile
 
Hizo mnazooziita dini za mababu ukizifuatilia kiundani zaidi utakuta ni ushirikina tu, mwisho wa siku lazima uwe mchawi
Sio kweli huu ni uongo kabisa, mbona kuna watu wanashinda na kulala makanisani na misikitini lkn ni wachawi wa kutupwa na ushahidi upo.

Dini hizi za kuletewa hazimfanyi mtu aache dhambi tunaona hata humu jinsi wafuasi wa hizo dini wanavyochuana kwenye ligi ya matusi na kukashifiana.

Hizi dini hazina tofauti na vyama vya siasa na ndio maana siku hizi vijana wengi wanaachana nazo na kubaki kuamini Mungu bila kufuata imani za dini.
 
Katika bara la Afrika dini hizo zinaegemea zaidi kwenye matambiko kwa mizimu ya ukoo ili isaidie jamaa zao.

Siku hizi idadi ya wafuasi wa dini hizo inazidi kupungua na kuziachia nafasi dini za kimataifa, hasa Ukristo na Uislamu.

Hata hivyo mabaki ya imani ya asili yanawaandama waliojiunga na dini hizo, hasa kwa namna inayotazamwa nazo kuwa ushirikina.

Dini za jadi ni dini za mababu ambazo zinafuata miiko na maadili halisi ya taifa au kabila fulani.
Hizi dini za Kiafrica ndo za kukakaa kwenye makutano ya barabara mkitambika kisha kutoa kafara za watu?

Upuuzi mtupu
 
WaAfrica dini zetu ni Upendo, Ujasiri, Ushirikiano, Amani na Kuridhika.

Uislam na Ukristo ni dini za Warabu/Wazungu na Watumwa.
 
Hizi dini za Kiafrica ndo za kukakaa kwenye makutano ya barabara mkitambika kisha kutoa kafara za watu?

Upuuzi mtupu
Sio kweli hizi ni propaganda mlizopewa na hao waliowaletea tamaduni zao na kuwadanganya kwamba ni dini.

Wakawadanganya kwamba ili uende mbinguni ni lazima utumie majina yao na hata mavazi uvae kama wanavyovaa wao na hata lugha uongee yao, yaani ujinga mtupu.
 
WaAfrica dini zetu ni Upendo, Ujasiri, Ushirikiano, Amani na Kuridhika.

Uislam na Ukristo ni dini za Warabu/Wazungu na Watumwa.
Usiwasingizie, waarabu halisi (mabedui) hawakuwa na dini walikuwa kama wewe (wapagani), walikuwa na miungu 360 waliyoiabudu pale Makka.

Awali kulikuwa na utamaduni wa kiyahudi ambao leo ndiyo tunaita dini ya kiyahudi. Ibrahimu alimkimbia baba yake kwa sababu ya kuabudu sanamu, alipokuwa Kanani ndipo alipotokewa na Mungu. Dini ilianza kwa mkataba wa Mungu na Musa ilipopewa Taurati (hiyo ndiyo dini ya kwanza). Dini ya pili ni Yesu alipokuja kama Neno la Mungu na kuanzisha Ukristo (maana yake kupakwa mafuta) ndiyo maana anaitwa Masihi. Dini lazima iwe na kitabu chake kama mkataba wa Mungu na watu. Ibrahimu alitokewa na Mungu akafanya Ibada lakini hakuanzisha dini kwa sababu hakupewa kitabu ila Imani na Ibada yake ndiyo iliyorithiwa na uzao wake baadaye na kuwa sehemu ya Madhehebu ya dini hizi. Uislam umechukua/kuacha yaliyomo kwenye Taurati (siyo yote) na pia umechukua/kuacha yaliyomo kwenye Biblia na kuunda huu Uislam.

