Wabunge 46 na mawaziri 13 wahamasisha wananchi kutaka JK ajiuzulu

Kichuguu,
Mkuu nakubaliana sana na maelezo yako na hakika hii habari nzima inaonyesha wazi jinsi JK alivyokuwa na wakati mgumu ndani ya chama chake..
Kinachonishinda mimi kuelewa ni hizi kampeni kupingwa na wana mazingira kama kweli zipo..
Naweza kukubali kuwepo kwake kwa sababu zilizotolewa kwani chombo hiki cha Haki za binadamu na mazingira kipo mikoa yote na huyu mchungaji ni msemaji mwakilishi wa chombo hicho hivyo sii mawazo yake binafsi ila yeye ni mwakilishi wa mawazo ya wanaharakati wa chombo hicho..
Hadi hapa, sioni kosa lolote la huyu mchungaji ikiwa anaifanya kazi yake..
Tatizo linakuja naposoma habari nzima kuhusu hawa mawaziri 13 na Wabunge 46 ambao wameshindwa kuwakilisha mawazo yao bungeni badala yake wanaendesha kampeni chini chini huko mikoani..
Kimsingi madai yao yana nguvu sana hasa wanaposema kuwa Rais ajiuzulu kwa sababu Serikali yake imeshindwa kutekeleza maazimio ya Bunge..

Hii sababu kama ingeandamana na maelezo kamili yanayohusiana na maazimio ambayo yalipitishwa na bunge JK kashindwa kuyatekeleza ingetusaidia sana wananchi kuelewa zaidi kwani hadi leo hii madai mengi ya wananchi yanatokana na ahadi za JK, sio maazimio yaliyopitishwa na bunge letu...

Sasa ikiwa hawa wabunge na mawaziri ni katika fungu la Mafisadi ningependa sana kuelewa hayo maazimio yaliyopitishwa ambayo JK kashindwa kuyatekeleza..Ina niuwia vigumu kufikiria kwa fikra zangu hawa Mafisadi wanaweza vipi kuendesha kampeni kama hizi wakati JK anafanya kila analoweza kuwalinda. Je, ni Maazimio yapi hayo!

Na sio kweli kabisa kuwa JK ni kiongozi bora kuliko wote ama amekuwa na wakati mgumu kuliko Nyerere.. Haya ni matusi kwa mwalimu, JK amepewa nchi ikiwa katika hali nzuri sana kiuchumi na kama tunazungumzia Mafisadi tukumbuke tu kwamba Ufisadi ni kama crimes nyingine zozote zile. Zilikuwepo na zitaendelea kuwepo isipokuwa kusimamisha kwa sheria ndio njia pekee ya kulinda na kuondoa maradhi haya..
Lowassa, Rostam kina Patel na wengine wote ni kizazi kipya cha Ufisadi ambao wameibuka baada ya sisi kuachia milango wazi hata iwe kwa amri ya Mkapa..Nina hakika kama JK au Mwinyi au Mkapa ndio wangeutafuta Uhuru wa Tanzania basi hadi leo hii tungekuwa tukitawaliwa na hawa wote wasingeweza Upinzani wa kina Fundikira, Marealle, Mtenvu na mgawanyiko wa makabila yote tulokuwa nayo.. nasema hivi jamani, temea mate chini, umlaani shetani kwanihawa wote kina Mwinyi, Mkapa na JK wameikuta nchi imeshawekwa sawa...

JK anaweza kabisa kupunguza au hata kusimamisha Grand Corruption kwa siku moja kwa sababu wahalifu wanafahamika na ushahidi upo wazi kabisa... hakuna mtu anayemlaumu JK kwa kushindwa kuondoa corruption, haya niu maradhi hayawezi kwisha kabisa kwani crimes ni sawa maradhi ya binadamu, mfano wa Maleria..Hatuwezi kabisa kuondoa mardhi haya ikiwa mbu wataendelea kuzaana na hakuna jitihada zinazofanywa kuzuia mbu kuzaana, kinga na hata dawa za mbu..Mfumo wa utawala wa JK hivi sasa umeshindwa kabisa kufanya hata mojawapo ktk kupambana na Ufisadi zaidi ya kutambua tatizo la kuwepo maradhi haya..

