Waambieni mapema wanaowaza kujiua: “wataruka majivu na kukanyaga moto.”

Waambieni mapema wanaowaza kujiua: “wataruka majivu na kukanyaga moto.”

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
1,679
Reaction score
2,123
Inasikitisha sana kusikia kesi za watu wanaojiua, ama kwa kunywa sumu, kwa kujinyonga, kwa kujipiga risasi au kwa kujitupa chini kutoka ghorofani. Wanaofanya hivyo huwa wanafikiri kwamba wakijiua ndio watapumzika tabu zao. Wanafikiri kujiua ndio mwisho wa kero walizo nazo. Wanadhani wakijiua wata-rest in peace. Mawazo hayo ni potofu; tuyapinge kwa njia zote. Yanatoka kwa yule mwovu shetani na mapepo yake.

Ukweli ni kwamba kujiua ni hasara. Anayejiua kwa kufikiri anaepuka matatizo, ni sawa na mtu anayeruka majivu na kukanyaga moto. Kujiua ni dhambi(Kutoka 20:13). “Usiue” ni moja kati ya amri kumi za Mungu. Katika 1 Wakorintho 3:16-17 tunasoma pia kuwa miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu. Mtu akiliharibu hekalu hilo, Maandiko yamenena wazi Mungu atamharibu mtu huyo.

Watendao dhambi za aina zote, wakifa, wanaenda kuteseka motoni. Kitabu cha Luka 16:22-24(SRUV) kinatupa picha ya hali ilivyo baada ya mtu mwenye dhambi kufa:
"Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Abrahamu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Abrahamu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. Akalia, akasema, Ee baba Abrahamu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, aupoze ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu."

Hivyo tuwashauri mapema, tuwaonye, tuwaambie ukweli huo wanaotaka kujiua.

Duniani kuna dhiki nyingi lakini hilo lisiwe sababu ya kumfanya mtu ajiue. Maana akijiua sekunde ile ile anaingia katika mateso mazito kuliko yale aliyokuwa anayapata duniani. Wenye mawazo ya kujiua tuwape pia Maandiko haya yenye faraja na matumaini:
Yohana 16:33
“...Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo, mimi nimeushinda ulimwengu.”
Yohana 14:1-3
“Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Katika nyumba ya Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi muwepo.”

Yesu atakaporudi, wote tunaomwamini na kuishi maisha matakatifu, atatunyakua na kutupeleka mbinguni kwenye raha isiyo na mwisho. Hatutakumbuka tena tabu na dhiki za dunia hii.
 
Mawazo ya kujiua yakikuijia:

Kwanza yakemee, kwakuwa yanatoka kwa Ibilisi. Ibilisi hakupendi anataka uangamie. Hiyo ndiyo furaha yake.

Pili, usiishi kama vile uko kisiwani – Tafuta Msaada.
Unapohisi huzuni au mzigo mzito, usiubebe peke yako. Tafuta mtu unayemwamini – rafiki, Mchungaji, au mshauri wa kiroho, mweleze shida uliyo nayo, utapata msaada. Katika Kitabu cha Mhubiri 4:9-10 imeandikwa hivi:
“Afadhali wawili kuliko mmoja... Kwa maana waweza kusaidiana; lakini mtu aliye peke yake akianguka hana wa kumwinua.”

Kumbuka katika dunia hii wapo watu ukiwaeleza shida ulizo nazo watakujali na kukusaidia
 
Inasikitisha sana kusikia kesi za watu wanaojiua, ama kwa kunywa sumu, kwa kujinyonga, kwa kujipiga risasi au kwa kujitupa chini kutoka ghorofani. Wanaofanya hivyo huwa wanafikiri kwamba wakijiua ndio watapumzika tabu zao. Wanafikiri kujiua ndio mwisho wa kero walizo nazo. Wanadhani wakijiua wata-rest in peace. Mawazo hayo ni potofu; tuyapinge kwa njia zote. Yanatoka kwa yule mwovu shetani na mapepo yake.

Ukweli ni kwamba kujiua ni hasara. Anayejiua kwa kufikiri anaepuka matatizo, ni sawa na mtu anayeruka majivu na kukanyaga moto. Kujiua ni dhambi(Kutoka 20:13). “Usiue” ni moja kati ya amri kumi za Mungu. Katika 1 Wakorintho 3:16-17 tunasoma pia kuwa miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu. Mtu akiliharibu hekalu hilo, Maandiko yamenena wazi Mungu atamharibu mtu huyo.

