Wabunge 35 wa Tanzania Washiriki Mafunzo ya APSEZ Nchini India

Wabunge 35 wa Tanzania Washiriki Mafunzo ya APSEZ Nchini India

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

WABUNGE 35 KWENYE MAFUNZO YA APSEZ NCHINI INDIA

Wabunge 35 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka kamati mbalimbali za Bunge hilo wapo katika ziara ya mafunzo Nchini India, kujifunza kuhusu ushirikishaji wa Sekta binafsi katika Uwekezaji, Usimamizi na Uendelezaji kwenye shughuli za bandari kutoka APSEZ, ambayo ni kampuni kubwa iliyowekeza Katika Bandari 13 ndani na nje ya India.

Wabunge hao wameongozwa na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa, ambaye katika mafunzo hayo ametoa maelezo ya utangulizi kuhusu ziara ya Mafunzo kwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waliotembelea Makao Makuu ya kampuni ya Adani Ports and Special Economic Zone Limited ( APSEZ) mjini Ahmedabad, Jimbo la Gujarat Nchini India.

Baadhi ya Wabunge hao walioshiriki mafunzo ya APSEZ Mjini Ahmedabad ni pamoja na Mhe. Prof Makame Mbarawa (Waziri), Mhe. Atupele Mwakibete (NW), Mhe. Juliana Shonza, Mhe. Rose Tweve, Mhe. Nicholaus Ngassa, Mhe. Lucy John Sabu, Mhe. Erick Shigongo, Mhe. Festo Sanga, Mhe. Kasalali Mageni, Asia Halamga na wengine wengi.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-03-11 at 13.37.45(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-03-11 at 13.37.45(1).jpeg
    39.6 KB · Views: 5
  • WhatsApp Image 2023-03-11 at 13.37.45(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-03-11 at 13.37.45(2).jpeg
    47.9 KB · Views: 5
  • WhatsApp Image 2023-03-11 at 13.37.47(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-03-11 at 13.37.47(1).jpeg
    45.8 KB · Views: 5
  • WhatsApp Image 2023-03-11 at 13.37.48.jpeg
    WhatsApp Image 2023-03-11 at 13.37.48.jpeg
    33.2 KB · Views: 5
  • WhatsApp Image 2023-03-11 at 13.37.45.jpeg
    WhatsApp Image 2023-03-11 at 13.37.45.jpeg
    31.4 KB · Views: 5
Zile ziara na semina zisizokuwa na tija zimerejea tena.

Hapo unakuta gharama za kusafirisha delegate yote hiyo inatosha kujenga madarasa kadhaa na madawati.

Halafu tunakwenda kukopa fedha kwa mambo ambayo yapo ndani ya uwezo wetu.
 
Zile ziara na semina zisizokuwa na tija zimerejea tena.

Hapo unakuta gharama za kusafirisha delegate yote hiyo inatosha kujenga madarasa kadhaa na madawati.

Halafu tunakwenda kukopa fedha kwa mambo ambayo yapo ndani ya uwezo wetu.
Kama hukubaliani na haya, Dawa tuiondowe Ccm madarakani, unasemaje?
 
Ni style ya kuboost kipato kwa njia halali.

Magufuli hata haya alikuwa hataki, huwezi kuwabana watu hata kuingiza pesa halali kwa njia halali.

Ni kweli ni ulaji tu hapo lakini kwa njia halali.
Hao wanaenda kujifunza nini huko , matumizi mabaya ya fedha za umma , kuna siku tutasweka ndani for miuses of public fund...mjomba alipiga pini huu upuuzi .....
 
Hao wanaenda kujifunza nini huko , matumizi mabaya ya fedha za umma , kuna siku tutasweka ndani for miuses of public fund...mjomba alipiga pini huu upuuzi .....
Dunia ya leo ni Dunia ya utandawazi ,Dunia iko kiganjani sasa haya mambo ya kwenda kujifunza physically niya kipindi cha miaaka 100 iliyopita ,,tukisema kijani inadumaza uchumi wa nchi hii muwe mnatuelewana ndugu wananchi....
 
Hiyo Kampuni ya India utakuta inajenga Mazingira ya kupewa Bandari yetu baada ya TICS!
Ulale pema Hayati Dr. Magufuli, yale maujinga ujinga yamerudi tena kwa kasi!
 
Hiyo kampuni ikija kupewa uendeshaji wa bandari nchini nani atashangaa
Nikiangalia majina ya wabunge hao sioni hata mmoja atakayeleta tija yoyote
 
Hiyo Kampuni ya India utakuta inajenga Mazingira ya kupewa Bandari yetu baada ya TICS!
Ulale pema Hayati Dr. Magufuli, yale maujinga ujinga yamerudi tena kwa kasi!
Inajenga mazingira au imeshapewa? Unachelewa sana kupata habari
 
Hatuna wabunge wakuleta manufaa tunao machawa wa prezoo kila anayeingia ikulu wao ni kumsifu na kumshukuru kuliko wamshukuruvyo Muumba
 
Back
Top Bottom