Waafrika wanaoshangilia ushindi wa Trump kwa sababu ya misaada kupunguzwa ni wavivu wa kufikiri.

Waafrika wanaoshangilia ushindi wa Trump kwa sababu ya misaada kupunguzwa ni wavivu wa kufikiri.

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kuna kundi kubwa la Waafrika waliofurahia na kushangilia sana ushindi wa Trump, kila nikisikia au nikisoma sababu wanazozitoa kumuhusudu Trump naona kama mfumo wao wa umeme kichwani una hitilafu, Tuangalie hoja moja ya kupunguzwa msaada na utegemezi wetu kwa mfano

Wale wanaosema misaada ya US itapungua kwa nchi za Africa na mashirika ya UN kama WHO hivyo tutajitegemea wanafikiria kivivu kwa kushindwa kuunganisha mambo. Chukulia mfano Tanzania ambayo inapokea msaada wa karibia $Million 500 kwa mwaka kutoka US, hivi kupungwa kwa hizi fedha kweli ndio kutaifanya serikali ya CCM kubadili sera zake za matumizi kwa viongozi na vitu visivyo vya kipaumbele??

Kupunguzwa kwa misaada ni hasara kwa watu masikini wa vijijini kwa sababu viongozi hawawezi kubadili mtindo wao wa maisha kwa kupunguzwa au kuondolewa msaada, mfano mzuri ni Zimbabwe.
Watakaoumia ni raia wanyonge wanaotegema Zahanati, ARVs, chanjo na condoms za ruzuku kutoka US.

Misaada ikipunguzwa au ikikatwa China ipo na fedha nyingi tu ila ni mkopo , viongozi watabadilisha mitaa kutoka Washington kuelekea Beijing huku raia wategemea misaada wakiumia zaidi kulipia mikopo ya Kichina kugharamia Afya kwa mfano, Sahauni hilo suala kwamba eti matumizi mabovu yatapunguzwa.
Screenshot_20241107-111906_X.jpg
 
Trump hatakiwi kupunguza misaada, anatakiwa kuikata kabisa asitoe hata shilingi kumi. Haiwezekani watu wanasafiri kwa gharama za umma kwenda kufanya cocktail parties nje, pesa zinazotumika ku recruit machawa na kununua ma LC 300. Nasemaje Trump kata kabisa misaada akili itukae sawa.
 
hivyo unataka tulie..?
huyu ndo atatufanya tuinuke maana mtu akipitia shida ndo atajua afanye nini hao viongozi tutaumana nao mpk kieleweke!
 
Miafrika akili hamna hela za misaada wanaenda Kukaa kikao Marekani hawa watu nyie hamuwajui..
 
nyie wahamiaji haramu jiandaeni kurudi africa acheni mmeharibu sn nchi ya watu

jiandaeni milioni 11 tunawafukuza
 
Misaada inalemaza sana. Hasa hii ya masharti ya kukubali abortions na ushoga haifai
 
Kuna kundi kubwa la Waafrika waliofurahia na kushangilia sana ushindi wa Trump, kila nikisikia au nikisoma sababu wanazozitoa kumuhusudu Trump naona kama mfumo wao wa umeme kichwani una hitilafu, Tuangalie hoja moja ya kupunguzwa msaada na utegemezi wetu kwa mfano

Wale wanaosema misaada ya US itapungua kwa nchi za Africa na mashirika ya UN kama WHO hivyo tutajitegemea wanafikiria kivivu kwa kushindwa kuunganisha mambo. Chukulia mfano Tanzania ambayo inapokea msaada wa karibia $Million 500 kwa mwaka kutoka US, hivi kupungwa kwa hizi fedha kweli ndio kutaifanya serikali ya CCM kubadili sera zake za matumizi kwa viongozi na vitu visivyo vya kipaumbele??

Kupunguzwa kwa misaada ni hasara kwa watu masikini wa vijijini kwa sababu viongozi hawawezi kubadili mtindo wao wa maisha kwa kupunguzwa au kuondolewa msaada, mfano mzuri ni Zimbabwe.
Watakaoumia ni raia wanyonge wanaotegema Zahanati, ARVs, chanjo na condoms za ruzuku kutoka US.

Misaada ikipunguzwa au ikikatwa China ipo na fedha nyingi tu ila ni mkopo , viongozi watabadilisha mitaa kutoka Washington kuelekea Beijing huku raia wategemea misaada wakiumia zaidi kulipia mikopo ya Kichina kugharamia Afya kwa mfano, Sahauni hilo suala kwamba eti matumizi mabovu yatapunguzwa.
View attachment 3146022
Watu hao wakionja joto ya jiwe akili zitafunguka na kukataa kugeuzwa chawa kwamanufaa ya watafuna kodi na misaada ya maendeleo na mengineyo.
 
wewe ndo umeme mdogo kichwani.wewe unaona nisawa kua Taifa lakusaidiwa saidiwa ata mambo ambayo yako ndani ya uwezo wetu.Wacha hiyo misaada ikate mengine yatajulikana uko mbele.Tatizo la afrika ni viongozi,tukiteseka tutajua namna yakudili nao hadi nchi itakapopata viongozi wanaojitambua.
 
Back
Top Bottom