''Wacheza bao, wavaa kobasi waliokuwa na ilmu akhera'' na wasifu wa Julius Nyerere

''Wacheza bao, wavaa kobasi waliokuwa na ilmu akhera'' na wasifu wa Julius Nyerere

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Azarel kaandika maneno hayo hapo chini:

"Nyerere alikuwa mwerevu na mwenye uwezo mkubwa wa kuongoza.
Aliwafumbua macho wacheza bao, wale wavaa kobasi waliokuwa na Ilmu Akhera tu." Azarel (JForum)

(Nimesahihisha makosa ya ucharazi na wapi iwe herufi kubwa au ndogo) ila nimeacha ''kobasi,'' iwe hivyo kwa sababu maalum.

Kauli hii imenitia hamu nipitie picha zilizoko ndani ya kitabu cha Wasifu wa Julius Nyerere na kwa bahati mbaya sikukuta picha za watu hawa, ''wacheza bao, wavaa kobasi walikuwa na Ilmu Akhera tu,'' chembelecho Azarel.

Lakini mimi ninazo picha za hawa wacheza bao nk. pamoja na wavaa mabaibui katika Maktaba yangu ambayo waandishi wa Wasifu wa kitabu cha Julius Nyerere wamesema ni kati ya maktaba tatu bora - maktaba ya Salim Ahmed Salim, Hashim Mbita na ya Mohamed Said.

Picha ya mbali kabisa wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika katika maktaba yoyote ni hii ya Wazee wa TANU walipigana Nyerere.

Picha hii ilipigwa mwezi August 1954 baada ya Kamati ya UNO kuzuru Tanganyika kuja kusikiliza maoni ya wanannchi.

Said Chamwenyewe ndiye aliyewakilisha maoni ya Watanganyika akiwa mjumbe katika Baraza la Wazee wa TANU Dar es Salaam, Makao Makuu, New Street.

Said Chamwenyewe ndiye aliyeiletea TANU wanachama wake wa kwanza kutoka Rufiji.

Baraza la Wazee wa TANU ndiyo waliyotayarisha safari ya Territorial President wa TANU Julius Nyerere kwenda UNO February, 1955

Picha nyingine ya zamani sana ni ya Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU akiwa na Julius Nyerere na John Rupia kwenye tawi la TANU alilofungua Ali Msham nyumbani kwake Mtaa wa Jaribu Magomeni Mapipa 1954/55.

Hao nyuma ya viongozi hao wa TANU ni Bantu Group kivazi chao ni hizo kaniki na wamebeba silaha za jadi mashoka, mikuki na pinde kwa ajili ya ulinzi wa viongozi wapigania uhuru wa Tanganyika.

Picha nyingine ni ya akina mama wavaa mabaibui wakimsindikiza Julius Nyerere Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam safari ya kwanza UNO 1955.

Picha ya mwisho ni ya wazalendo Iddi Faizi Mafungo Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) na Mweka Hazina wa TANU kavaa kobazi, kanzu na tarbushi na Sheikh Mohamed Ramia kavaa kobazi, kanzu na kofia wakiwa na Julius Nyerere wakitembea majimboni kuwahamisisha wananchi kujiunga na TANU kudai uhuru wa Tanganyika.

Picha hiyo imepigwa Dodoma Railway Station mwaka wa 1955.

Picha hizi zinatosha kuwa jibu kwa Azarel kuwa Nyerere hakufika Dar es Salaam akapokewa na watu wajinga kama anavyodhani.

Picha haisemi uongo.
Camera inaona kile jicho kilichoona.

Picha pia inasema maneno elfu moja.

Leo hawa wazee wangu waliompokea Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa mapenzi makubwa anatoka mtu anawatusi kwa sababu tu hawakuwa wavaa suti walikuwa wavaa kobazi kanzu na wakicheza bao.

Labda katika kitabu cha Wasifu wa Julius Nyerere wazalendo hawa wangelitajwa na picha hizi zikawepo wazee hawa wangepata heshima ile ile anayopewa Mwalimu Nyerere kama mpigania uhuru.

Haya yanatosha ingawa yapo mengi na picha nyingi za kuweka.

