Waafrika tumefikia kwenye hatua mbaya sana. Baadhi ya wachungaji wa kilokole wamejipa uungu mtu, wanapenda kutukuzwa, kuabudiwa na kusujudiwa

Waafrika tumefikia kwenye hatua mbaya sana. Baadhi ya wachungaji wa kilokole wamejipa uungu mtu, wanapenda kutukuzwa, kuabudiwa na kusujudiwa

Mkuu hapo sipingani na wewe lkn tambua kuna baadhi ya makanisa hayo ya kinabii watu wanashinda makanisani tangu asubuhi mpaka jioni 24/7
Katika hali ya kawaida, mtu anayeshinda kanisani kila siku basi hakuna anachochangia kwa kanisa hilo, na kama anachangia basi ana vyanzo kadhaa vingine vimuwezeshayo kupata cha kuchangia kwa kanisa!
Ninachojua, kama kuna wanufaikao ktk kanisa, wao kuhudhuria kanisani kwa huduma, na huhudumia watu tofauti tofauti wasio waumini wa kila siku kwa kanisa hilo!
Kwa wahudumu kuwa kanisani kila siku ni sawa kwa kuwa hiyo kazi kwao ndiyo chanzo chao cha mapato!
I tell you the truth, its not easy for everyone to be busy every day being in the church for nothing, never!
 
Mkuu jongea kanisan.usiache kwenda kwasababu ya hayo.Wakileta habar za michango wewe unpiga kimya.Ukiona una nafas ya kutoa unatoa vinginevyo unafanya ibada kwa Mungu wako unarud nyumban.Simple like that
Je ni lazima kufanya ibada kwa Mungu wa wazungu na waarabu? Ina maana sisi waafrika hatuna Mungu wetu?
 
Sijui lini sisi waafrika tutaamka kutoka katika hili. Maana usingizi huu ni mzito na tumefunikwa blanketi zito na nje kuna baridi kali …..hizi imani hazina hata miaka 500 Afrika….je mababu zetu ilikwaje? Waliiishije? Na Leo hata majina yetu ya asili yamepotea…..na denn waliotutesaaa, kutuuua, kutuuzaaa kama mbwa…kutufunga minyororo Leo eti tunawaabudu…..na kwenda kuhiji kwao badala ya kwa mababu zetu….
 
Sijui lini sisi waafrika tutaamka kutoka katika hili. Maana usingizi huu ni mzito na tumefunikwa blanketi zito na nje kuna baridi kali …..hizi imani hazina hata miaka 500 Afrika….je mababu zetu ilikwaje? Waliiishije? Na Leo hata majina yetu ya asili yamepotea…..na denn waliotutesaaa, kutuuua, kutuuzaaa kama mbwa…kutufunga minyororo Leo eti tunawaabudu…..na kwenda kuhiji kwao badala ya kwa mababu zetu….
Kumbuka, kila jambo lina wakati wake, kupingana na jambo ktk wakati wake hutofanikiwa, wakati wake ukipita mambo yanabadilika!
 
Aliyesema dini ni kasumba sawa na bangi hakukosea. Si Ukristo, Ubudha wala Uislam, wote ni utumwa wa kujitakia ambapo mabwana wanaofuga watumwa hutokea kuwa matajiri wakati watumwa wakiendelea kuwaramba matako.
Upuuzi huo sisi Waislam hatunaga.
Kwanza kwenye Uislam ukiongeza kitu ambacho hakipo kwenye Quraan ama Hadithi ya mtume ujue kichapo kinakuhusu.

Tatizo wakristo wengi hamuijui Bible kwa kuisoma, bali munaishia kuzibeba tu mikononi.

Tofauti na sisi Waislam, wengi tunakijua kitabu chetu kwa kukisoma.

Yani ukiingia msikitini ni wachache wasie ijua kilicho andikwa kwenye Quraan, yani mpaka mtoto wa miaka kumi na mbili anajua kuisoma na kuielewa Quraan.

