Hao Wachezaji wa Timu ya Taifa Stars, Kocha wao Amunike ambaye namchukia mpaka basi kwakuwa hafai na hatufai pia pamoja na TFF hadi Wizara husika wasitake kutufanya Watanzania wote ni Majuha. Ukweli ni kwamba wameshajua kuwa Makapu ya Magoli tunaenda Kurudi nayo kutoka huko nchini Misri hivyo sasa wanatujenga Kisaikolojia ili hata wakifanya huko vibaya basi Kisingizio kikuwa kiwe Wachezaji waligoma, michango haikutosha na kwamba Serikali iliwatenga.
Ni Mwendawazimu tu pekee ndiyo atadhani kuwa Taifa Stars itazifungwa Timu za Senegal, Algeria na Kenya ambazo itakabiliana nazo. Kitu pekee ninachokijua na nina uhakika nacho kama Taifa Stars hii ya Kocha Mbovu na Mbinafsi itatoka huko na Alama ( Point ) basi ni 1 moja ila nina uhakika wa 100% kuwa Taifa Stars itamaliza huko ikiwa na Alama ( Point ) Sifuri ( Zero ) kabisa.
Kocha mwenye Akili na anayejua vyema Mpira kamwe hawezi Kuwaacha Wachezaji wazuri, tegemeo na muhimu kama akina Mkude, Ajib, Chilunda, Banda na Kichuya huku akifanya pia Kosa kubwa mno la Kumuacha ( Kumuondoa ) Kikosini Mchezaji Kinda kabisa Kelvin John ambaye nina uhakika angekuwepo tu huko hata kama asingempanga Kwake Yeye ( Kelvin John ) ingekuwa ni exposure ya Kutosha ambayo ingemjenga na kumsaidia pia hata Kisaikolojia na baadae ndiyo angekuja kuwa Mbadala mzuri mno wa Nahodha Mbwana Ally Samatta Kikosini.
Kama kuna Mtanzania ambaye anaiombea mabaya Taifa Stars ifungwe basi ni Mimi na mtanisamehe sana kwa hili.