Elections 2010 Wachakachuaji wa demokrasia na kura ni akina nani??

Elections 2010 Wachakachuaji wa demokrasia na kura ni akina nani??

kinepi_nepi

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2007
Posts
869
Reaction score
239
Miaka mingi wasimamizi wa vituo kutoka NEC huwa wanakuwa waalimu. Na miaka ya 1995, 2000,2005 tunalia CCM inatuibia kura zetu. CCM inatumia waalimu hawa kuwafanya waiingize ikulu kwa kuwaghilibu kubadili matokeo.
Wakiingia ikulu waalimu hawa wanaachwa solemba.

Mwaka huu sijui nani watatumika na NEC kuwa maofisa wa NEC ndani ya vituo zaidi ya 50,000.

Wasimamizi wa vituo wanaoletwa na Lewis Makame ndio watu muhimu sana, najua CCM haihitaji wote 52,000 inahitaji baadhi tu ili kuwatumia kutimiza dhuluma zao, ila wakati umefika wananchi kunusa kudadisi ili kuweza kuwajua mawakala pandikizi. Tusikubali kutumiwa kulinda familia ya mtu mmoja ili tu waendelee kutumaliza, kutumia mali zetu, kutesa watoto wetu, kutunyima elimu bora na kuchukua mali zetu na kutuachia mabua.

Mawakala ni wakati wa kuchukua fedha zao na kusaini ukweli, ripoti ukweli, jumlisha ukweli. Nchi inajengwa na majasiri wachache, kuwa jasiri leo kwenye taifa lako, kuwa mfano kwa familia yako, kizazi chako na taifa lako. Kubali kuacha historia yenye enzi.
 
Back
Top Bottom