BARAZA LA WAZEE WA TANU KWA MAJINA.jpg
SHEIKH SULEIMAN TAKADIR NA BANTU GROUP.jpg
TATU BITI MZEE.JPG
IDD FAIZ MAFUNGO.JPG
 
ni ukwel usiopingika wavaa kanzu na mabuibui walimsapot(walihusika) pakubwa katka harakat za kudai uhuru wazee hawa serikal ingewakumbuka
Mmoja kati ya wavaa kobasi na kanzu na nyumbani kwake Mtaa wa Tandamti wana TANU walikuwa na barza wakicheza bao alikuwa Mzee Mshume Kiyate.

Mzee Mshume alimpenda sana Mwalimu Nyerere hakuna mtu asiyejua historia ya Mzee Mshume na Julius Nyerere.

Mzee Mshume alikuwa kama baba kwa Mwalimu na Mama Maria.

Bahati mbaya mno kuwa kati yao hakuna aliyeeleza wao waliishi vipi na Mzee Mshume toka wako Magomeni mwaka wa 1955 hadi wanaingia Ikulu 1961.

Uteuzi wa Nyerere kuchukua uongozi wa TAA 1953 ulifanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu Nansio Ukerewe kati ys Hamza Mwapachu, Abdulwahid Syked na Ali Mwinyi Tambwe ndani ya miezi minne ya mwanzo ya 1953.

Kisa hiki nimekieleza mara nyingi.

Uchaguzi uliomtia Nyerere katika uongozi kama Rais wa TAA ulifanyika Ukumbi wa Arnautoglo April 1953 kati ya Abdul Sykes na Julius Nyerere.

Nyerere akachaguliwa Rais na Abdul Sykes Makamu wa Rais.

Mwaka wa 1954 TANU ikaundwa.

Bahati mbaya sana Julius Nyerere hakupata kueleza historia hii.

Picha hapo chini inamuonyesha Mzee Mshume Kiyate akimvisha kitambi Julius Nyerere katika kumfariji baada ya maasi ya Tanganyika Rifles mwaka wa 1964.

Mzee Mshume alimpiga Nyerere kilemba pia kama ishara ya kumhakikishia kuwa bado yupo madarakani na wazee wa Dar es Salaam wako nyuma yake.l

Mimi napata akili zangu namuona Mzee Mshume Kiyate akiwa kwenye koti, kanzu na kofia.

Leo anatoka mtu anawatukana wazee hawa?

Hivi leo nani angetuamini sisi na historia hii kama tungelikuwa hatuna picha hizi za wazee wetu?

Picha hii alinipa Mwalimu wangu Mzee Kissinger miaka mingi nyuma.
Screenshot_20200517-063609.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
l
 
wakoloni waarabu waislamu hawakuwahi kuwaendeleza waafrika, walikuja kufanya biashara ya utumwa na pembe za ndovu, hawakujenga shule, wala hospitali, tofauti na wazungu waliojenga shule
 
Azarel kaandika maneno hayo hapo chini:

"Nyerere alikuwa mwerevu na mwenye uwezo mkubwa wa kuongoza.
Aliwafumbua macho wacheza bao, wale wavaa kobasi waliokuwa na Ilmu Akhera tu." Azarel (JForum)

(Nimesahihisha makosa ya ucharazi na wapi iwe herufi kubwa au ndogo) ila nimeacha ''kobasi,'' iwe hivyo kwa sababu maalum.

Kauli hii imenitia hamu nipitie picha zilizoko ndani ya kitabu cha Wasifu wa Julius Nyerere na kwa bahati mbaya sikukuta picha za watu hawa, ''wacheza bao, wavaa kobasi walikuwa na Ilmu Akhera tu,'' chembelecho Azarel.

Lakini mimi ninazo picha za hawa wacheza bao nk. pamoja na wavaa mabaibui katika Maktaba yangu ambayo waandishi wa Wasifu wa kitabu cha Julius Nyerere wamesema ni kati ya maktaba tatu bora - maktaba ya Salim Ahmed Salim, Hashim Mbita na ya Mohamed Said.

Picha ya mbali kabisa wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika katika maktaba yoyote ni hii ya Wazee wa TANU walipigana Nyerere.

Picha hii ilipigwa mwezi August 1954 baada ya Kamati ya UNO kuzuru Tanganyika kuja kusikiliza maoni ya wanannchi.

Said Chamwenyewe ndiye aliyewakilisha maoni ya Watanganyika akiwa mjumbe katika Baraza la Wazee wa TANU Dar es Salaam, Makao Makuu, New Street.

