Wadau kupinga Job Ndugai kuwa Mgeni Rasmi kwenye Tamasha la Simba Day ina maana gani?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426


Job Ndugai ni Spika wa Bunge la Tanzania , huu ni wadhifa mkubwa mno, mtu mwenye cheo hiki anastahili kupendwa na kuheshimiwa na kila mtu katika nchi hii , Huyu ni kiongozi wa Mhimili muhimu mno wa Bunge.

Lakini cha kushangaza ni hiki , Baada ya uongozi wa Simba kumteua Ndugai kuwa Mgeni Rasmi kwenye Tamasha muhimu la Simba day watu wengi wameshang'aa na kupigwa butwaa , wengi wanapinga Ndugai kupewa heshima hiyo huku wakidai hastahili , si mwanamichezo na wala hana mvuto kwenye siasa za nchi hii , kimsingi kumteua huyu kuwa Mgeni rasmi kumeleta kama nuksi kwenye Tamasha hilo , Ni kama kuweka nazi kwenye supu .

Wako waliojiapiza kwamba Muda ambao Ndugai ataingia uwanjani wao watajiondokea zao , hata kama wamelipa pesa zao.

Kwa mnajua mambo ya namna hii, Jambo hili ni ishara ya kitu gani?
 
Hii ni MO day, na siyo Simba day,
Mwenye sherehe ndiyo amemualika mwana CCM mwenzake awe mgeni rasmi, so huwezi kumpangia,

Simba wakitaka mgeni wao awe nani waandae sherehe yao.
Unateseka ukiwa na aki na ukwa ?
 
Nakwenda uwanjani kwa ajili ya Simba na sio Ndugai
 
Wanaopinga hawajui umuhimu wa Spika katika nchi. Tuwaelimishe badala ya kuwapuuza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…