Na unahisi hili jukwaa tungeliita ukumbi wa mkutano,ungenyoosha mkono uchangie kitu kama hiki ulichaondika?HAMIA KENYA AMBAKO ARDHI IKO MIKONONI MWA WATU WACHACHE
Kwa sababu Uhuru mwenyewe wakikuyu wenzake hawamtaki; na sababu kubwa ni kushikana mkono na Mluo, Raila; kabila ambalo halikubaliani kabisa na Kikuyu kihistoria.Hivie? Nasikia mwaka huu hata hawaangalii San mgombea anatoka wapi.Nimepata habar hata eneo alilopigia kura Uhuru Kenyatta,aliyeongoza kwa kura nyingi ni Ruto
Mkuu nimekupata vizuri.Nikiwa na swali nitakuuliza.Umejitahidi.
Mwanzo nilitaka kupuuza, lakini kadri nilivyosoma mada nikaona kweli umechanganyikiwa na siasa zilivyo Kenya.
Mkuu 'sepema', hakuna tofauti kati yetu na Kenya katika mambo ya msingi. Wote ni fursa tu kwa wanaojvisha kilemba cha uanasiasa.
Kama unataka kutafuta tofauti kati yao na sisi, tazama sehemu hizi mbili muhimu:
1. Ukabila
2. CCM
Tofauti zetu kubwa kwa sasa ni katika mambo haya mawili.
Hapa kwetu bila uwepo wa CCM, nasi pia tungekuwa na vyama vingi vinavyoibuka kila wakati wa uchaguzi ili kutafuta maslahi. Ila kwa kuwa bado ipo CCM inayounganisha wenye maslahi yao, basi tupo tofauti na Kenya. Wanaojiita viongozi wamejazana huko CCM wakijua maslahi yao huko ndiko yalipo; kwa nini wahangaike na kuanzisha vyama vingine?
Kenya, jambo muhimu kuliko yote ni kabila. Hata katika uchaguzi huu unaoonekana kuwa kama wa mfano kwa wengine, bado ukabila ndio msingi mkuu, na kila kiongozi anayetaka kuongoza ni lazima aweke kabila mbele, hasa kwa wakikuyu na Kalenjin na waluo. Ili ushindi upatikane ni lazima Kikuyu wakubali. au Kalenjini wakubali.
Kwa hiyo hivi vikabila vingine vyote, viongozi wa huko wanaunda tuvyama ili waweze kuungana na kile kinachoongozwa na Mkikuyu au Kalenjini au Mluo ili kutafuta maslahi
Hizi ni siasa za kilaghai, kama zilivyo zile za CCM hapa kwetu.
Sasas nimalizie kwa tahadhari: Tanzania nao tunaelekea kwenye miunganiko ya tuvyama, kama ilivyo Kenya. Hivi vyama vya mfukoni vinabebwa na CCM na huenda CHADEMA nao wakawa njiani kujiingiza ili na wao waweze kuingia serikalini wapate ulaji (maslahi). Bila shaka Samia na Mbowe bado wanalipika hili jinsi litakavyopakuliwa.
Uganda ni mali ya M7 kama Rwanda ilivyo mali ya Kagame kupitia kwenye vyama vyao vya kijeshi.
Kuna ngome za wagombea ambazo zinaweza kubadili upepo kwa hawa wagombea ifikapo kesho asubuhi ?#UCHAGUZIKENYA: Zoezi la kuhesabu kura linaendelea ambapo hadi kufikia Saa 02:32 Mchana, Mgombea wa Azimio la Umoja, Raila Odinga amejikusanyia kura 1,890,299 sawa na 49.58% huku Mgombea wa UDA, Naibu Rais William Ruto akiwa na kura 1,868,853 sawa na 49.02%
#ITVUchaguziKenyaUpdates
Nashukuru pia kwa hili.Nikiwa naswali lingine nitaomba ufafanuzi wako mkuu.Imenilazimu nirudi kuhusu hili:
Siyo kweli.