Nyinyi kanisani anae ijua Bíblia ni mchungaji tu, wafuasi kalibu wote hawaji.

Kiufupi kanisani asipokua mchungaji basi ibada hakuna siku hiyo, wakati msikitini hata sheykh asipokuepo hata mimi naswalisha.
 
Katika hali ya kawaida, mtu anayeshinda kanisani kila siku basi hakuna anachochangia kwa kanisa hilo, na kama anachangia basi ana vyanzo kadhaa vingine vimuwezeshayo kupata cha kuchangia kwa kanisa!
Ninachojua, kama kuna wanufaikao ktk kanisa, wao kuhudhuria kanisani kwa huduma, na huhudumia watu tofauti tofauti wasio waumini wa kila siku kwa kanisa hilo!
Kwa wahudumu kuwa kanisani kila siku ni sawa kwa kuwa hiyo kazi kwao ndiyo chanzo chao cha mapato!
I tell you the truth, its not easy for everyone to be busy every day being in the church for nothing, never!
Kiongozi nakupa taarifa sahihi ninyi mnaojiita manabii,mitume sijui makuhani wa zama hizi sehemu yenu ni bottom less pit or hell you always deceive worshipers kupitia miujiza ya kipepo huwezi kuthibitisha humu kuwa attending to church without struggling to find your own bread utapata chochote kutoka kanjsani you are a living lier
 
Mimi ni mlokole mzuri tu na ni mzee wa kanisa TAG ila huwa napingana sana na baadhi ya mafundisho na mifumo ya vyuo vya biblia jinsi vinavyo wa shape watu wao. Huwa nawaukiza watu ni kwanini walokole wengi ni masikini? Wale walokole wafukutwa tofaut sana na wakristo huko KKKT au RC MAFUNDISHO ni tatizo sana.

Yan huwa time nyingine unamwangalia mchungaji af unamoima unaona kabisa hapa hamna usalama huko tunapopelekana.
NB

Nimezaliwa Moravian nimekulia UKWATA.
Wengi ya walokole sisi..tumeweka kila kitu ktk imani..akili tumemwachia shetani..mtu hasomi anategemea kufaulu kwa maombi au mafuta ya upako...naona kabisa kana mwokozi hatotokea huku kwa walokole..basi siku zijazo watoto wetu watasusia imani kabisaaa...maana wanavyoona wazazi wanafanya ujinga kwa kigezo cha imani..wataaachaaa....
 
Dini zote na madhehebu yote yanapumbaza waumini.

Uzuri wa dini inawapumnaza waumini wake wote halafu mnabaki kuchekana, mlokole anaona mkatoliki anaibiwa, mkatoliki anaona mlokole anatapeliwa, wote mnakua kazi yenu ni kuchekana.

Vile vile msabato atamcheka na kumshangaa mlutheri ama mtu anaedali jumapili na mtu wa jumapili ataona mtu anaesali jumamosi kama amechanganyikiwa, yote hii inatokana na dini kuwapumbaza wote kwa kiwango kile kile.

Haya mambo ya dini ni utapeli kama utapeli mwingine, mungu wala shetani hawapo.
Ukweli ni kwamba hakuna dhehebu sahihi hapa duniani..na tukumbuke kuwa ktk biblia hakuna eneo Yesu alisema hawa wako sahihi..wale sio sahihi...alisema atakae mwamini hatohukumiwa..na asiyemwamini atahukumiwa. Binafsi baada ya kutambua hili..limenisaidia kuheshimu na kupenda kila mtu anajiita mkristo..kamwe sijioni wa thamani zaidi ya mwingine..na kwangu kanisa bora..ni lile litakaloniwezesha kumjua na kumtii Yesu ktk roho na kweli period...nikikuta mlutheli anafundisha vema au sawa na biblia..nasali..mkatoliki..twende kazi.
 
