Wachezaji wazee simba wanaiangamiza timu

Khalifavinnie

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2017
Posts
2,796
Reaction score
2,367
Habarini wana simba sports chama kubwa kwa maneno kama kina dada wasusi wa mitaani,simba ni timu maarufu kwa kusindikiza na kuzisumbua timu zenye uwezo wa kisoka barani afrika,kiufupi tunaita timu sumbufu lakini si timu shindani,na mpaka leo ni timu ambayo haifahamiki inatafuta nini kwenye soka la kimataifa zaidi ya kuzisumbua timu pinzani..
Simba kama walivyo na desturi yao falsafa yao ni kukamia mechi za kundi ili kuvuka kwenda angalau robo,wakifika hapo porojo zote kelele na vibweko vya wendawazimu vinaishia hapo na mashabiki kuridhika kuwa ndiyo uimara na utamaduni wa timu yao kufikia hapo,wamecheza michuano ya kimataifa zaidi ya mara nyingi tuu katika hizo nyingi wakiwa na mahesabu mara4 huku 3 zikiwa robo ya club bingwa huku1 ikiwa ya shirikisho,tukigusia club bingwa wali BOMOLEWA na TP MAZEMBE,CAIZER CHIEF na WYDAD CASABLANKA huku shirikisho waki TANDIKWA na ORANDO pirates....
Awamu hizo zote simba kila akifika mtoano ni kipigo nyumbani,na hata makundi huvuka kwa machoko mchuzi,washabiki wa simba ni vibwengo halisi ambao timu yao ikiifunga timu kubwa barani africa wanaona wao sasa timu imemaliza kazi na wao wanaamini ndiyo wakubwa wa soka lakini kiuhalisia huwa ni mawazo na akili za wenda wazimu tu soka ni kutawala katika dhana ya kutwaa vikombe kwa kipindi kirefu yaani mara kwa mara,mfano hai ni AL AHLY wao ndio wakubwa wa soka la vilabu africa wanatwaa makombe mara kwa mara wakikosa msimu mmoja basi ujao watabeba tuu na muda mwingine huwa wanatwaa back to ba back...
Ukikutana sasa na vibwengo wa timu yetu pendwa hapa tanzania wao ni makelele tuu kwanzia wasemaji wao wa tibu na mbana pua(wanamfaamu)kuwaaminisha uwongo na uzandiki dhidi ya sifa ya timu,kiuhalisia simba inamiliki wazee wengi kuliko vijana na ndio maana energy ya soka wanapokutana na timu shindani huwaishia na kutandikwa kama watoto,aiwezekani timu ikawa na...

CHAMA miaka 38
KAPOMBE miaka 39
BOKO miaka 43
MZAMIRU miaka 38
SHABALALA miaka 36
KIBU miaka 34
NTIBANZOKIZA miaka 41
NGOMA miaka 35
KANUTI miaka 33
INONGA miaka 34
MARONE miaka 32
PHIRI miaka 35
BALEKE miaka 34
MIQUISSOINE miaka 32

hao ndio key player wao kwamba ndo wafanye nini?,hata ligi ya tz nina wasiwasi wakaisikia kwenye bomba wasipoamka hii timu ikiplesiwa unaona kabisa inavyokata moto kwenye mechi dhidi ya prison walianza kutafuna muda dk ya60 na gori zao za ofside na penati ya machokumchuzi,,muda ujao nitaiongelea YOUNG DAR AFRICANI.....
 
Nilikuwa nimeenda hospitali kutafuta matibabu, pale Mapokezi mhudumu akaniuliza "Unatumia bima ya NHIF au ipi?", nikamjibu "NHIF!" Jirani yangu alikuwa amekaa raia mmoja shabiki wa Utopwenga (namfahamu maana huwa namwona kwenye kibanda umiza) akashtuka. Nikajua tu jamaa alifikiri nimetaja IHEFU badala ya NHIF.
 
Naona unapost huku unackizia utamu wa 'Mkuyenge' kunako mtaroni. !
 
Kichaa kimeanza baada ya mechi moja tu.
Ngojea part 2 lawama za marefa na TFF na Karia mwenyewe na Bodi ya ligi.Hawa Utopolo mbona wepesi hivyo.Chafya tu mnalalamika. Je malaria ikianza si ndio wote mtakuwa vichaa?
 