Kalonzo -Ukambani, ana watu wake, kabila la wakamba, ndiyo maana kila upande ulitaka aingie kwao
Mudavadi -Waluhya, yeye nguvu yake ni kuwapeleka waluhya upande wa Ruto
Karua na yule makamu wa Ruto, wapo huko kupeleka wakikuyu katika miungano waliyoteuliwa
Kule wameru, viongozi wao wakuu wengi wapo upande wa Ruto
Hali ni hivyo hivyo nchi nzima. Mugawanyiko ni wa viongozi kutafuta maslahi.
Miaka ya 80's alisema mwakasege alikua anatoka Kenya anakuja Tanzania akakaribia Namanga ghafla akaona anapotoka Kenya Kuna mwanga anapoelekea mbele ya boda Namanga Kuna Giza mpaka hapo utaelewa kwanin Kenya wapo tofauti na wengineWakuu heshima kwenu
Kwa miaka kadhaa nimekuwa nikifatilia siasa za nchi zetu za Afrika mashariki hususani kipindi Cha uchaguzi.
Rwanda na Uganda sijashuhudia chaguzi zao hivyo naziacha Kama zilivyo kwanza.
Katika nchi zinazounda jumuiya ya Afrika mashariki,ni Kenya tu ambayo ukiangalia siasa zao unaweza ushindwe kujua kuwa wanaigiza ama wapo serious na wanachokifanya.Nakama wapo serious nchi majirani tuige mifumo yao au tuachane nao?
Kenya hakuna chama Cha kisiasa chenye uhakika wa kutawala zaidi ya awamu mbili tangu ilivyoondoka KANU mwaka2002.
Kenya chama kinachompata raisi kinajifia mara tu utawala wa raisi husika unapokoma.Rejea kile chama kilichomuweka madarakani hayati Mwai Kibaki,na hata hiki kilichomuweka madarakani Uhuru Kenyatta.
Kenya hakuna kubebana kisiasa kwa kisingizio Cha tupo wote serikalini.Hii inajidhihirisha pale ambapo raisi Uhuru alivyokuwa kinyume na makamu wake kwenye kampeni huku akionekana dhahiri kumpigia kampeni mzee Raila Odinga.Pia ikumbukwe Kuna mawaziri walijigawa mapema wengine wakaenda kambi ya William Ruto huku wengine wakiwa upande wa Hapa unashindwa kuelewa kwenye vikao vya baraza la mawaziri wanakaaje na kuelewana kwenye Mambo muhimu ya kitaifa.
Kenya wanachagua raisi wao hata wakiwa nje ya Kenya.Uchaguzi huu wakenya walioko mabara mbalimbali wamepiga kura kwenye balozi zao.
Uhuru Kenyatta aliamua kuachana na chama Cha baba yake ambacho ndio chama Cha ukombozi nchini Kenya(KANU).
Wakuu,hii yakuachana na chama Cha baba walau kidogo inaweza kufanana na Ile ya Makongoro wa Tanzania aliyehamia NCCR nakuachana na CCM ya baba yake (japo alirudi).
Ninachoamini nikwamba hata baada yauchaguzi huu wa Kenya,chama kitakachoingia madarakani hakiwezi tena kujitokeza baada ya mihula miwili ya uongozi wake kupita(Kama kikichaguliwa kwa mihula miwili).
NB: Kila hoja niliyoandika nimeilinganisha na nchi ya Tanzania.
Naomba kusaidiwa;huu mfumo wa siasa na chaguzi za Kenya,unawezwa na wakenya peke yao ama hata sisi watanzania tunaweza kwenda nao?
Wasalaam!
Kwa kuongezea;
Wakenya hawapigi kura kwa kuangalia chama bali wanaangalia mtu, kwao chama baadae.Tofauti na nchi zingine ambazo chama chao kikishateua hata Kama ni boga litapigiwa kura za ndio.Ikibidi litasaidiwa kwa kuiba kura.
Kenya hawana vijana wanaoshinda na kukesha kwenye vibaraza vya ofisi za vyama vya siasa. Mambo ya vyama kwao yanasikika wakati wa uchaguzi tu.
Ni kwa sababu Uhuru alijiunga Kambi ya OdingaHivie? Nasikia mwaka huu hata hawaangalii San mgombea anatoka wapi.Nimepata habar hata eneo alilopigia kura Uhuru Kenyatta,aliyeongoza kwa kura nyingi ni Ruto
Kitu pekee tunachojitetea nacho ni ukabilaSiasa za ukabila lazima kuwe na Coalition,Tanzania hatuna huo ujinga ndio maana tuna vyama vyenye nguvu kama huko America.