Sifa zote anazopewa JK ni kutokana na kutambua kwake au niseme kukubali kuwa Tanzania ina tatizo kubwa la corruption lakini ameshindwa kabisa kuzuia mafisadi kuzaana. kuweka kinga na hata kutumia dawa ya kuua mafisadi ambayo ni kuwafikisha mahakamani akiendelea kudai kufanya utafiti zaidi...hali tayari serikali yake imesha toa diagnosis kuwa maradhi haya yapo na ndiyo yanayoua uchumi wa nchi yetu..

Jamani, tujiulize sote pamoja na mapenzi yetu kwa rais, chama au hata nchi yetu.. Kikwete ameweza kufanya nini ktk vita dhidi ya Mafisadi ili kukinga, kuzuia au hata kupambana na ufisadi ikiwa vyombo vilivyopo havitendi kazi yake kabisa!..

Tunachokiona kila siku katika magazeti ni vita baina ya mafisadi na wazalendo, Hivi kweli Kikwete akiambiwa Kipindupindu kimeingia Mbeya na kimeisha ua watu bado atataka ushahidi upi ikiwa wanamazingira watamwambia virusi vya Kipindsupindu vimebainika, bado atahitaji ushahidi gani zaidi..au kwa sababu hapa ana deal na maswahiba wake!.. imekuwa kama hadithi ya Wakerewe hawawezi kumuua nyoka Chatu, hata kama huyo nyoka amemeza mbuzi wake kwa sababu wanaamini kuua Chatu ni mkosi ktk familia..
Hivyo ni kweli JK anachemsha lakini naposikia kwamba hawa mawaziri na wabunge ni ktk kundi la Mafisadi nashindwa kuunganisha kabisa kwani JK amewalinda sana na hakika mdanganyika kwa hulka hana shukran..
Mtu kama Lowasssa aemjaa chuki miaka yote, hana rafiki isipokuwa kwa yule anayemwabudu yeye. Ukiwa mshindani wake tu iwe hata kimawazo basi wewe ni adui yake na yupo tayari kutumia kila njia ktk uwezo wake akumalize!..

Pamoja na yote haya ningependa sana kuelewa hawa wabunge na mawaziri wanapotaka JK ajiuzulu wao wanataka nani ashike nchi badala yake.. Shein au Sitta!..
 
Last edited:
Wanaharakati hao wamewataja wabunge 46 na mawaziri 13 ambao walisema wamekuwa wakizunguka maeneo mbalimbali nchini kuwahamasisha wananchi waunge mkono ajenda yao ya kumtaka Rais ajiuzulu.


Hii habari vipi?Kama wamewataja hao wabunge mbona hakuna majina?Ama tunachangia based on speculations?Ilitakiwa waandike kuwa wanaharakati hao wamesema kuwa kuna wabunge 46 na si kuandika kuwa wametajwa na wakati hakuna majina yaliyotajwa.
Halafu heading inasema wabunge 46 na mawaziri 13 wawahamasisha wananchi kutaka JK ajiuzulu,lakini ndani ni habari za hao wanaharakati wakiongozwa na mchungaji....Habari hii naona imetolewa nusu nusu. Wabunge 46 ni wengi,halafu hatujui kama hao mawaziri 13 ni miongoni mwa hao hao wabunge 46,kama sivyo,then hao mawaziri ambao ni lazima wawe wabunge kwanza,nao pia wakijumuishwa wanakuwa ni wabunge59 jumla bila kujali kama ni mawaziri ama la,ni vema tukawajua ni wakina nani hao.
 
Mangi where have you been?

