Wabunge pazeni sauti kuhusu fedha kiduchu wanazopewa TARURA

Wabunge pazeni sauti kuhusu fedha kiduchu wanazopewa TARURA

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,519
Kuna Mamlaka mbili zinazosimamia barabara za Mikoa na barabara za Vijijni(Halmashauri). Mamlaka hizi zinagawiwa fedha na Serikali kila mwaka kutekeleza kazi za barabara kwa Mikoa na Halmashauri zote Tanzania Bara.

N
itoe mfano. Awamu ya nne kabla ya kuanzishwa TARURA ujenzi wa barabara ulikuwa unasimamiwa na Halmashauri lakini katika awamu ya tano ukaanzishwa TARURA yaani TANZANIA RURAL ROADS AGENCY. Wakati wa awamu ya nne kwa wastani kila Halmashauri ilikuwa inagawiwa wastani wa Tshs 800,000,000 kila mwaka ingawaje walikuwa na matatizo katika utekelezaji wa majukumu yao lakini katika awamu hii ya tano chini ya TARURA Halmashauri hupewa wastani wa Tshs 300,000,000 kutekeleza kazi zote za ujenzi wa barabara katika Halmashauri wakati TANROADS wanapewa wastani wa Tshs10bn kwa mwaka. Tujiulize wapi kuna watu?

Natumaini vijijini ndiyo kuna watu. Tukumbuke kuwa mwaka huu kumekuwa na uharibifu mkubwa wa barabara katika maeneo ya vijijini.

Je, Tshs 300,000,000 inaweza kutosha kwa Halmashauri kwa uharibifu huu wa barabara zetu vijijini? Pili, kwa nini rate ya matengenezo ya barabara za Tanroad na TARURA ni tofauti? Mfano kutengeneza kilomita moja ya barabara ya Tanroad na TARURA kiwango cha TARURA kiko chini sana.

Waheshimiwa Wabunge, pazeni sauti zenu ili TARURA wangezewe fedha za matengenezo za barabara na ni wakati mzuri mko kwenye vikao vya Bunge.
 
300M kwa halimashauri nzima? hapo ubajeti vimiradi vya 25M-60M ukisema ubajeti 150M kwa mradi utaishia kujenga Box Culvert 3 pesa inaisha.
 
Pesa hakuna Mkuu iko pesa ya kijijini chato.
Kumbuka tu kuwa TARURA ni TANZANIA RURAL AND URBAN ROADS AGENCY. Kuwa inajumuisha na barabara za mijini, manispaa na majiji. BARABARA ZA TANROADS zina bajeti kubwa kwa sababu zinapitisha magari mengi na mizigo mizito. Sasa baada ya Elimu Hii Jenga upya hoja yako wataalam waweze kuchangia.
 
Wabunge!! Elimu, BOQ, Qs., theotodile, Jesus nut, CRB,Tamesa, Mfugale [emoji563], asphalt, bitumen, riding n flexible road, Shoulder, punching shear, precast, types of bridge, PRINCIPAL.engineer afu WABUNGE TENA.!! mwisho kabisa darasa LA Saba,mpk juu, kwenye kamati Weka university.
image_fc3e437b-6bf3-4fb5-8c4a-7f18f97ae8ef20210201_230159.jpeg
 
Hoja yangu iko pale pale kwamba hakuna pesa, pesa inapelekwa chato kijijini ambako hakuhusu kitu. Dhana kwamba barabara za mijini, manispaa na majiji hazihitaji kutengewa bajeti kubwa haina mashiko na ni DHAIFU. Watanzania tunalipa kodi kubwa sana barabara zote zinastahili kutengewa bajeti ya kutosha ili kutuepusha na barabara zilizojaa makorongo ambazo ni chanzo cha ajali nyingi na magari mengi kuharibika na pia mafuriko ya kutisha.
Kumbuka tu kuwa TARURA ni TANZANIA RURAL AND URBAN ROADS AGENCY. Kuwa inajumuisha na barabara za mijini, manispaa na majiji. BARABARA ZA TANROADS zina bajeti kubwa kwa sababu zinapitisha magari mengi na mizigo mizito. Sasa baada ya Elimu Hii Jenga upya hoja yako wataalam waweze kuchangia.
 
Hoja yako ni ya msingi, lakini ninaichangia kwa mtazamo mwingine. Mimi sioni umuhimu wa kuwa na taasisi hii ya TARURA, ni kupeana ulaji tu pasipo tija kwa Taifa. Hii shughuli ya barabara ingeachwa Halmashauri tu kama zamani chini ya idara ya ujenzi, Halmashauri zilikuwa na uwezo wa kujenga kilometa nyingi za barabara bila kupangiwa.

Kama kungekuwa na umuhimu sana wa kuziondoa barabara kwenye usimamizi wa Halmashauri, basi zingepelekwa TANROADS na sio kuanzisha TARURA. Kama ishu ni uzalishaji wa ajira, hao wafanyakazi wa TARURA wangeweza kuajiriwa Halmashauri au TANROADS kufanya kazi ileile wanayofanya sasa.

Sababu ya kutaka taasisi hiyo ifutwe ni kwa sababu haina ufanisi wowote toka kuanzishwa kwake, barabara zimekuwa mbovu sana na Halmashauri wanaziangalia tu maana hawaruhusiwi kuzirekebisha.
 
Kwa kuwa hawezi kutetea Wananchi Kwa kumuogopa mtukufu wamefanya kufanya comedi. Bungeni siku hizi kuna Akina Joti, Mpoki na Bi Njelakela.
 
Nani aikoromee serkali wakati walipitishwa kwa msamaha wa Rais kama wafungwa? Ata Rais alipitishwa na tume kama mfungwa.
 
Tarura iko chini ya Tamisemi (inahusika na barabara za tawala za mikoa na serikali za mitaa).

Tanroads iko serikali kuu (inahusika na bara bara kuu, e.g mkoa kwa mkoa). Na sidhani kama bajeti ya Tshs 10b zinatosha kwa barabara za kuunganisha mikoa yote hapa TZ

Barabara nyingi za vijijini ziko hoi. Kuna kijiji daraja lilikatika miaka 6 iliyopita, mpaka leo hii halijatengezwa.

Tarura haijawajibika vyovyote ktk barabara za halmashauri. Aidha fedha ni ndogo sana ktk kukamilisha miradi ya Ujenzi ya barabara au fedha hazipo kabisa.

Bora halmshauri zihusike zenyewe ktk kukarabati/kujenga barabara zao, kwa bajeti zao wenyewe, kama ilivyokuwa hapo awali (2015 kurudi nyuma).
 
Back
Top Bottom