MHMD maana yake 'mpakwa mafuta', au 'mpendwa wangu' na hilo siyo jina la mtu. Ndiyo maana pale Yerusalem kwenye Dome of the Rock haijaandikwa habari ya Mtume Muhammad kwenda kuonana na Mungu, ingekuwa ni kweli tukio hilo lingeandikwa mle ndani. Ikumbukwe Dome of the Rock imejengwa baada ya kufa Mtume Muhammad, hivyo tukio kubwa kama hilo lazima lingeandikwa humo. Kilichoandikwa humo ni ile shahada ambayo kama nilivyosema neno MHMD maana 'Mpakwa mafuta' au 'Mpendwa wangu', watawala wa nyakati hizo walikuwa wanajipa hadhi ya kuwa wao ni wateule wa Mungu na hivyo wanahadhi ya kuitwa Masihi wa Mwenyezi Mungu kama kina Daud na Suleiman n.k. hivyo hata Khalifa Abdul Malik aliyejenga Dome of the Rock aliandika hivyo na alianzisha pia sarafu aliyoweka msalaba. Historia sahihi inasema uzao wa Ibrahim ndiyo uliohitilafiana (Ishmael na Isack) na kuwa dini hizi mbili, lakini wote ni WAYAHUDI kwa asili na walitawanyika bara lote la Arabia na waliwakuta Mabedui wako huko wakiwa na upagani wao.
 
Mungu yupi?
Kwani wapo wangapi?
Kuna hoja humu ilitolewa na member akashauri wale wanaoamini katika dini hizi za kigeni wakae kwanza waelewane kuhusu tofauti zao juu ya Mungu ndipo wawashawishi wasiozifuata dini hizi. Hoja hii kwangu inamashiko pale ninapowaza ni kwanini kila upande wa dini hizi za kigeni huuona upande wa pili kuwa hautapata ufalme wa Mungu.
Tafsiri yake ni kwamba hizi dini Zina utapeki ndani yake wa kutaka kulazimisha watu waamini katika upande wake kuwa ndiko Kuna Mungu na hapo ndipo ukiwa na fikira pevu utakiona chanzo cha huo utapeki.

PLO Lumumba katika hotuba zake aliwahi kusema kwamba "kama Mungu alimuumba Binadamu kutoka katika udongo, udongo unafanana na rangi ya watu Gani hapa duniani?" na akaongeza kuwa "Mungu ni roho ambayohaiwezi kufinyangwa finyangwa na Binadamu Bali kuabudiwa katika makundi mbali mbali ya wanadami kwa tratibu zao".

Hivyo dini haipaswi kuabudiwa Bali Mungu ndiye.
 
Ukristo unamtaja mungu kama roho,na kwa kuwa ni roho macho ya nyama hayawezi kumuona.Mungu huyu hujidhihirisha kwa wanadamu kwa namna mbili:ANTHROMORPHIC-Mungu anavaa mwili wa binadamu(incarnate) na kuishi nao mpaka muda wake utakapotimia anaondoka.THERIOMORPHIC-Mungu anajidhihirisha kwa vitu vingine.Kwa kuwa mungu huhitaji patulivu kujidhihirisha:chini ya mti,pembeni ya jiwe,pembeni ya mto,chini ya mlima au pango yote haya ni maeneo tulivu(sanctuary) kwa iba(tambiko).Kujenga makanisa,misikiti,masinagogi ni matokeo ya binadamu kubanana na kuathiri mazingira asili.Unayemtuhumu mwafrika kuabudu chini ya mti,mlima,jiwe nk.wajua unachokiongea kweli?
 
Kwahio unamtunguliza mungu yupi..? Huyo mungu umemjua kupitia dini/imani ipi..?
Kabla ya kuja waarabu i.e:uislam na wazungu i.e: ukristo mababu na mabibi au WAAFRIKA wa zamani walimjua MUNGU kupitia dini/imani ipi?

Acha ujuha unaiaibisha AFRIKA
 
Sahihi mkuu watu wanazungumzia dini za mababu ila hawajui kuwa walichokuwa wakikifanya hao mababu ni uchawi
Unamaanisha mababu na mabibi wa Kiafrika kabla ya kuja ukristo na uislam woote walikuwa ni wachawi?

Je hakuna wachungaji na masheikh wachawi waliojificha kwenye uislam na ukristo?

Kama ukristo na uislam siyo uchawi na ndizo dini za kweli kwanini viongozi wanaapa kwa vitabu vya dini hizo na kuwataja mohamed na yesu lakini wanatenda uharifu na hawadhuriki??

99% ya Waafrika ni mizigo ya ukoloni na utumwa kutoka kwa warabu na wazungu.
 
Back
Top Bottom