Kila tunapokaribia duru za uchaguzi wa Serikali za Mitaa vuguvugu na joto la siasa linapanda. Kuna suala la wabunge 19 walikuwa CHADEMA na ambao suala lao liko mahakamani.
Hawa wabunge walifukuzwa uanachama na Kamati Kuu na kupata baraka za Baraza Kuu baada ya rufaa zao, na kisha suala hilo kuishia mahakamani.
Mazingira ya shauri hilo kisiasa ni kwamba serikali ilicheza faulo kubwa kwenye uchaguzi kwa nia ya kuifuta Chadema na upinzani wote, ikajikuta imepitiliza na hivyo kukosa upinzani Bungeni, hali iliyopelekea kukosa kigezo cha misaada kutoka nje kwa misingi wa kidemokrasia.
Suluhisho ikawa kuendeleza faulo kwa kuwapata wabunge 19 ili kujenga uhalali wa uwepo wa upinzani bungeni na demokrasia ili kupata misaada ya kibunge. Upande wa pili, wabunge hao nao wakaona uwezekano wa kuchaguliwa kuingia Bungeni kupitia chama chao( haupo) haiwezekani kwa vile CHADEMA ilikataa kupeleka wawakilishi Bungeni kwa hali iliyokuwa imejitokeza.
Soma Pia: CHADEMA mmejipangaje na wabunge 19 wa viti maalumu kutorudi bungeni tena mwaka 2025/26?
Awamu ya tano kwa mabavu ikawapata akina Halima( nao wakati ule wana hali mbaya ya kiuchumi) wakawa hawana namna. Na ni kwa sababu hiyo hiyo wameng'ang'ania bungeni na mamlaka kuwakumbatia(marriage of convenience). Kuna fununu wapo baadhi wangependa kurudi kundini. Nini kifanyike:
1. Hawa wana siasa ni nguli na wazuri pamoja na madhaifu yao,hivyo nashauri wale wenye nia ya kurudi wakubaliwe ili mradi taratibu zifuatwe.
2. Kila" case" ya mbunge iamuriwe kwa uzito wake"on its own merit" na kamati kuu na baraza watakapoomba kurudi. Huku mkizingatia mazingira ya siasa za wakati ule na sasa ni tofauti mno.
3. Ifanyike Cost/ benefit analysis ya kuwarudisha na kutowarudisha. Siasa ni "dynamic" na ni "game of chance" na uimara wa chama ni wanachama na wapenzi wenyewe.
4.Siasa haina urafiki na uadui wa kudumu
5. "Rigidity" kwenye siasa ni mbaya na ujenzi wa chama ni zoezi la "flexibility" huku mkizingatia malengo ya chama. kushupaza shingo ni kukosa weredi wa kushughulikia mambo kwa uhalisia wake.
Hawa wabunge walifukuzwa uanachama na Kamati Kuu na kupata baraka za Baraza Kuu baada ya rufaa zao, na kisha suala hilo kuishia mahakamani.
Mazingira ya shauri hilo kisiasa ni kwamba serikali ilicheza faulo kubwa kwenye uchaguzi kwa nia ya kuifuta Chadema na upinzani wote, ikajikuta imepitiliza na hivyo kukosa upinzani Bungeni, hali iliyopelekea kukosa kigezo cha misaada kutoka nje kwa misingi wa kidemokrasia.
Suluhisho ikawa kuendeleza faulo kwa kuwapata wabunge 19 ili kujenga uhalali wa uwepo wa upinzani bungeni na demokrasia ili kupata misaada ya kibunge. Upande wa pili, wabunge hao nao wakaona uwezekano wa kuchaguliwa kuingia Bungeni kupitia chama chao( haupo) haiwezekani kwa vile CHADEMA ilikataa kupeleka wawakilishi Bungeni kwa hali iliyokuwa imejitokeza.
Soma Pia: CHADEMA mmejipangaje na wabunge 19 wa viti maalumu kutorudi bungeni tena mwaka 2025/26?
Awamu ya tano kwa mabavu ikawapata akina Halima( nao wakati ule wana hali mbaya ya kiuchumi) wakawa hawana namna. Na ni kwa sababu hiyo hiyo wameng'ang'ania bungeni na mamlaka kuwakumbatia(marriage of convenience). Kuna fununu wapo baadhi wangependa kurudi kundini. Nini kifanyike:
1. Hawa wana siasa ni nguli na wazuri pamoja na madhaifu yao,hivyo nashauri wale wenye nia ya kurudi wakubaliwe ili mradi taratibu zifuatwe.
2. Kila" case" ya mbunge iamuriwe kwa uzito wake"on its own merit" na kamati kuu na baraza watakapoomba kurudi. Huku mkizingatia mazingira ya siasa za wakati ule na sasa ni tofauti mno.
3. Ifanyike Cost/ benefit analysis ya kuwarudisha na kutowarudisha. Siasa ni "dynamic" na ni "game of chance" na uimara wa chama ni wanachama na wapenzi wenyewe.
4.Siasa haina urafiki na uadui wa kudumu
5. "Rigidity" kwenye siasa ni mbaya na ujenzi wa chama ni zoezi la "flexibility" huku mkizingatia malengo ya chama. kushupaza shingo ni kukosa weredi wa kushughulikia mambo kwa uhalisia wake.