Pamoja na Simba kuwa na wachezaji wenye umri mkubwa sidhani kama ni tatizo sana. Ili timu ifanye vizuri ni lazima iwe na mchanganyiko wa wachezaji wenye umri mkubwa, wenye umri wa wakati na wenye umri mdogo ambao Simba inao wote hao. Tatizo la Simba ni uwoga wa benchi la ufundi kufanya kufanya "rotation" na "sub". Benchi la ufundi bado halijafanikiwa kabisa "kublend" kikosi chao kiwe na mchanganyiko ndio maana baada ya dakika ya 60 kwenye mechi ya Prison Simba walikata moto mpaka penalti ilipopatikana ndio ikawa nafuu kwao. Wachezaji kama Boko na Saidoo kwa umri wao ili wakupe ufanisi inabidi watumike angalau kwa muda usiozidi dakika 30 lakini wakizidi baada ya hapo ni mateso kwa wachezaji wenzao kwani akili zao zinakuwa zinataka lakini miili yao inakuwa imechoka kutokana na umri.

Na mpaka sasa sijajua kuna siri gani kati ya Saidoo na kucheza dakika zote 90 tena kwenye mechi zote mpaka za kirafiki. Ni wakati sasa uongozi uwajulishe wapenzi na wanachama wake juu ya vipengele vya mkataba wake iwapo kuna kipengele kinacholazimisha Saidoo acheze mechi zote kwa dakika 90. Haiwezekani mchezaji anacheza namba 10 ambaye ndio anatakiwa achezeshe timu pale mbele lakini hawezi mpaka Chama atoke pembeni kushoto na kulia aje afanye hiyo kazi. Sasa hivi kama kuna mchezaji wa Simba anayeongoza kwa kupoteza mipira, kupiga chenga zisizofanikiwa, kuanguka anguka uwanjani na kulazimisha kupiga mashuti ya ovyo basi ni Saidoo. Lakini maajabu ni kuwa Saidoo ndio mchezaji mwenye uhakika kwenye "first eleven" na ndio mchezaji mwenye uhakika wa kumaliza dakika zote tisini. Na mbaya zaidi hata benchi la ufundi lilikuwa halijui wakati Simba anaongoza 2 - 1 dhidi ya Prison ilikuwaje wakaanza kuzidiwa ghafla. Na benchi la ufundi la Simba lipo radhi kumtoa hata Kibu ambaye anasaidia kukaba na kutembeza timu japo mapungufu yake ni kuwa hana jicho la goli na wakamwacha Saidoo uwanjani anazurura na kupoteza mipira.

Kikubwa kwa Simba sio umri wa wachezaji wao bali ni namna benchi lao la ufundi litakavyoweza kuwachanganya wachezaji wenye umri mkubwa, wa kati na umri mdogo ili kupata timu iliyo bora kwani wachezaji walio wengi kwenye kikosi chao wana uwezo mkubwa. Na ikumbukwe kuwa mpira sasa hivi unahitaji vijana zaidi kwani umekuwa ni mchezo wa kasi sana na nguvu nyingi.

Ni mtizamo tu.
 
Kwanini usitumie kanuni ndogo tu za Uandishi.

1. Vituo.
2. Mkato
3. Mshangao,koma nk.

Andiko lote Hilo kama halina aya inakuwa ngumu kulisoma, linaonekana ni takataka.

Huwezi kuandika andiko refu kiasi hicho bila aya.

JISAHIHISHE, UPUMBAVU MTUPU.
 

Hongera sana Mkuu umejitahidi sana Kujenga hoja na Kuandika vizuri mno.

Umeandika Ukweli MTUPU almost kwa Asilimia Mia.

Ila nikudokeze na kukuongezea kitu

1. Saidio anapoteza sana Mipira pale Simba, akifuatiwa na KIBU Mzamiru na Kanute.

2. Said Ntibazonkiza ni kati ya Wachezaji walio FITI MNO Tanzania saidio yupo fiti MNO kimwili
Ananguvu sana, Miguu Iko fit, mwili upo fit stamina ya juu mno.
Katika wachezaji walio fit zaidi Tanzania ni Mzamiru, Saido, Bajana, KIBU na kanute
Miili yaoa na stamina Yao Wana NGUVU mno hawachoki na wanaweza wakacheza hata Mechi Tano kwa siku.

3. Profile ya Saido ni kubwa Sana NADHANI ndiye mchezaji mwenye mafanikio zaidi anayecheza Tanzania.

4. Siamini sana Katika USHIRIKINA lakini huko kuanguka, kupiga Mipira Nje, kukosa MAGOLi nk
HUO NI USHIRIKINA UNAOFANYA NA MAADUI WAKE YANGA NA NDANI YA SIMBA.

Karibu kwa mjadala.
 
Bigirimana alitoka Newcastle under 17
 
Nilipoona neno "timu ikiplesiwa"tu nikajua mwandishi ana level gani ya akili!
 
Unategemea hayo yote kutoka kwa mtu anayeandika neno "timu ikiplesiwa"?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…