Ushoga kwenye Kabumbu.
Hili jambo halisemwi sana lakini kwenye miaka ya themanini ulizuka mtindo wa ushoga kwenye timu za Kandanda Tanzania.
Ilikuwa inasemwa kuwa chanzo huwa ni Makocha "mabasha" ambao walikuwa wanatajwa hadi kwa majina. Ilisemwa kuwa hao makocha walikuwa wanatumia nafasi yao kuwarubuni baadhi ya wachezaji.
Hili suala ingawa anayetajwa ni mchezaji wa Simba ambaye alikuja kukanusha baadae, lakini uvumi wake ulikuwa ni mkubwa sana nyakati zile.
Tofauti ya wakati ule na sasa kulikuwa na udhibiti mkubwa wa habari kwa kuwa vyombo vya habari vilikuwa ni vichache na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano haikuwa kama ilivyo sasa. Kwa ivo habari nyingi ziliishia zilikotoka.
Ushoga kwenye Kandanda hapa Tanzania ulikuwepo.