Wachezaji Taifa star wanadai posho zao

Wachezaji Taifa star wanadai posho zao

nasikia Kelvin John anatakiwa na TP Mazembe?

Ni kweli na Jamaa ( TP Mazembe ) wako Jijini Dar es Salaam tokea jana Kuzungumza na Viongozi wa Vilabu na wanawataka Wachezaji Watatu Mohammed Hussein Tshabalala ( Zimbwe Jr ) wa Simba SC, Faisal Salum ( Fei Toto ) wa Yanga FC na huyo Dogo Kelvin John.
 
Ni kweli na Jamaa ( TP Mazembe ) wako Jijini Dar es Salaam tokea jana Kuzungumza na Viongozi wa Vilabu na wanawataka Wachezaji Watatu Mohammed Hussein Tshabalala ( Zimbwe Jr ) wa Simba SC, Faisal Salum ( Fei Toto ) wa Yanga FC na huyo Dogo Kelvin John.
Mungu awasaidie
 
Wawalipe tu pesa zao wasitake kuwadhulumu.

Mimi naomba wasiwalipe kabisa ili Wachezaji wapandwe na Jazba kisha Wafungishe Makusudi ili tuondolewe mapema na wale tunaomchukia Kocha Amunike tujiandae Kumpopoa na Mawe pale JNIA kama akirudi na Timu.
 
Hao Wachezaji wa Timu ya Taifa Stars, Kocha wao Amunike ambaye namchukia mpaka basi kwakuwa hafai na hatufai pia pamoja na TFF hadi Wizara husika wasitake kutufanya Watanzania wote ni Majuha. Ukweli ni kwamba wameshajua kuwa Makapu ya Magoli tunaenda Kurudi nayo kutoka huko nchini Misri hivyo sasa wanatujenga Kisaikolojia ili hata wakifanya huko vibaya basi Kisingizio kikuwa kiwe Wachezaji waligoma, michango haikutosha na kwamba Serikali iliwatenga.

Ni Mwendawazimu tu pekee ndiyo atadhani kuwa Taifa Stars itazifungwa Timu za Senegal, Algeria na Kenya ambazo itakabiliana nazo. Kitu pekee ninachokijua na nina uhakika nacho kama Taifa Stars hii ya Kocha Mbovu na Mbinafsi itatoka huko na Alama ( Point ) basi ni 1 moja ila nina uhakika wa 100% kuwa Taifa Stars itamaliza huko ikiwa na Alama ( Point ) Sifuri ( Zero ) kabisa.

Kocha mwenye Akili na anayejua vyema Mpira kamwe hawezi Kuwaacha Wachezaji wazuri, tegemeo na muhimu kama akina Mkude, Ajib, Chilunda, Banda na Kichuya huku akifanya pia Kosa kubwa mno la Kumuacha ( Kumuondoa ) Kikosini Mchezaji Kinda kabisa Kelvin John ambaye nina uhakika angekuwepo tu huko hata kama asingempanga Kwake Yeye ( Kelvin John ) ingekuwa ni exposure ya Kutosha ambayo ingemjenga na kumsaidia pia hata Kisaikolojia na baadae ndiyo angekuja kuwa Mbadala mzuri mno wa Nahodha Mbwana Ally Samatta Kikosini.

Kama kuna Mtanzania ambaye anaiombea mabaya Taifa Stars ifungwe basi ni Mimi na mtanisamehe sana kwa hili.
Kazi ya ukocha ilitangazwa, uliomba? Isiwe ni mahaba niue kwa hao wachezaji!
 
Timu hii itanipa pesa sana ntaiua mechi zote vilaza kabisa inabidi watangulize uzaelendo kwanza kwasababu ni nchi sio club
Hakuna uzalendo kwenye kazi.
Mbona rais anachukua mshahara au wabunge ambao tulitegemea wawe wazalendo...

Kwenye maslahi yao wapewe aiseeh..
Maana siku msuva akija dukani kwako akasema anaomba mchele kisa ni mzalendo kutoka taifa stars nina uhakika hutampa..

Wapewe stahiki yao kama walivyoahidiwa
 
Ahahaha anatafuna feza za watanganyika
Rais wa TFF Wallace Karia wakati anaomba Kura alikuwa na Kg 47 nina uhakika kwa jinsi alivyo sasa na kwa Pesa anazopiga na Maslahi anayoyapata hapo ukimpima atakuwa na Kg 175.
 
Wapewe tu. Hiyo ni ajira kama zingine.
Hao ni mabalozi wetu katika ulimwengu wa soka
 
Back
Top Bottom