Ng'wale
JF-Expert Member
- Nov 24, 2011
- 4,690
- 3,399
mimi nilisoma Bsc ed kwasababu niliupenda ualimu kuliko dentistry niliyoomba na nikaipata.
Kwa nini uliomba kitu ambacho hukuwa unakipenda? ambacho baadaye ukaacha kukisoma? Hukua na uhakika? Kiukweli najua wapo walimu ambao wako vizuri kitaaluma kama wewe na wengine wachache, lakini ukweli lazima usemwe na ubaki palepale (ukweli utasimama) waliowengi wametelezea huko baada ya kushindwa maeneo waliyoyataka. Tunashukuru kwenu ninyi wachache ambao ufaulu wenu ni mzuri na mkaamua kuingia huko.
Kama serikali ikaamua kwamba kusoma ualimu isiwe ''adhabu'', tutainua elimu yetu na HILO NDO LILIKUA WAZO LANGU KUU KATIKA MAELEZO YANGU YOTE maana malipo ya walimu ni duni na ndicho kinachopelekea watu wanaofanya vizuri katika mitihani yao wasipende kusoma ualimu, ''wachache kama ninyi mmejitolea'' Big up.