Waafrika tumefikia kwenye hatua mbaya sana. Baadhi ya wachungaji wa kilokole wamejipa uungu mtu, wanapenda kutukuzwa, kuabudiwa na kusujudiwa

Huu ni uzi bora kabisa kwa mwaka huu. Yatokeapo hayo yanatoa taswira kwamba watu wapo gizani kwa kiwango gani
 
mafanikio ya watu weusi kama Barack Obama,
ni mafanikio gani aliyapata huyu mtu kiasi cha sisi waafrika kujivunia?

what I know alitumika kuvunja umoja wa Africa uliokuwa katika mchakato pevu chini ya gadafi, na kuforce ushoga na mambo mengi, he is just a black weapon in white hands.

kwa hayo mengine tuko pamoja
 
Na ni tango pori haswaaa
 
Hata mimi ni mmoravian mkuu huko nako kumeharibika sana siku hizi yaani ibada nzima inatawaliwa na michango mwanzo mwisho
 
Mkuu hapo sipingani na wewe lkn tambua kuna baadhi ya makanisa hayo ya kinabii watu wanashinda makanisani tangu asubuhi mpaka jioni 24/7
 
Huyo roho wa mafanikio yukoje?
Ndugu, naona unataka kuleta msamiati mpya.
 
Huu ni uzi bora kabisa kwa mwaka huu. Yatokeapo hayo yanatoa taswira kwamba watu wapo gizani kwa kiwango gani
Ahsante Sana mkuu lkn ajabu watu hawatachangia kama walivyoshadadia uzi wa kuhusu Hamisa Mobeto akiwa ananyonyana ulimi na Rick Ross Tanzania kuna vijana wa hovyo sana[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Yaani Mwenyezi Mungu amesema sana kuwatahadharisha wanadamu , lakini hawsikii, sa si anakuona hujaokoka, kwahiyo wewe utamuambia nini : Mungu anasema ; watu wangu wanapotea kwa kukosa maarifa, tena , jamani siku za mwisho kutakuwa na manabii wa uongo - wapi hawasikii,
kuna dhehebu moja Askofu anasafiri na kiti chake, afu wakati wa Ibada inawekwa sauti kuuuuuubwaaa yaani mpaka mimi nilikuwa nawaonea sana huruma wamama walioongozana na watoto chini ya miaka 10. yaani ni kelele hata tulio mbali tunaona shida.
sasa hii yote ni kuwapumbaza waumini kwamba pale ndo kuna Mungu na huyo kiongzo ndiyo '' mwenyewe '' chochote asemacho, kasema Mungu. ( yaani kisaikolojia anakuwa kawateka hasa wa mama) ma sauti hayo makubwa, yaani shida, shiiiiidaa
 
Wachina hawaamini kwenye uikristo lakin wameendelea sana ulishajiulizaga
Ili ufanikiwe unatakiwa uwezekeze kwenye kazi na sio kusubiria miujiza
 
Ni kweli hatujaumbwa tuishi kwa miujiza lakin dini imekua biashara
 
Huyo roho wa mafanikio yukoje?
Ndugu, naona unataka kuleta msamiati mpya.
Usichokijua, mtu mmoja anaweza kuishi huku ndani yake kuna roho wengi kwa kazi tofauti tofauti wanaomwendesha mtu huyo! Usifunge ufahamu wako, jiachie usome vyanzo vingine vya maarifa juu ya mambo ktk ulimwengu wa roho!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…