Wadada; ni kweli hamtembei na khanga za akiba kwenye mikoba yenu?

Dam55

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2015
Posts
5,641
Reaction score
11,958
Kuna tuhuma nzito dhidi yenu kuwa siku hizi hamtembei na khanga za akiba kwenye mikoba yenu.

Wengi wanasema kuwa nyinyi wadada wa sasa huwa hamchukui tahadhari kabisa

Yani mkishavaa hivyo visuriwali vyenu ndo basi tena hamkumbuki kubeba nguo nyingine.
Mnaumbuka sana kwa tabia hii. Au ndo uchafu wenyewe huu.

Wadada wa JF hebu nijibuni hapa na nyie ndo tabia yenu??
 
Inategemea mtu na mtu kwa anayejua faida ya kuwa na khanga kwenye mkoba lazima awe nayo , hawezi kuacha hata siku moja.
Nisije kuuliza swali ka kichochezi hapa.
 
Ni kweli, wadada wengi wa mjini hawabebi khanga. Isipokuwa kazi maalum.

Wakati wa ujana wangu, nilikua najua karibia Madanguro yote. Sasa ukitaka kwenda kuchomoa kifaa, kuna ishara moja kubwa sana kutaka kumjua huyu ni yeye ama la.

Ishara hiyo ni utakuta kakumbatia khanga au mtandio kwapani au kaushika mkononi pamoja na kipochi chake.

Khanga hizi zilitumika sana. Kutokana na kuwa ni 'show time', khanga ilitandikwa tu uchochoroni mnapiga show yenu kila ntu anasepa zake...... Hata kwenye Club ukimkuta mnaongea bei tu Chap Chap.

Hawaachi khanga hata iweje.
 
Kanga? Hapana hilo ni vazi la chumbani siku hizi tunabeba mitandio na iko ya kila dizaini.
 
Mimi nilazima nibebe hata km tatizo hutolipata wewe anaweza akapata mtu mwingine ukamsitiri nayooo
Upo sahihi mkuu,mwezi uliopita kuna dada alipatwa na ada yake ktk mazingira ambayo angekuwa na kanga angestirika,Ilibidi watoto wa kiume waliokuwapo pale wakamuombee kanga jirani
 
mimi nisipokua na mtandio kwenye handbag basi khanga siwezi tembea bila hivyo

tunaojua maana zake hatuwezi acha kubeba
 
Mimi nilazima nibebe hata km tatizo hutolipata wewe anaweza akapata mtu mwingine ukamsitiri nayooo
Samahani, naomba kuuliza.

Ni ya nini haswa hua inakua?

Kuna mdau amesema na nguo za ndani za akiba.

Vyote hivyo ni.vya nini?
 
Upo sahihi mkuu,mwezi uliopita kuna dada alipatwa na ada yake ktk mazingira ambayo angekuwa na kanga angestirika,Ilibidi watoto wa kiume waliokuwapo pale wakamuombee kanga jirani
What's that?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…