Ukweli ni kwamba hakuna dhehebu sahihi hapa duniani..na tukumbuke kuwa ktk biblia hakuna eneo Yesu alisema hawa wako sahihi..wale sio sahihi...alisema atakae mwamini hatohukumiwa..na asiyemwamini atahukumiwa. Binafsi baada ya kutambua hili..limenisaidia kuheshimu na kupenda kila mtu anajiita mkristo..kamwe sijioni wa thamani zaidi ya mwingine..na kwangu kanisa bora..ni lile litakaloniwezesha kumjua na kumtii Yesu ktk roho na kweli period...nikikuta mlutheli anafundisha vema au sawa na biblia..nasali..mkatoliki..twende kazi.
Hakika wewe ni mcha Mungu wakweli ubarikiwe mnoo kiongozi wangu hii post yako imenibariki sana sana
 
Yaani tumetekwa na dini mpaka misionaries waliotuletea ili watutawale wanatushangaa [emoji849][emoji849][emoji849] yaani mtu haambiliki chochote kuhusu anachosema mchungaji huku akimwambia mavuno yake yote amtolee bwana(pastor) huku akioteshwa ndoto za watu wanaofanya kazi kwa bidii sana mchungaji anajisifia alikuwa analala njaa na mkewe lakini sasa anamiliki V8 na nyumba ya ghorofa na muumini anashangilia huku anaenda kula kiporo kilichobaki jana.
 
Mm najiuliza tu.wale babu zetu ambao waliishi kabla ya kuja hiz dini nao hukumu yao siku ya ufufuo itakuwaje

Maana waliamin miungu yao na walifanikiwa vizuri tu

Walioleta din huko kwao mauaji ushoga na wengne hawaend kanisani kabisa nao tunawaweka kundi gani?

Wachina hawaamin katika dini na ndio taifa linalokuja kasi Sana kwa maendeleo

Mm binafsi namashaka Sana na hizi dini za kuletewa na waarabu na wazungu

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Hi
 
Dini zote na madhehebu yote yanapumbaza waumini.

Uzuri wa dini inawapumnaza waumini wake wote halafu mnabaki kuchekana, mlokole anaona mkatoliki anaibiwa, mkatoliki anaona mlokole anatapeliwa, wote mnakua kazi yenu ni kuchekana.

Vile vile msabato atamcheka na kumshangaa mlutheri ama mtu anaedali jumapili na mtu wa jumapili ataona mtu anaesali jumamosi kama amechanganyikiwa, yote hii inatokana na dini kuwapumbaza wote kwa kiwango kile kile.

Haya mambo ya dini ni utapeli kama utapeli mwingine, mungu wala shetani hawapo.
Ebwana wiki kama moja iliyopita nilikaa tu kitaa, mara nikaona vitu vya ajabu, waya aina za kopa zikawa zinajikusanya zikajifinyanga finyanga, ikatengenezeka coil, mara madini ya chuma yakajitengeza mapangaboi, ikatengezeka stendi na vitu vingine pia. Nikwambiavyo sahivi nina feni nzuri imo ndani iliyojitengeneza wenyewe.
Unaaamini?

Note: Mleta mada yupo sahihi sana sana sana, ila haiusiani na kukanusha uwepo wa Mungu
 
Dini zote na madhehebu yote yanapumbaza waumini.

Uzuri wa dini inawapumnaza waumini wake wote halafu mnabaki kuchekana, mlokole anaona mkatoliki anaibiwa, mkatoliki anaona mlokole anatapeliwa, wote mnakua kazi yenu ni kuchekana.

Vile vile msabato atamcheka na kumshangaa mlutheri ama mtu anaedali jumapili na mtu wa jumapili ataona mtu anaesali jumamosi kama amechanganyikiwa, yote hii inatokana na dini kuwapumbaza wote kwa kiwango kile kile.

Haya mambo ya dini ni utapeli kama utapeli mwingine, mungu wala shetani hawapo.
Ebwana wiki kama moja iliyopita nilikaa tu kitaa, mara nikaona vitu vya ajabu, waya aina za kopa zikawa zinajikusanya zikajifinyanga finyanga, ikatengenezeka coil, mara madini ya chuma yakajitengeza mapangaboi, ikatengezeka stendi na vitu vingine pia. Nikwambiavyo sahivi nina feni nzuri imo ndani iliyojitengeneza wenyewe.
Unaaamini?

