ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,938
- 6,942
Serikali pia inapaswa kushusha bei ya EFD ili wafanyabiashara wasiwe na sababu ya kupinga kuzitumia. Hili ni swala la msingi. Kama mchakato wa zabuni ktk upatikanaji wake uligubikwa na rushwa au ukiukwaji wa sheria, uchunguzi ufanyike na wahusika wawajibishwe.
Kwa miaka mingi CCM haikutaka Wananchi wajue kuwa wanalipa kodi kila wanaponunua bidhaa. Swala la kuhamasisha ulipaji kodi limeachwa kwa TRA tena ktk msisitizo mdogo. Tunahitaji mapinduzi katika hili.
Watanzania waambiwe kwamba kwa kila sh. 100 inayotolewa kununua bidhaa au huduma Kuna sh. 18 ni hela ya kulipia hosptiali, kujenga barabara, kuleta maji nk. Watu wajue kuwa maendeleo ni Mali Yao. Hiii misemo ya CCM imejenga barabara huku Wananchi wakifichwa Khs uhusika wao na Ujenzi huo zipungue na hata zikome.
kwa maoni yangu mashine za EFD sio za kuuzia wafanya biashara bali wapewe bure kwani watazitumia kuitengenezea malato serikali.
waliozinunua kwa rushwa ili kuwabamiza wafanyabiashara, magufuri atumbue tu majipu hayo