Nimeona video babu Tale anagawa kanga afu yuko proud[emoji23]Kenya hakuna vikundi vya wajinga wanaogombea jezi za timu za mpira.
Wako serious na maswala na agenda za maisha yao.
Viongozi wa Sasa wa Kenya walishapelekwa the Hague na wakaonja joto la jiwe huko hivyo hawataki kurudia makosa yaliyowapeleka the Hague baada ya machafuko ya 2007.Wakuu heshima kwenu
Kwa miaka kadhaa nimekuwa nikifatilia siasa za nchi zetu za Afrika mashariki hususani kipindi Cha uchaguzi.
Rwanda na Uganda sijashuhudia chaguzi zao hivyo naziacha Kama zilivyo kwanza.
Katika nchi zinazounda jumuiya ya Afrika mashariki,ni Kenya tu ambayo ukiangalia siasa zao unaweza ushindwe kujua kuwa wanaigiza ama wapo serious na wanachokifanya.Nakama wapo serious nchi majirani tuige mifumo yao au tuachane nao?
Kenya hakuna chama Cha kisiasa chenye uhakika wa kutawala zaidi ya awamu mbili tangu ilivyoondoka KANU mwaka2002.
Kenya chama kinachompata raisi kinajifia mara tu utawala wa raisi husika unapokoma.Rejea kile chama kilichomuweka madarakani hayati Mwai Kibaki,na hata hiki kilichomuweka madarakani Uhuru Kenyatta.
Kenya hakuna kubebana kisiasa kwa kisingizio Cha tupo wote serikalini.Hii inajidhihirisha pale ambapo raisi Uhuru alivyokuwa kinyume na makamu wake kwenye kampeni huku akionekana dhahiri kumpigia kampeni mzee Raila Odinga.Pia ikumbukwe Kuna mawaziri walijigawa mapema wengine wakaenda kambi ya William Ruto huku wengine wakiwa upande wa Hapa unashindwa kuelewa kwenye vikao vya baraza la mawaziri wanakaaje na kuelewana kwenye Mambo muhimu ya kitaifa.
Kenya wanachagua raisi wao hata wakiwa nje ya Kenya.Uchaguzi huu wakenya walioko mabara mbalimbali wamepiga kura kwenye balozi zao.
Uhuru Kenyatta aliamua kuachana na chama Cha baba yake ambacho ndio chama Cha ukombozi nchini Kenya(KANU).
Wakuu,hii yakuachana na chama Cha baba walau kidogo inaweza kufanana na Ile ya Makongoro wa Tanzania aliyehamia NCCR nakuachana na CCM ya baba yake (japo alirudi).
Ninachoamini nikwamba hata baada yauchaguzi huu wa Kenya,chama kitakachoingia madarakani hakiwezi tena kujitokeza baada ya mihula miwili ya uongozi wake kupita(Kama kikichaguliwa kwa mihula miwili).
NB: Kila hoja niliyoandika nimeilinganisha na nchi ya Tanzania.
Naomba kusaidiwa;huu mfumo wa siasa na chaguzi za Kenya,unawezwa na wakenya peke yao ama hata sisi watanzania tunaweza kwenda nao?
Wasalaam!
Kwa kuongezea;
Wakenya hawapigi kura kwa kuangalia chama bali wanaangalia mtu, kwao chama baadae.Tofauti na nchi zingine ambazo chama chao kikishateua hata Kama ni boga litapigiwa kura za ndio.Ikibidi litasaidiwa kwa kuiba kura.
Kenya hawana vijana wanaoshinda na kukesha kwenye vibaraza vya ofisi za vyama vya siasa. Mambo ya vyama kwao yanasikika wakati wa uchaguzi tu.
Sehemu yeyote yenye ukabila na majimbo au kaunti kama wanavyoita huko huwa na vyama vya coalition,refer ujerumani,Nigeria nk..Kitu pekee tunachojitetea nacho ni ukabila
Doooh!Tanzania raia wake hatujitambui sijui tulirogwa na nani? Yaani kama maiti fikilia hata ngumi anatamba aliyepigwa na jamii inampa madili! Kwa sababu wengi tunaroho mbaya na umasikini umetujaa tumekalia umbeya tu! Ukimwambia mtu tunataka katiba mpya hakuelewi! Basi tume huru ya uchaguzi pia hataki kuisikia sielewi aliyeturoga!