Said Chamwenyewe ndiye aliyeiletea TANU wanachama wake wa kwanza kutoka Rufiji.

Baraza la Wazee wa TANU ndiyo waliyotayarisha safari ya Territorial President wa TANU Julius Nyerere kwenda UNO February, 1955

Picha nyingine ya zamani sana ni ya Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU akiwa na Julius Nyerere na John Rupia kwenye tawi la TANU alilofungua Ali Msham nyumbani kwake Mtaa wa Jaribu Magomeni Mapipa 1954/55.

Hao nyuma ya viongozi hao wa TANU ni Bantu Group kivazi chao ni hizo kaniki na wamebeba silaha za jadi mashoka, mikuki na pinde kwa ajili ya ulinzi wa viongozi wapigania uhuru wa Tanganyika.

Picha nyingine ni ya akina mama wavaa mabaibui wakimsindikiza Julius Nyerere Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam safari ya kwanza UNO 1955.

Picha ya mwisho ni ya wazalendo Iddi Faizi Mafungo Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) na Mweka Hazina wa TANU kavaa kobazi, kanzu na tarbushi na Sheikh Mohamed Ramia kavaa kobazi, kanzu na kofia wakiwa na Julius Nyerere wakitembea majimboni kuwahamisisha wananchi kujiunga na TANU kudai uhuru wa Tanganyika.

Picha hiyo imepigwa Dodoma Railway Station mwaka wa 1955.

Picha hizi zinatosha kuwa jibu kwa Azarel kuwa Nyerere hakufika Dar es Salaam akapokewa na watu wajinga kama anavyodhani.

Picha haisemi uongo.
Camera inaona kile jicho kilichoona.

Picha pia inasema maneno elfu moja.

Leo hawa wazee wangu waliompokea Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa mapenzi makubwa anatoka mtu anawatusi kwa sababu tu hawakuwa wavaa suti walikuwa wavaa kobazi kanzu na wakicheza bao.

Labda katika kitabu cha Wasifu wa Julius Nyerere wazalendo hawa wangelitajwa na picha hizi zikawepo wazee hawa wangepata heshima ile ile anayopewa Mwalimu Nyerere kama mpigania uhuru.

Haya yanatosha ingawa yapo mengi na picha nyingi za kuweka.
MS nimekupata katika maoni yako na nakubaliana nawe juu ya hao waungwana kumkubali Mwalimu.
Hata hivyo maoni ya huyu Azarel wa JF yana ukakasi wa kutokuwa mwelewa.
Huyu Azarel si mwelewa kwa kukosa chimbuko ya historia si tu ya Tanganyika na TANU bali hata historia ya Mwalimu.

Hivyo basi Huyu Azarel hawezi kuwa msemaji mwenye uhimili katika kitu chochote na hayo aliyosema yatabaki kuwa maoni yake binafsi yasiyo na mashiko.
 
MS nimekupata katika maoni yako na nakubaliana nawe juu ya hao waungwana kumkubali Mwalimu.
Hata hivyo maoni ya huyu Azarel wa JF yana ukakasi wa kutokuwa mwelewa.
Huyu Azarel si mwelewa kwa kukosa chimbuko ya historia si tu ya Tanganyika na TANU bali hata historia ya Mwalimu.

Hivyo basi Huyu Azarel hawezi kuwa msemaji mwenye uhimili katika kitu chochote na hayo aliyosema yatabaki kuwa maoni yake binafsi yasiyo na mashiko.
Jidu...
Ahsante sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
wakoloni waarabu waislamu hawakuwahi kuwaendeleza waafrika, walikuja kufanya biashara ya utumwa na pembe za ndovu, hawakujenga shule, wala hospitali, tofauti na wazungu waliojenga shule
Laki...
Tafuta maana ya ukoloni kwanza utaelewa nafasi ya Waarabu katika Pwani ya Afrika ya Mashariki.

Pili napenda kukufahamisha kuwa Waislam ndiyo walikuwa watu wa kwanza kuelimika kwa kuwa na zile zinzoitwa 3Rs, yaani Reading, Writing and Arithmetic ambavyo vyote hivi vilisomeshwa katika madrasa zilizoenea kote walipokuwa Waislam.

Mmeshionari Johann Krapf alipofika Vuga kwa Chief Kimweri alishangaa kumkuta yeye na wanae wote wanajua kusoma na kuandika wakitumia alfabetu za Kiarabu.

