Uchaguzi 2020 Wabunge wa CCM mpya ni mkakati maalum wa kubadili katiba, Paul Makonda na Alexander Mnyeti ni kishindo kikuu

Hao wapinzani wa kupeleka bungeni wako wapi ?
Cha msingi mi naona wananchi tuamke tupeleke wabunge wa upinzani wakutosha bungeni, vinginevyo tutakuja kujuta huko mbele. Mungu epusha haya yasitokee
 
Hii ni kweli kabisa kila mwenye akili timamu ameshaona hili taifa linakoelekea,kama hawa watu wataingia bungeni kuanzia januari 2021,hii nchi itabadilika sana!
 
Dalili zinaonekana, mtu kama Musiba anataka kwenda bungeni kufanya nini?!

Amesifia kwenye gazeti lake ameona hiyo haitoshi sasa anataka kupeleka mapambio yake bungeni, hilo bunge lijalo linaweza kuwa la hovyo zaidi ya lile lililopita la Ndugai.
Kila mtu anao uhuru wa kugombea ubunge na kuchaguliwa ikiwa itawafaa wapiga kura. Wewe ni nani mpaka useme huyu anafaa na yule hafai.
 
Tuki fikia uko basi watanzania Tutakua tume kubari kuolewa na CCM
 
Hii iwe funzo kwa waasisi wa katiba mbovu inayompa mamlaka yasiokuwa na ukomo mtu mmoja kwenye nchi.Pia vyama kutokuwa na nguvu ya kumdhibiti rais.
Kwa kweli Tanzania inapitia kipindi kigumu labda Mungu aingilie kati huko mbeleni kwa kupindua meza kibabe.
 
Hata wakibadili katiba kwa kumlenga mtu na ulafi tu hawataweza kuongeza miaka ya kuishi. Wakifanya hivo future yao itajakuwa ni mateso na kilio na kusaga meno. Haihitaji akili nyingi kujua hili.

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
 
Hata Bunge zima liunge mkono hoja ya kuongezewa muda rais ,huku kitaani hatutokubali hata iweje,kama anataka kujiongezea muda ajiongezee kwake huko chato gbadolite aifanye nchi yake atawale milele.

Mandingo Mlaza kifo cha Mende Kondoo atashinda kawe? Betina anawezana kumuondoa Sugu kweli?. "Kichaa Huru" huyo ndio hata tatu bora hayupo!!! Huyo Mnyeti hata kama ni chagua la JIWE wananchi washamkataa kabla hata ajachatueliwa kugombea!! Kwa Makonda 50% 50% inategemea hoja/mashambulizi na kulinda kura kutoka upinzani.
 

Mkuu uko sahihi sana, lengo la Magufuli ni kuongezewa muda wa kukaa madarakani, hilo angelifanya bila hata hao wabunge uliowataja kwenda huko bungeni. Kuna uzi nilisema jana humu, uchaguzi huu utakuwa ni wa hoja V/S bunduki, lengo ni kupata serikali inayotii amri ya mtu mmoja. Ila uzuri, uongozi sio lazima upatikane kwa njia ya kura tu. Njia ya kura ni njia ya amani, lakini sio njia pekee. Maadamu njia hii ya kura imepuuzwa na kunajisiwa, basi tutegemee njia mbadala wa kura kupata uongozi.
 
Ndio, tatizo wenye bongo wameungamishwa na kwamba wakipigwa kofi kushoto wanageuza kulia lije lingine baada hapo huingia kwenye mapambio ya sifa!
Imani mpya mseto!
 
Inaweza kuwa hivyo au isiwe. Inawezekana kina Makonda na Gwajima wanataka uwaziri, mpaka uwaziri Mkuu

Paul Makonda huwa anaamini siku moja atakuwa Rais wa nchi hii.
Believe me haitokaa itokee. Kwenye uwaziri hapo sawa
 
Binadamu ni kiumbe anayezoea na akishazoea anaamini, akishaamini anajihami na woga wote unamtoka. Ukitaka kuamini chukua binadamu, mfungie sehemu halafu kila siku ingia mpige kofi, kesho tena kofi fanya hivyo kwa muda halafu angalia respond yake kila muda unapokwenda.
 
Magufuli hataongeza hata dakika moja. Akithubutu lazima watanzania tukatae.
 
Jamani Mh. Rais kasema wazi, hawezi ongeza muda, muda wake ukiisha anaondoka zake, kwanini mnamsemea maneno ya uongo, lini Mh. Rais kasema anataka kuongeza muda? Huku ni kuchafuana, acheni hizo plz
 
KAMA UNAFIKIRI CCM PEKE YAO NDIO WANAWEZA KUFANYA HIYO 'SHIKWAMBI' UMEPOTEA, THIS TIME CCM INAENDA KUAIBIKA KWA KISHINDO!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…