Katika tathmini au uoni wako hapo ndo umeona vizuri, ila hujaona kwa undani.Kenya hakuna chama Cha kisiasa chenye uhakika wa kutawala zaidi ya awamu mbili tangu ilivyoondoka KANU mwaka2002.
Nimepata uelewa flan hapaKatika tathmini au uoni wako hapo ndo umeona vizuri, ila hujaona kwa undani.
Kenya kuna chama kimoja kikuu cha siasa. Chama hicho ni kabila na ukanda.
Ukanda wanaojiita "watu wa milimani" yaani wakikuyu na wakalenjini na wengineo wa maeneo ya Mlima Kenya ndiyo wanaotawala.
Asili ya hawa watu kutawala ni kwamba Mzungu anapenda sehemu za baridi kama vile Iringa na Mbeya. Kwa hiyo Mzungu alipovamia Kenya alikwenda moja kwa moja kukaa maeneo ya baridi na mji mkuu akaweka Nairobi ambako ni eneo la baridi.
Ili mzungu akae ilibidi awafukuze waAfrika waliokuwa wanaishi hapo, wengi wao wakiwa ni waKikuyu. Aliwafukuza halafu akachukua ardhi yao akalima kahawa, na ili waAfrika hao waje kumfanyia kazi kama manamba akatunga sheria ya kodi ya kichwa, ambayo usipolipa unaadhibiwa kwa kudhalilishwa kwa kuchapwa viboko hadharani eneo la sokoni, au mbele ya mke na watoto wako. Au ukiwa sugu zaidi unafungwa jela.
Kwa hiyo wale walioporwa ardhi wakajikuta tena wanalazimika kuwa watumwa kumlimia mzungu kahawa zake ili wapate pesa ya kulipa kodi. Maana pesa halali ilikuwa ni ile anayochapisha mzungu.
Hapa ndo watu wa milimani wakapata hasira mara kumi dhidi ya mzungu na kuhakikisha wanapigana naye kufa na kupona aondoke kwenye ardhi yao.
Mzungu kwa kutambua kuwa hawa watu aliowapora ardhi wanamchukia akaenda kwa wajaluo ambao ni watu wa bondeni kwenye ufukwe wa ziwa Nyaza ila aliowaona wana akili za darasani. Hawa ndo akawapa kipaumbele cha kuwasomesha elimu yake ili wamsaidie kazi za kiutawala ofisini. Hakutaka wakikuyu na wakalenjini ambao alikuwa amewapora ardhi wasome na kukaa maofisini maana wangemhujumu.
Wajaluo ni wapenda sifa sana, na kitendo cha kutunukiwa hadhi hiyo na Mzungu kikawavimbisha vichwa, wakajikuta wanafurahi kushiriki kwenye ukoloni.
Kitendo hiki kiliwachukiza sana wakikuyu na wakalenjini. Hivyo harakati zao za kudai uhuru zilipofanikiwa waliapa kwamba Mjaluo hatakuja kutawala Kenya!
Hizo ndo siasa za Kenya. Hivyo vyama vinavyobadilika kila msimu wa uchaguzi visikusumbue. Na katu usije ukapiga debe kwamba Tanzania iige siasa za Kenya. Tuna urithi tofauti kidogo kati yetu na wao.
Wajaluo nao wana hasiria sana kwa sababu ya kuwekwa kando kwa miaka 59 sasa, kwa hiyo Uhuru Kenyatta ni kama aliona awahurumie kidogo. Aidha ni hivyo au ni mchezo tu wa kisiasa kwa sababu katika siasa mara nyingi sana mgombea anayeungwa mkono na Rais anayemaliza muda wake huwa anakataliwa na wapiga kura. Kwa hiyo kama wewe ni Rais ukitaka kumsaidia mgombea wakati mwingine ni vizuri ukampiga vita waziwazi ili wananchi wakuchukie wewe Rais unayeondoka na wamuunge mkono mgombea uliyesema humtaki.