Watendao dhambi za aina zote, wakifa, wanaenda kuteseka motoni. Kitabu cha Luka 16:22-24(SRUV) kinatupa picha ya hali ilivyo baada ya mtu mwenye dhambi kufa:
"Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Abrahamu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Abrahamu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. Akalia, akasema, Ee baba Abrahamu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, aupoze ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu."

Hivyo tuwashauri mapema, tuwaonye, tuwaambie ukweli huo wanaotaka kujiua.

Duniani kuna dhiki nyingi lakini hilo lisiwe sababu ya kumfanya mtu ajiue. Maana akijiua sekunde ile ile anaingia katika mateso mazito kuliko yale aliyokuwa anayapata duniani. Wenye mawazo ya kujiua tuwape pia Maandiko haya yenye faraja na matumaini:
Yohana 16:33
“...Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo, mimi nimeushinda ulimwengu.”
Yohana 14:1-3
“Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Katika nyumba ya Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi muwepo.”

Yesu atakaporudi, wote tunaomwamini na kuishi maisha matakatifu, atatunyakua na kutupeleka mbinguni kwenye raha isiyo na mwisho. Hatutakumbuka tena tabu na dhiki za dunia hii.
Ukisikia mtu anataka kujiua unaweza kumwambia maneno haya:

"Ndugu, Mungu anakupenda. Alikuumba kwa kusudi maalum, na maisha yako yana thamani kubwa machoni pake. Katika Yeremia 29:11 BWANA anasema:
“Maana nayajua mawazo ninayowawazia, asema Bwana, mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.

Hata kama sasa hivi huoni tumaini, Mungu ana mpango mzuri na maisha yako, endelea kusubiri, usikate tamaa.
 
Kuna vipindi kwenye maisha hataa kuelewa wanachosema watu haulewi,
Wazo pekee linakuaga kupumzika.
 
Kuna vipindi kwenye maisha hataa kuelewa wanachosema watu haulewi,
Wazo pekee linakuaga kupumzika.
Hayo mawazo ya kwamba mtu atapumzika akijiua ndo sasa tunatakiwa tuyapigie kelele kwamba ni mawazo potofu. Kama tulivyoona kwa Maandiko, ni wazi kabisa mtu akijiua haendi kupumzika. Anaenda kwenye mateso makali zaidi. Ila shetani na mapepo yake wanaeneza uongo kuwa ukijiua utapumzika. Shetani ni mwongo(Yohana 8:44). Yeye ameishahukumiwa kwenda motoni, hivyo akiona watu wana matatizo anawashawishi watende dhambi ya kujiua ili waangamie pamoja naye.
 
Inasikitisha sana kusikia kesi za watu wanaojiua, ama kwa kunywa sumu, kwa kujinyonga, kwa kujipiga risasi au kwa kujitupa chini kutoka ghorofani. Wanaofanya hivyo huwa wanafikiri kwamba wakijiua ndio watapumzika tabu zao. Wanafikiri kujiua ndio mwisho wa kero walizo nazo. Wanadhani wakijiua wata-rest in peace. Mawazo hayo ni potofu; tuyapinge kwa njia zote. Yanatoka kwa yule mwovu shetani na mapepo yake.

Ukweli ni kwamba kujiua ni hasara. Anayejiua kwa kufikiri anaepuka matatizo, ni sawa na mtu anayeruka majivu na kukanyaga moto. Kujiua ni dhambi(Kutoka 20:13). “Usiue” ni moja kati ya amri kumi za Mungu. Katika 1 Wakorintho 3:16-17 tunasoma pia kuwa miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu. Mtu akiliharibu hekalu hilo, Maandiko yamenena wazi Mungu atamharibu mtu huyo.

Watendao dhambi za aina zote, wakifa, wanaenda kuteseka motoni. Kitabu cha Luka 16:22-24(SRUV) kinatupa picha ya hali ilivyo baada ya mtu mwenye dhambi kufa:
"Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Abrahamu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Abrahamu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. Akalia, akasema, Ee baba Abrahamu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, aupoze ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu."

Hivyo tuwashauri mapema, tuwaonye, tuwaambie ukweli huo wanaotaka kujiua.

Duniani kuna dhiki nyingi lakini hilo lisiwe sababu ya kumfanya mtu ajiue. Maana akijiua sekunde ile ile anaingia katika mateso mazito kuliko yale aliyokuwa anayapata duniani. Wenye mawazo ya kujiua tuwape pia Maandiko haya yenye faraja na matumaini:
Yohana 16:33
“...Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo, mimi nimeushinda ulimwengu.”
Yohana 14:1-3
“Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Katika nyumba ya Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi muwepo.”