Mkuu summer iko busy kidogo,siko off kama nilivyotarajia,i do have a few classes ndio maana,hata hivyo nimemiss sana jamvi na i will be around as much as i can afford to...Tuko pamoja hamna shida Mungu anasaidia.
 
mie naona kikwete ni weak sana kuliko watu walivyo mtegemea.

Change we can believe in- Itaanza kipindi cha pili cha Kikwete, mtajuuuuta kumwita Weak, kusema uongozi umemshinda, kusema mwoga. Tutamkumbuka Mkapa na kusema alikuwa mpole. Nyie subirini. Mabadiliko makubwa yaja, maadui watapondwapondwa, mafisadi watafinyangwa. Tumpe Kikwete kipindi cha pili jamani alete mabadiliko, kwani kipindi cha kwanza kilikuwa cha kulipa fadhila kwa waliomuweka kipindi cha pili atakuwa kasimama mwenyewe na hapo sasa ndipo atajenga historia katika uongozi wetu kwa kuwa rais wa kwanza kuruhusu madiliko makubwa ndani ya nchi bila kujali itikadi ya Chama.
 

Mkuu una maana kuwa hao atakaowaponda ponda na kuwafinyanga ndio hao hao ambao ameona awalipe fadhila kwanza kabla ya kuwafanyia mambo hayo second term?Ama kuna tofauti kati ya waliomweka madarakani na mafisadi?Weka wazi hapo ili tuelewe mkuu unless maadui wake sio waliomweka madarakani na waliomweka madarakani sio mafisadi.
 

Mkuu angalia, usiwaachie watoto wakaandika comment kama hizi, watu watafikirini wewe! hata mimi imeshawahi kunitokea! watoto hao hawajui kujiuliza kwanza na kuwaza hewa na kujiridhisha na upepo.

Kwa kumjibu ni kuwa JK hana sababu ya kusubiri au kulipa fadhila! an kila kitu, kama analipa fadhila basi ni kwa wale walioiba fedha benki na kumweka madarakani , kwa maana nyingine sentensi zako za kwanza ameshamuhukumu JK kuwa ni fisadi , amewekwa kifisadi, JE FADHILI ALIZOZILIPA NI NINI? SI KUWAACHIA MAFISADI WAZIDI KUIFISADI NCHI NGAU KIDOGO! THEN NDIO AANZE KUWA MSAFI!

ELEZA AMELIPAJE FADHILA!
 
Hao Mawaziri na Wabunge wako wapi? wanatakiwa wajulikane kwanza.......ujue wakishajulikana ndio hata wananchi wanaweza kuwapa support au sio?
 
Wameyataja hayo majina mtungini au kwenye Kibuyu watu wakashindwa kuyasikia? Hii habari ina ukweli wowote??. Kama wametajwa then hii habari haijakamilika, ni UZUSHI tu. Lete majina hapa....
 

Mkuu kama kweli wewe unaishi kwenye dunia halisi, basi utakuwa unajua ukweli wa mambo yanayotokea Tanzania. Pamoja na kuwa Mkapa alitulaghai, huwezi kumlinganisha na JK hata Kidogo kwa angle yoyote ile ya uongozi. Kikwete ameonesha uwezo mdogo sana wa utawala na ameonesha udhaifu mkubwa.
Kutokana na experience ya miaka mitano( Mitano kasoro) ya uongozi wake, hakuna kitu chochote anachoweza kutuambia tumchague tena, labda wapiga kura wote wawe ni wale wa pilau, T-shirt, na elfu 5 tano. Ni Rais Handsome, ambaye alikuwa na opportunity nzuri ya kufanya maajabu na kuiendeleza Tanzania. Mambo ambayo rais ambaye hakuwa na mvuto kama Mkapa hakuweza kufanya JK angeweza. JK alikuwa na uwezo wa kupitisha hata bomoabomoa na asilaaniwe na watu, lakini Mkapa alihitaji FFU. Pampja na hilo JK hakuna alilofanya mpaka sasa zaidi ya kujilinda against mafisadi wanaomsumbua kila kukicha.
Kwa hiyo si kweli kuwa JK ni rais bora kabisa Tanzania kuwahi kutokea, na sio kweli kuwa Tanzania hiwezi kupata Rais mzuri kama yeye. Kuna watanzania wengi tu ambao hatuwajui wanaweza kuwa marais wazuri.
 