Note: Mleta mada yupo sahihi sana sana sana, ila haiusiani na kukanusha uwepo wa Mungu
 
Upuuzi huo sisi Waislam hatunaga.
Kwanza kwenye Uislam ukiongeza kitu ambacho hakipo kwenye Quraan ama Hadithi ya mtume ujue kichapo kinakuhusu.

Tatizo wakristo wengi hamuijui Bible kwa kuisoma, bali munaishia kuzibeba tu mikononi.

Tofauti na sisi Waislam, wengi tunakijua kitabu chetu kwa kukisoma.

Yani ukiingia msikitini ni wachache wasie ijua kilicho andikwa kwenye Quraan, yani mpaka mtoto wa miaka kumi na mbili anajua kuisoma na kuielewa Quraan.

Nyinyi kanisani anae ijua Bíblia ni mchungaji tu, wafuasi kalibu wote hawaji.

Kiufupi kanisani asipokua mchungaji basi ibada hakuna siku hiyo, wakati msikitini hata sheykh asipokuepo hata mimi naswalisha.
Nyani haoni kundule. Nyie tena ndo msiseme. Wakati wakristo wamegeuka watumwa wa kutegemea miujiza na wokovu, waislam mnategemea ugaidi. Mko tayari kuua kwa ajili ya Allah na Mtume lakini si kwa ajili ya wazazi wenu. Utasikia mtu mzima akisema "ukimtukana Mtume kichwa chako halali yangu." Ukitaka kujua ni mtumwa mtukane baba au mama yake, anakwenda polisi. Waafrika wote ni watumwa ukiondoa wale ambao hawaamini kwenye utumwa huu ambao nyinyi huwaita makafiri na wakristo huwaita wapagani. Angalia majina yenu na mafungamano yenu. Mnabaguliwa na wazungu na waarabu lakini hamjitambui. Miungu yenu ni ima ya kiarabu au kizungu. Manasujudu kila siku kuelekea kwa mabwana zenu. Mnajiita waislam au wakristo kwanza lakini si waswahili. Mnatuchelewesha kweli kweli. Hata kushiriki mabishano haya ni kwa vile sina jinsi. mnaboa kweli kweli wanangu. Mnafundishwa hata kutawaza na namna ya kuanza kula utadhani hamkuwa mkiyafanya haya kabla ya kuingizwa utumwani. Kila kitu chenu ni kitamu na halali isipokuwa kujitambua ndo haramu.
 
Makala hii iliandikwa kwa kiingereza na Mwandishi Kay Musonda na kuchapishwa na jarida la Modern Ghana, toleo no.215 la April 1 mwaka huu. Nimefanya tafsiri isiyo rasmi ya Kiswahili pengine tutapata la kujifunza.

____________

Afrika kwa sasa inashuhudia aina mpya ya utumwa kupitia Ukristo (ulokole). Aina hii ya utumwa wa imani imewafanya watu wengi kuwa wavivu wa kufikiri na uwezo wa kutafakari mambo umedumazwa.

Baadhi ya wachungaji wa kilokole wamejipa uungu mtu. Wanapenda kutukuzwa, kuabudiwa na kusujudiwa. Wanajituza wao zaidi kuliko kumtukuza yule wanayemhubiri.

Wachungaji wa aina hii hawawezi kuongelea mafanikio ya watu weusi kama Barack Obama, Serena Williums, na Usain Bolt. Hawawezi kuongelea wagunduzi waliosaidia kutransform dunia kama kina Albert Einstein, Steve Jobs na wengine. Hawawezi kuongelea Wanasayansi waliodedicate maisha yao na wengine kufia maabara wakitafuta dawa za kutibu magonjwa mbalimbali yanayoisumbua Afrika.

Hawawezi kuongea kuhusu wanafasihi vijana kama Chimamanda Ngozi na Ben Okri, au wakongwe kama Chinua Achebe na Ngugi wa Thiong'o.

