Wadau Man U na Pogba imekaaje?

Wadau Man U na Pogba imekaaje?

Abu Ubaidah Commando

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2016
Posts
7,591
Reaction score
6,946
Man U' naona mmejikoroga wenyewe, na sioni Pogba alichofanya cha maana hadi leo hii zaidi ya kuruka ruka uwanjani na kumtegemea Ibrahimovich.

Tangu ajiunge 2011–2012 Manchester United, kacheza mechi 3 bila goli lolote.

2016 hadi leo hii kishacheza mechi 6 na kapachika goli 1 tu.

Mlishindwa nini kumnunua mchezaji na mshambuliaji aliyekua FC Napoli na timu ya Argentina, na kwa sasa kanunuliwa Juventus, GONZALO HIGUAIN na anakila style ya ufungaji, since ajiunge na Juventus kacheza michezo 7 na tayari kapachika magoli 6., kila mechi alizocheza kapiga goli 2,1,2,1

Leo timu yake imepata ushindi kwa uwezo wake mwenyewe wakisaidiana na mshambuliaji mwenzake hatari Paulo Dybala dhidi ya Empoli katika league zao (Serie A) Leo hii na kupata ushindi wa 3--0 dhidi ya Empoli.

Higuain 2,Paulo Dybala 1.


Higuain angewafaa sana tu pale tena kwa pesa ndogo EURO M94.
 
Mbona una matatizo hivyo...unajua tofauti ya kiungo na mshambuliaji??? Au unavyojua kila mchezaji anayenunuliwa ni mfungaji!!!

For your information pogba hajanunuliwa amerudishwa nyumbani kwake old traford!!! We endeleza majungu wenzako wanacheza soka!!
 
Back
Top Bottom