Watu wa Pwani wao kwa kuona wametengwa katika hili bifu kuu la kati ya watu wa milimani dhidi ya wajaluo wao wakaona watangaza kujitenga. Walifanya kampeni na vuguvugu la Pwani si Kenya mwaka 2010-2011 wakitangaza Jamhuri ya Mombasa kuwa ni jamhuri huru iliyojitenga kutoka kwenye Jamhuri ya Kenya. Hii ilitokana na vita iliyoibuka kati ya watu wa milimani na Wajaluo kufuatia uchaguzi wa Rais wa Kenya wa mwaka 2007 ambapo Wajaluo waliona mtu wao Raila Odinga amenyang'anywa ushindi.
View attachment 2320307 View attachment 2320312
Nimepata uelewa flan hapaKatika tathmini au uoni wako hapo ndo umeona vizuri, ila hujaona kwa undani.
Kenya kuna chama kimoja kikuu cha siasa. Chama hicho ni kabila na ukanda.
Ukanda wanaojiita "watu wa milimani" yaani wakikuyu na wakalenjini na wengineo wa maeneo ya Mlima Kenya ndiyo wanaotawala.
Asili ya hawa watu kutawala ni kwamba Mzungu anapenda sehemu za baridi kama vile Iringa na Mbeya. Kwa hiyo Mzungu alipovamia Kenya alikwenda moja kwa moja kukaa maeneo ya baridi na mji mkuu akaweka Nairobi ambako ni eneo la baridi.
Ili mzungu akae ilibidi awafukuze waAfrika waliokuwa wanaishi hapo, wengi wao wakiwa ni waKikuyu. Aliwafukuza halafu akachukua ardhi yao akalima kahawa, na ili waAfrika hao waje kumfanyia kazi kama manamba akatunga sheria ya kodi ya kichwa, ambayo usipolipa unaadhibiwa kwa kudhalilishwa kwa kuchapwa viboko hadharani eneo la sokoni, au mbele ya mke na watoto wako. Au ukiwa sugu zaidi unafungwa jela.
Kwa hiyo wale walioporwa ardhi wakajikuta tena wanalazimika kuwa watumwa kumlimia mzungu kahawa zake ili wapate pesa ya kulipa kodi. Maana pesa halali ilikuwa ni ile anayochapisha mzungu.
Hapa ndo watu wa milimani wakapata hasira mara kumi dhidi ya mzungu na kuhakikisha wanapigana naye kufa na kupona aondoke kwenye ardhi yao.
Mzungu kwa kutambua kuwa hawa watu aliowapora ardhi wanamchukia akaenda kwa wajaluo ambao ni watu wa bondeni kwenye ufukwe wa ziwa Nyaza ila aliowaona wana akili za darasani. Hawa ndo akawapa kipaumbele cha kuwasomesha elimu yake ili wamsaidie kazi za kiutawala ofisini. Hakutaka wakikuyu na wakalenjini ambao alikuwa amewapora ardhi wasome na kukaa maofisini maana wangemhujumu.
Wajaluo ni wapenda sifa sana, na kitendo cha kutunukiwa hadhi hiyo na Mzungu kikawavimbisha vichwa, wakajikuta wanafurahi kushiriki kwenye ukoloni.
Kitendo hiki kiliwachukiza sana wakikuyu na wakalenjini. Hivyo harakati zao za kudai uhuru zilipofanikiwa waliapa kwamba Mjaluo hatakuja kutawala Kenya!
Hizo ndo siasa za Kenya. Hivyo vyama vinavyobadilika kila msimu wa uchaguzi visikusumbue. Na katu usije ukapiga debe kwamba Tanzania iige siasa za Kenya. Tuna urithi tofauti kidogo kati yetu na wao.
Wajaluo nao wana hasiria sana kwa sababu ya kuwekwa kando kwa miaka 59 sasa, kwa hiyo Uhuru Kenyatta ni kama aliona awahurumie kidogo. Aidha ni hivyo au ni mchezo tu wa kisiasa kwa sababu katika siasa mara nyingi sana mgombea anayeungwa mkono na Rais anayemaliza muda wake huwa anakataliwa na wapiga kura. Kwa hiyo kama wewe ni Rais ukitaka kumsaidia mgombea wakati mwingine ni vizuri ukampiga vita waziwazi ili wananchi wakuchukie wewe Rais unayeondoka na wamuunge mkono mgombea uliyesema humtaki.
