Wabunge waitaka Serikali kuacha tabia ya kushikilia maiti ndugu wanaposhindwa kulipa gharama za matibabu

Wabunge waitaka Serikali kuacha tabia ya kushikilia maiti ndugu wanaposhindwa kulipa gharama za matibabu

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
886c6a82d40440edb54aacc2837e2124

Wabunge wametaka Serikali kuacha tabia ya kushikilia miili ya wanaofariki na ndugu zao kushindwa kulipa gharama za matibabu kwa wagonjwa wanaofariki badala yake imetakiwa kusamehe.

Hoja hiyo ilitolewa na Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi (Sugu) na Mussa Mbarouk wa Tanga wakati wakichangia taarifa ya Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii leo Alhamis Februari 6 2020.

Mbarouk alitoa mfano wa mama aliyemuomba Rais amlipie Sh 5milioni alizokuwa akidaiwa na hospitali ikiwa ni gharama za matibabu kwa mgonjwa wake.

“Maiti wasidaiwe, Kama akifariki ndugu zake wapigiwe simu waje kumchukua ndugu yao na si kumdhalilisha kwa muda mrefu,”amesema.

Naye Sugu amesema Serikali imekuwa ikisema hakuna Mtanzania anayekosa matibabu lakini wanashikilia maiti hospitalini.

Amesema hatua ya kuzuia miili ya waliokufa inawanyima Watanzania wa kwenda kufanya ibada kwa ndugu zao wanaofariki kwa kushindwa kulipia gharama za matibabu.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndungulile amejibu hoja hiyo kwa kusema wananchi wanaokosa fedha za kulipia matitabu wanapaswa kwenda kwenye dawati la ustawi wa jamii linalokuwepo katika kila hospitali.

Amesema hawana maiti ambayo wanaishikilia kwa sababu ya madai ya gharama za matibabu kwa sababu ya utaratibu huo.
 
Naunga mkono hoja,usikute mtu kafariki kwa kukosa laki5 apate huduma bora,halafu wanataka ilipwe laki8 hatari
 
Ni ajabu kubwa. Tanzania maiti anadaiwa. Serikali kila siku inajisifu imefanikiwa kukusanya fedha nyingi. Bunge litoe tamko MAITI isidaiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ni baada ya kubainika kwamba kumbe Maiti huuzwa kwa ndugu , kwa maana ni lazima kuikomboa maiti ya ndugu yako Hospital za umma iwapo mgonjwa wako atakufa , hii ni biashara kamili .
 
Serikali haimjali mtanzania wa hali ya chini fisiemu walaaniwe
Ukitaka kujua kuna sitofaham siku moja jifanye umepotelea wodi ya wazazi hapa Mbagala Zakheem utatamani kulia jinsi wauguzi walivyozidiwa na wagonjwa waliokuja kujifunguana hao akina mama wenyewe waliokuja kujifunguana wanavyolazwa sakafuni tena kwa kurundikana.Jamaa yangu kapoteza mtoto akiwa tumboni kwa kukosa huduma stahiki
 
Ukitaka kujua kuna sitofaham siku moja jifanye umepotelea wodi ya wazazi hapa Mbagala Zakheem utatamani kulia jinsi wauguzi walivyozidiwa na wagonjwa waliokuja kujifunguana hao akina mama wenyewe waliokuja kujifunguana wanavyolazwa sakafuni tena kwa kurundikana.Jamaa yangu kapoteza mtoto akiwa tumboni kwa kukosa huduma stahiki
Nadhani Mbagala ndio eneo linaloongoza kwa kuzaa bila mpango kwa sasa duniani , hakujawahi kuwa na mwanamke mgumba Mbagala
 
Nani alipie sasa hizo gharama? Mbona mazishi ya gharama mnalipia? Serikali atakayekataa kulipia maiti ya Mzazi/Mtoto/Mike/Mume akatwe kwenye mshahara wake kwa lazima!
 
Nani alipie sasa hizo gharama? Mbona mazishi ya gharama mnalipia? Serikali atakayekataa kulipia maiti ya Mzazi/Mtoto/Mike/Mume akatwe kwenye mshahara wake kwa lazima!
Ambao sio watumishi?
 
Wanafiki tu.

Hospitali zimepunguziwa sana ruzuku toka serikali na kibaya zaidi hospitali kubwa zinalazimishwa kutoa gawio.

Sasa hapo unategemea zitatoa wapi pesa kama siyo kukamua mpaka maiti ?

Hao wabunge wanazungumza utafikiri hawajui tatizo ni Magufuli.
 
Back
Top Bottom