Kila pembe ya dunia kuna watu waliofanikiwa kutokana na maarifa, bidii, ubunifu, na weledi. Wapo wafanyabiashara, wanasiasa, wanafasihi na hata wanasayansi wanaofanya mambo makubwa ya kuisaidia dunia yetu. Lakini wachungaji wa Afrika hawatawaongelea watu wa aina hii.

Wao wataongelea mtu aliyepata kazi kimiujiza licha ya kukosa sifa za kupata kazi hiyo, kwa sababu tu aliombewa na kupewa mafuta ya upako siku ya interview ya kazi.

Wataongelea kuhusu kijana aliyetoa mshahara wake wote kwa miezi mitatu mfululizo kwa Mchungaji wake kama mbegu ya mafanikio, baadae akawa 'Boss' kazini.

Au wataongelea kuhusu kijana aliyefeli sekondari lakini baada ya baba yake kumalizia ukarabati wa nyumba ya Mchungaji, alipokea barua ya kupata 'admision' chuo kikuu bila hata kurudia mitihani.

Wachungaji hawa hutumia 'miujiza na shuhuda feki' kama njia ya kuwafumba akili wafuasi wao. Kule Afrika kusini kuna Mchungaji alidanganya kufufua mtu. Hata alipoomba msamaha bado kuna waumini wanaendelea kumuamini na kumsujudu.

Wachungaji hawa wamegundua haya ndio mahubiri yanayopendwa sana huku Afrika. Hawataki kuhubiri kuhusu Aliko Dangote alivyoanza biashara na magumu aliyopitia.

Wanahubiri kuhusu mama Janeth aliyekua mama Ntilie huko Enugu, lakini alipotumia mtaji wake wote wa shilingi laki 5 kununua mafuta ya upako kwa Nabii fulani, ghafla biashara yake ikakua na sasa anamiliki mahoteli makubwa pande zote za nchi. Yani bila mtaji, bila business plan, bila timeline ghafla tu akamiliki mahoteli. Na waumini watashangia kwa kusema Ameen.

Aina hii ya ukristo imepanda mbegu ya uvivu wa kufikiri kwa vijana wengi wa Afrika ambao wanalazimishwa kumuona Mungu kama Mfadhili wa wavivu, au wasiostahili. Kwamba mwanafunzi hata asiposoma anajua akipewa mafuta ya upako atafaulu tu siku ya mtihani. Mfanyabiashara hata asipokua mbunifu anajua akienda kwa 'baba wa miujiza' biashara yake itapanuka ghafla bin vuu. Mfanyakazi hata asipowajibika kazini anajua akitoa fungu la kumi kwa 'Dokta Upako' atapanda cheo.

Kwa baadhi ya makanisa Afrika namna pekee ya kufanikiwa ni kufanya kile wanachokiita kupanda mbegu, kupaka mafuta ya upako au kunyunyuziwa maji ya baraka. Eti wanaofanikiwa haraka ni watu 30 wa mwazo wanaokimbilia mbele ya kanisa kila mmoja akiwa ameshika noti ya dola 100.

Aina hii ya mahubiri inawafanya watu waamini kwamba Mungu hawapendi wanaojituma na kuwa wabunifu katika kazi, badala yake anawapenda zaidi wanaotoa zaka, sadaka, malimbuko na fungu la 10 hata kama ni wavivu. Hii sio sawa hata kidogo kwa sababu Biblia inakataa uvivu kwa nguvu zote (Mithali 12:27)
_
Watu wanaaminishwa kwamba ukishatoa sadaka kanisani unaweza kuamka kila siku asubuhi ukapayuka 'Mimi ni Milionea' halafu ukavuta shuka na kuendelea kulala fofofo, ukisubiri sadaka uliyotoa ikupe muujiza wa kuokota hela, ili upate mtaji wa biashara unayoiwaza.