Watu wa Pwani wao kwa kuona wametengwa katika hili bifu kuu la kati ya watu wa milimani dhidi ya wajaluo wao wakaona watangaza kujitenga. Walifanya kampeni na vuguvugu la Pwani si Kenya mwaka 2010-2011 wakitangaza Jamhuri ya Mombasa kuwa ni jamhuri huru iliyojitenga kutoka kwenye Jamhuri ya Kenya. Hii ilitokana na vita iliyoibuka kati ya watu wa milimani na Wajaluo kufuatia uchaguzi wa Rais wa Kenya wa mwaka 2007 ambapo Wajaluo waliona mtu wao Raila Odinga amenyang'anywa ushindi.
View attachment 2320307 View attachment 2320312
Wakuu heshima kwenu
Kwa miaka kadhaa nimekuwa nikifatilia siasa za nchi zetu za Afrika mashariki hususani kipindi Cha uchaguzi.
Rwanda na Uganda sijashuhudia chaguzi zao hivyo naziacha Kama zilivyo kwanza.
Katika nchi zinazounda jumuiya ya Afrika mashariki,ni Kenya tu ambayo ukiangalia siasa zao unaweza ushindwe kujua kuwa wanaigiza ama wapo serious na wanachokifanya.Nakama wapo serious nchi majirani tuige mifumo yao au tuachane nao?
Kenya hakuna chama Cha kisiasa chenye uhakika wa kutawala zaidi ya awamu mbili tangu ilivyoondoka KANU mwaka2002.
Kenya chama kinachompata raisi kinajifia mara tu utawala wa raisi husika unapokoma.Rejea kile chama kilichomuweka madarakani hayati Mwai Kibaki,na hata hiki kilichomuweka madarakani Uhuru Kenyatta.
Kenya hakuna kubebana kisiasa kwa kisingizio Cha tupo wote serikalini.Hii inajidhihirisha pale ambapo raisi Uhuru alivyokuwa kinyume na makamu wake kwenye kampeni huku akionekana dhahiri kumpigia kampeni mzee Raila Odinga.Pia ikumbukwe Kuna mawaziri walijigawa mapema wengine wakaenda kambi ya William Ruto huku wengine wakiwa upande wa Hapa unashindwa kuelewa kwenye vikao vya baraza la mawaziri wanakaaje na kuelewana kwenye Mambo muhimu ya kitaifa.
Kenya wanachagua raisi wao hata wakiwa nje ya Kenya.Uchaguzi huu wakenya walioko mabara mbalimbali wamepiga kura kwenye balozi zao.
Uhuru Kenyatta aliamua kuachana na chama Cha baba yake ambacho ndio chama Cha ukombozi nchini Kenya(KANU).
Wakuu,hii yakuachana na chama Cha baba walau kidogo inaweza kufanana na Ile ya Makongoro wa Tanzania aliyehamia NCCR nakuachana na CCM ya baba yake (japo alirudi).
Ninachoamini nikwamba hata baada yauchaguzi huu wa Kenya,chama kitakachoingia madarakani hakiwezi tena kujitokeza baada ya mihula miwili ya uongozi wake kupita(Kama kikichaguliwa kwa mihula miwili).
NB: Kila hoja niliyoandika nimeilinganisha na nchi ya Tanzania.
Naomba kusaidiwa;huu mfumo wa siasa na chaguzi za Kenya,unawezwa na wakenya peke yao ama hata sisi watanzania tunaweza kwenda nao?
Wasalaam!
Kwa kuongezea;
Wakenya hawapigi kura kwa kuangalia chama bali wanaangalia mtu, kwao chama baadae.Tofauti na nchi zingine ambazo chama chao kikishateua hata Kama ni boga litapigiwa kura za ndio.Ikibidi litasaidiwa kwa kuiba kura.
Kenya hawana vijana wanaoshinda na kukesha kwenye vibaraza vya ofisi za vyama vya siasa. Mambo ya vyama kwao yanasikika wakati wa uchaguzi tu.