wachungaji/manabii wanaoona mapepo tu

greatrwega61

New Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
3
Reaction score
0
Jamani naomba msaada juu ya hili
Kuna watu wanajiita wachungaji/manabii ambao maombi yao siku zote yanalenga kuondoa mapepo,kuondoa mikosi,kuhusisha kila tatizo la kiafya na shetani/mapepo matokeo yake jamii imechanganyikiwa na kusambaratika kiimani,imani za awali zinayumba na waumini wanaongezeka kwa kuona wenzao waliotangulia wanavyofaidi huduma hii,naombeni mchango wa mawazo tunaelekea wapi katika hili!
 
Mafelia siku zote hupenda kusema matatizo yetu huletwa na bahati mbaya/mikosi/shetani - Wakati ukiangalia kiukweli ni kuwa kuna sababu ambayo unaweza kui trace kwa kila balaa litokealo; Hao jamaa wamegundua kuwa huo ndo udhaifu mkubwa wa kondoo watoaji wa fungu la kumi - Ukichukulia kuwa wako kibiznes zaid
 
Marko16:17-18 nanukuu; na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio,kwa JINA langu watatoa pepo,watasema kwa lugha mpya,18 watashika nyoka,hata wakinywa kitu cha kufisha,hakitawadhuru kabisa,wataweka mikono juu ya wagonjwa,nao watapata afya....kama dini yako inaona pepo ni kawaida...Ukristo pepo ni laana,utumwa na tena ni UCHAFU..
 
.... kaze kweli kweli, mie nadhani ni biashara, wajasiriamali wengi sana kutokana na ugumu wa maisha. wakumbuka gharika ya loliondo, wakaibuka wajomba na mashangazi na wao wanagawa vikombe, waungwana wakapanga foleni. Pia wengi wetu hatuamini mafanikio yetu binafsi yanatokana na jitihada binafsi kwanza, watu waamini nguvu za giza zaidi kwenye kukwamisha maendeleo na kuleta maendeleo
 
Wajinga ndiyo waliwao!!
 
Hata shetani alibatizwa anaujua ukweli na anautumia kuwadanganya ili awaangushe mumsindikize moton, kumbuka alipoasi alitupwa pamoja na malaika waovu ambao ni malini wanaotumiwa na mawakala wa shetani yaani wana wakuasi waujuao ukweli ila wameamua kumtumikia shetani wakiwemo hao manabii wauongo wanafanya kazi kwa nguvu za kuzimu /majin wanayapandikiza na kujifanya kuwaombea na kuyatoa kwa miujiza yakishetani ndo maana mikutano mingi na makanisa yametekwa na wimbi hili na kwakuwa sisi hupenda miujiza tunakamatwa kirahs tuwe makini na dini zetu na viongozi wetu wa dini. Utawatambuaje?
Ni kwakuyachunguza mafundisho yao na kuwatazama matendo yao maana unapoitazama boriti ya mwenzio wakat yako hujaitoa n uongo, unapozikata sheria na kumkubali Mungu unadanganya kwasababu Yesu alisema ukimpenda upende na sheria zake.
 
time will tell ila nachojua mateso huwa yana part katika ukombozi, sasa unapotaka kuyakimbia sijui huwa ni uoga au ninini, abt mapepo, sidhani kama ni mengi kihiivyo coz jesus alisema "awezaje mtu kuingia kwa yule mwenye nguvu sipomfunga huyo kwanza? "so alimshinda shetani b4!! hebu jiulize hayo mapepo mengi ni africa tu? inawezekana yapo, lakini sio kwa rate hiyo tunayoiona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…