Mtu huna kazi, huna biashara wala wazo la biashara, huna ujuzi, huna elimu, lakini kila siku unashinda kanisani kumsikiliza Mchungaji anayesema kesho utakua milionea na wewe unasema "Baba napokea/Dady I receive". Huu ni utani.

Waambieni wanaofanya utani huu kwa kofia za Uchungaji, Uaskofu, Unabii au Utume kwamba wanamkosea Mungu. Waambieni Mungu wetu ni Mungu wa kanuni, na hana kanuni ya kuwabariki wavivu. Tuache kufundisha waumini wetu kwamba uvivu unalipa kupitia miujiza.

Mafanikio ni matokeo ya bidii, ubunifu na weledi. Biblia inazungumzia kuhusu karama. Hebu kila mtu atumie karama alizopewa kwa bidii, ubunifu na weledi aone kama hatafanikiwa. Sio sahihi kuwaambia watu wabweteke tu na kusubiria mafanikio kama kusubiria daladala kituoni kwa sababu tu wamepakwa mafuta ya upako.

Mungu alishatubariki tangu wakati wa uumbaji wetu. Ni wajibu wetu kujibidisha katika yale tufanyayo ili baraka zake ziambatane nasi (Kumb 28:6).

Wazungu na Wachina wanazidi kushindana katika kuitawala dunia kwenye mambo mbalimbali kuanzia viwanda, biashara, sayansi na teknolojia. Sisi tuko 'busy' kununua maji ya upako tukiamini yatatufanya tuwe kama Jack Ma au Bill Gates. Upuuzi.

Tumeumbwa kuitawala hii dunia (Mwanzo 1:28). Tutumie vipawa na karama tulizopewa ili kutimiza kusudi hilo la Mungu. Tusiruhusu Askofu, Mchungaji, Nabii, mtume au kiongozi mwingine yeyote wa dini atutawale akili zetu kwa kutuhubiria mafanikio ya miujiza. Wao wanaishi kifahari kwa sadaka za waumini wao, huku waumini wakiendelea kuwa mafukara wa kutupwa.

Biblia inasema kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa (Mithali 1:7). Tutafute maarifa, tufanye kazi kwa bidii, na tumuabudu Mungu katika roho na kweli. Kwa kufanya hivyo tutapata MAFANIKIO katika mambo yote tuyafanyayo.
AKILI KICHWANI, PESA MFUKONI, YESU MOYONI.
 
Wengi ya walokole sisi..tumeweka kila kitu ktk imani..akili tumemwachia shetani..mtu hasomi anategemea kufaulu kwa maombi au mafuta ya upako...naona kabisa kana mwokozi hatotokea huku kwa walokole..basi siku zijazo watoto wetu watasusia imani kabisaaa...maana wanavyoona wazazi wanafanya ujinga kwa kigezo cha imani..wataaachaaa....
Tunajificha kwenye kichaka cha maombi na maombezi dhidi ya nguvu za giza.kwamba kila tatizo linalotusibu basi shetani .ofcz shetan mtaabishaji yupo ila walokole wengi sis ni wavivu sanaaa na tunaishi kwa mazoea sana kupitiliza
 
Je ni lazima kufanya ibada kwa Mungu wa wazungu na waarabu? Ina maana sisi waafrika hatuna Mungu wetu?
Kwakua sie tumzaliwa n kukuzwa kwenye iman hii hatuna namna.Kama kuna wenye iman zingine (i hope wapo) na wanaona zinawanufaisha basi nao ruksa kuendelea na ibada zao as long as hazi wa cost.maana hata kama ukristo au uislam unakuongezea gharama badala ya kukupa manufaa (sio ya kifedha tuu) nasi hazina maana.
Maana kama mwanadamu/mshkaji wako wa karibu anaweza akakusaidia au akaguswa na kuumia kwa matatizo ulio nayo basi Mungu anapaswa kufanya zaid ya hapo..Kama huoni hilo bas imani haina faida.imani hiz za kukamuana pesaaa mwanzo mwisho za kazi gani sasa.
 
Back
Top Bottom