Yesu atakaporudi, wote tunaomwamini na kuishi maisha matakatifu, atatunyakua na kutupeleka mbinguni kwenye raha isiyo na mwisho. Hatutakumbuka tena tabu na dhiki za dunia hii.
Watu wanapuuza kusoma Biblia, lakini Biblia ina maneno mengi ya faraja hata kwa wanaokabiliwa na hali za kutaka kujiua. Ukiona mtu anawaza kujiua, msomee Zaburi 34:17-18. Maandiko hayo yanatushauri kumlilia Mungu kwa maombi. Mungu yu karibu na wenye shida na yuko tayari kuwasaidia wanaomlilia.
 
duniani sio nyumbani kwetu.bali tupo kwenye mchakato wakukuza ufahamu wetu wajuu zaidi.
na hupaswi kuutoa uhai wako kufanya hivo ni kwenda kinyuma na asili.
 
Duuuh mungu tuepushe na matatizo ya dunia
Amen.

Ila ukiandika Jina la Mungu anza na herufi kubwa(M). Shetani ndiye anayeitwa mungu wa dunia hii. "... mungu wa dunia hii amepofusha fikra za wasioamini, ili wasione nuru ya Injili ya utukufu wa Kristo, aliye sura ya Mungu." (2 Wakorintho 4:4)
 
Amen.

Ila ukiandika Jina la Mungu anza na herufi kubwa(M). Shetani ndiye anayeitwa mungu wa dunia hii. "... mungu wa dunia hii amepofusha fikra za wasioamini, ili wasione nuru ya Injili ya utukufu wa Kristo, aliye sura ya Mungu." (2 Wakorintho 4:
Asante
 
Inasikitisha sana kusikia kesi za watu wanaojiua, ama kwa kunywa sumu, kwa kujinyonga, kwa kujipiga risasi au kwa kujitupa chini kutoka ghorofani. Wanaofanya hivyo huwa wanafikiri kwamba wakijiua ndio watapumzika tabu zao. Wanafikiri kujiua ndio mwisho wa kero walizo nazo. Wanadhani wakijiua wata-rest in peace. Mawazo hayo ni potofu; tuyapinge kwa njia zote. Yanatoka kwa yule mwovu shetani na mapepo yake.

Ukweli ni kwamba kujiua ni hasara. Anayejiua kwa kufikiri anaepuka matatizo, ni sawa na mtu anayeruka majivu na kukanyaga moto. Kujiua ni dhambi(Kutoka 20:13). “Usiue” ni moja kati ya amri kumi za Mungu. Katika 1 Wakorintho 3:16-17 tunasoma pia kuwa miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu. Mtu akiliharibu hekalu hilo, Maandiko yamenena wazi Mungu atamharibu mtu huyo.

Watendao dhambi za aina zote, wakifa, wanaenda kuteseka motoni. Kitabu cha Luka 16:22-24(SRUV) kinatupa picha ya hali ilivyo baada ya mtu mwenye dhambi kufa:
"Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Abrahamu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Abrahamu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. Akalia, akasema, Ee baba Abrahamu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, aupoze ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu."

Hivyo tuwashauri mapema, tuwaonye, tuwaambie ukweli huo wanaotaka kujiua.

Duniani kuna dhiki nyingi lakini hilo lisiwe sababu ya kumfanya mtu ajiue. Maana akijiua sekunde ile ile anaingia katika mateso mazito kuliko yale aliyokuwa anayapata duniani. Wenye mawazo ya kujiua tuwape pia Maandiko haya yenye faraja na matumaini:
Yohana 16:33
“...Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo, mimi nimeushinda ulimwengu.”
Yohana 14:1-3
“Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Katika nyumba ya Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi muwepo.”

Yesu atakaporudi, wote tunaomwamini na kuishi maisha matakatifu, atatunyakua na kutupeleka mbinguni kwenye raha isiyo na mwisho. Hatutakumbuka tena tabu na dhiki za dunia hii.
Watu wanaendelea kujiua. Inaonekana ujumbe huo haujawafikia wanaowaza kujiua. Please share.
 
Mawazo ya kujiua ni pepo.
Uko sahihi.
Shetani na mapepo yanapomshawishi mtu ajiue yanamwambia maneno yanayoonekana kama vile yako sawa, kumbe ni udanganyifu. Tazama hapa jinsi shetani alivyomshawishi Yesu ajiue kwa kujitupa chini kutoka juu ya mnara eti Mungu atamletea malaika wamuokoe.
Mathayo 4:1-17 SRUV
"...Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako."
 
Back
Top Bottom