Wababa wanalalamika sana kutengwa na watoto wao kimawasliano hata kiuchumi. Je, shida ni nini? Wamama mnaliongeleaje hili? Watoto mnafanya haya kweli?

Hahaaa wamama wenyewe ndo hawa dada zangu kina cariha , Demi etc. utaanza vip kuwasimamia sijui

Si unaona mwenyewe misimamo yao, hadi kidume mwenyewe inasalimu amri, chezeyaaa
Mimi nimemuheshimu baba yangu hadi siku anafariki nimeshakuwa mtu mzima, sijawahi kumtenga au kumuona hana thamani. Baba na mama yangu wote wana thamani sawa.

Ukiona baba hathaminiwi basi tambua kuwa hakusimama vzr kwenye nafasi yake kimajukumu au ni mnyanyasaji kwa mke wake na watoto wameshuhudia.
 
Nazungumzia ujumla bwana, siku hizi hata wamama wakitoka kazini wanakaa kwenye sofa, kazi yao kutuma tu, hayo malezi walishawaachia wasaídizi wa nyumbani kwa asilimia kubwa tu. 50-50 inaapply sana tu kwa kizazi hiki.
 
Si nyie ndo mnawalisha sumu! Yani wanawake hamjuagi mnachotaka adamu alikuwa anaishi vizuri tu mpaka akina mende Simba na wanyama wote!.. alipokuja sasa mwanamke akafanya yake simba akaanza kumuona adamu Kama ugali tu..🤣
Duh!
 
Wanasababisha wenyewe bwana, nna rafik yang kaolewa lakini yupo close na babake balaa. hii ni sabb babake alkua hvyo alkua anamjulia hali sana kipindi tunasoma, wanaume badilikeni.
 
Mke mdogo nae anakuja anazikula mali zako yeye na watoto wake, daah kweli wanaume wanachezewa sana nchi hii...
 

Watoto wanajua kuwa baba ahudumiwa na mama kwa kila kitu wanajua wakimpatia mama baba naye atafaidi, tofauti na baba wengi ndiyo hao wanahonga nyumba ndogo.
 
This is a problem. Ila ninyi wamama ndiyo tatizo aisee.

Shida inaanza tangu watoto wakiwa wadogo, inafika siku ya sikukuu baba unamuachia mama pesa ya nguo za watoto mkiwa chumbani, mama akitoka anaanza, "wanangu nawapendaaa, twendeni nikawanunulie nguo nzuriii, mpendeze", watoto wanajua mama ndiyo katoa pesa. Watoto wanaanza kumhusudu mama.

Pili, mtoto anakosea, mama ananisubiri baba nikirudi ndiyo anamshtaki mtoto kwangu tena tukiwa faragha, mimi nikitoka chumbani ni bakora kwa kwenda mbele, halafu mama huyohuyo anaenda kumbembeleza, utasikia, "mwanangu mzuri, tema mate tukamchape baba!".

Yani nina mifano mingi sana ila sema tu nipo kwenye mazingira ambayo siyo rafiki.
 
Wewe ni mtoto kwa baba yako. Vipi unaliongeleaje hili?
 
[emoji736][emoji736][emoji736]
 
Word ☝☝☝☝
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…