Waandamanaji Nairobi wavamia jengo la Bunge baada ya kuwashinda nguvu polisi, yasemwa waandamanaji 10 wameuawa kwa kupigwa risasi halisi

Waandamanaji Nairobi wavamia jengo la Bunge baada ya kuwashinda nguvu polisi, yasemwa waandamanaji 10 wameuawa kwa kupigwa risasi halisi

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
1719324594957.png

Picha na AP.

Waandamanaji 10 wanaripotiwa kuuawa na polisi baada ya kuvamia jengo la Bunge la nchi hiyo na kuwashinda nguvu polisi.

Hali kwa sasa ni shwari kidogo baada ya polisi kuongeza nguvu ya idadi katika eneo hilo. Idadi ya watu wapatao 5o wamejeruhiwa na huenda idadi hiyo ikaongezeka.

Sehemu moja ya jengo hilo la Bunge imeshika moto na moto huo bado waendelea.

Tukio hilo limetokea mara tu baada ya Bunge hilo kupitisha mswada wa sheria ya kodi inoongeza kodi katika bidhaa mbalimbali nchini huo.

Raisi Ruto amesema kuongeza kodi huko kutathibiti kukopa mikopo ambayo itaiathiri nchi hiyo kiuchumi.

Yadaiwa kuwa wabunge wengi walopitisha mswada huo wamepokea mlungula ili kurahisisha kupitishwa kwa muswaada huo ambao utaathiri wakenya wengi walo na kipato cha chini, wafanyabiashara na wachuuzi.

1719325960371.png

Picha na AP.

Kuna majeruhi wengi ambao wamejeruhiwa kwa risasi ambapo polisi waliamua kutumia nguvu na risasi halisi badala ya risasi za bandia au "rubber bullets".

Muswada huo uitwao Finance Bill 2024 umepitishwa leo asubuhi na wabunge kwa kura zipatazo 295 dhidi ya kura 106 huku kura tatu zikiharibika.

Chama cha Kwanza Alliance cha raisi Ruto kina wabunge wengi Bungeni na uwingi wao umerahisisha kupitishwa kwa mswada huo.

Mswada uo hivi sasa upo mezani kwa raisi Ruto ukingojea atie saini kuwa sheria rasmi.
 
Hila viongozi wa nchi za africa huwa solution ya matatizo ya kifedha huwa wanaona kupandisha gharama kwa wananchi badala ya kupunguza matumizi ya serikali ya sio ya lazima unakuta nchi ina hali ngumu kifedha lakini hyo hyo nchi imetoa order gari za dhamani kubwa kwa ajili ya viongozi wakati wangeweza kununua gari nzuri kwa bei ya chini
 
Back
Top Bottom