Mkuu unachosema ni kama ndoto za alinacha. Sidhani kama baada ya kipindi cha kwanza atakuwa amewafikisha mafisadi wote kwenye mkono wa sheria, sidhani kama ya kwake yatakuwa yamefutwa, sidhani kama anaweza kutekeleza manifesto ya chama kwa kiwango chohcote kile, nyota njema huonekana tangu asubuhi. Mafisadi wana-leverage nyingi tu againts JK, wanaweza kumlipua at anytime na akaonekana vibaya mbele za wapiga kura. Sulihusho ni kuingia 2010 na candidate mpya. Kama JK akiinebdelea 2010 ni wazi kuwa ataendelea kuilinda serikali yake.
Tunapozungumzia nguvu ya JK sio uwezo wa kuonesha ubabe kama MKAPA, au uwezo wa kutumia rungu la dola, udhaifu wake uko kwenye thinking capacity, kujieleza, kujudge na kufanya maamuzi na kuyasimamia, haya hata ukimpa mika 20 hayawezi kubadilika.
 

Acha upuuzi bwana, utamkumbuka wewe, nani haoni kama nchi imemshinda?
eti tutamkumbuka kikwete!!! kwa yapi?
 

Huyu anawahi mchuma. Kuomba kazi siyo lazima utume barua ya maombi. Hata kulamba viatu kwaweza kumpatia kazi ya nguvu ili aanze kutuzuga. Shida ni approach za kipuuzi ambazo baadhi ya watu wanatumia. Halafu nachukia sana inapotokea kuwa watu wa dini wanajiingiza kichwa kichwa kutetea mambo ambayo hayana maslahi kwa taifa.
 
ni watz wachache sana ambao wanaweza kujiumauma kuhusu uwezo wa huyu kikwete,jamani hafai!!!!!!!!!!!!!kashindwa kazi,wote wanaomtetea kikwete wameshindwa vipi kunmshauri kabla mambo hayajawa mabaya,wamechelewa na rais kafulia.............
 
hivi kwa nini JK asijiuzuru tu tukajua moja.au anataka mpaka taulo lianguke ndo ajue kuwa vitu viko serious....mi naona nchi haina utawala ni ama sokoni tu kila mtu anazungumza lake ,mara huyu uwa albino,mara znz siyo nchi,mara vunjenimuungano muone mara niongezeeni ulinzi.ni upuuzi mtupu
 

well said!
Tunapozungumzia nguvu ya JK sio uwezo wa kuonesha ubabe kama MKAPA, au uwezo wa kutumia rungu la dola, udhaifu wake uko kwenye thinking capacity, kujieleza, kujudge na kufanya maamuzi na kuyasimamia, haya hata ukimpa mika 20 hayawezi kubadilika.
 
Nahisi mkuu wa kaya hatembelei ukumbi . Una manufaa babu. Mshauirini awe anapitia mwenyewe sio through Salva
 
tunaomba majina ya hao 'mashujaa'
 
Mbadala wa Kikwete ni yupi? Baadhi yetu kuna mazuri mengi tu tunayaona chini ya UONGOZI wa JK likiwemo hili la NYINYI kumsema HOVYO humu ndani. Tunaona mabarabara yanaendelea kujengwa, shule zinajengwa, DEMOKRASIA inaendelea kukua na kupanuka, huduma kwenye ofisi za UMMA zinaimarika na kuboreshwa, kwa mara ya kwanza nimeona majina mazito tu yakisimamishwa kizimbani na kupanda karandinga za Magereza,.....
 

...............na UDOM inaendelea kujengwa!japo sheria za ugavi za nchi hii zinatatanisha sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…