Wajerumani sasa hawa ndiyo wakoloni walipoingia Tanganyika walitoa ajira nyingi kwa Waislam kwa kuwa ndiyo walikuwa watu wenye elimu.

Wakoloni hawakupendezewa na maendeleo haya ya Waislam wakapiga marufuku alfabeti za Kiarabu na kuanza kusomesha za Kirumi katika shule zao na elimu ikawa chini ya wamishionari na wakoloni.

Hapa ndipo uliopoanza ubaguzi dhidi ya Waislam.

Waislam wakaamua kupambana na ukoloni historia ambayo nimeiandika kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wakati lazima ukubali kwamba nyerere alikuwa na elimu kubwa au upeo mkubwa kuwashinda hao wapigania Uhuru wenzake ndio maana aliwatumia kama ngazi kisha aka wa-dump

Hayo haya kuwa makosa ya nyerere kwa sababu katika siasa na maisha mwenye elimu au upeo mkubwa humtumia mwenye upeo Mdogo ili kuweza kufikia malengo yake ... So hayo ni matatizo yao wenyewe maana walishindwa kuchanga karata zao vyema nakutambua kwamba nyerere anawatumia kama ngazi .... Kwa namna 1 ama nyingine tunaweza kusema kwamba hao wazee upeo wao kwa wakati huo haukuwa toshelezi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: T11
Kuna wakati lazima ukubali kwamba nyerere alikuwa na elimu kubwa au upeo mkubwa kuwashinda hao wapigania Uhuru wenzake ndio maana aliwatumia kama ngazi kisha aka wa-dump

Hayo haya kuwa makosa ya nyerere kwa sababu katika siasa na maisha mwenye elimu au upeo mkubwa humtumia mwenye upeo Mdogo ili kuweza kufikia malengo yake ... So hayo ni matatizo yao wenyewe maana walishindwa kuchanga karata zao vyema nakutambua kwamba nyerere anawatumia kama ngazi .... Kwa namna 1 ama nyingine tunaweza kusema kwamba hao wazee upeo wao kwa wakati huo haukuwa toshelezi

Sent using Jamii Forums mobile app
Hearly,
Baraza la Wazee wa TANU ni sehemu moja katika historia ya TANU na kupigania uhuru.

Walikuwapo vijana waliokuwa wakiendesha mambo.

Inahitaji uijue kwanza historia ya TANU ndiyo utakuwa na uelewa wa hayo unayotaka kuchangia.

Kwa miaka minne Abdul hakuitisha "delegates conference," akijaribu kumleta Chief Kidaha katika TAA.

Hii ilichukua miaka miwili hadi 1952 alipokutana na Julius Nyerere.

Hakika Mwalimu alikuwa na elimu kubwa kupita wenzake wengi na hili walilitambua na ndiyo sababu ya Nyerere kupewa uongozi wa TANU.

Nyerere hakumtumia mtu yeyote.

Hawa wote niliowataja walipigana kupata uhuru kwa manufaa ya nchi.

Peke yake asingefika popote na ndiyo unaona kila alipokwenda Tanganyika nzima alipokewa na wazalendo na wengine walikuwa katika harakati za kuikomboa Tanganyika kabla yake.

Soma historia ya Sheikh Hassan bin Ameir utaelewa.

Changamoto hiyo uliyoiita, "dumping," haikuwa kama unavyodhani kwani ni jambo zito sana na nimelieleza kwa urefu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Athari zake zinaonekana hadi leo na ndiyo sababu ikaamuliwa kuandikwa historia ya Nyerere kujaribu kuweka mambo sawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mohamed Said, kati ya hao wazee wa Dar-es-salaam, naomba unitajie walioteuliwa kushika nyazifa za kiserikali Tangu Uhuru, Jamuhuri hadi Muungano.

Maana kama walikuwa kipaumbele kwenye kupigania uhuru bila shaka walikumbukwa kwenye nyazifa nyeti za serikali ya wakati huo. La sivyo watakuwa walimkaribisha Nyerere awaongoze tu.

Pia mwandishi wa kitabu cha UWIKE USIWIKE KUTAKUCHWA kuna ajenda gani aliyofanya kitabu chake kipigwe ban.

Mwisho kwenye historia ya uhuru wa Tanganyika. Je kuna mtu anaitwa Martin Kayamba.

Naomba unijuze hayo tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom