Wadau na wajasiriamali, naomba kujuzwa kuhusu Mr. Kuku Farms na uhalisia wa aina ile ya biashara

Wadau na wajasiriamali, naomba kujuzwa kuhusu Mr. Kuku Farms na uhalisia wa aina ile ya biashara

Mkuu DECI na CCM wapi na wapi Mkuu? Btw watu wa DECI pesa zenu zipo Biotii

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaulizaje DECI na CCM wapi na wapi na unajua wazi ccm walichukua zile pesa na kuziingiza katika kampeni yao, easy money for them kutoka kwa waliowaota watuhumiwa wa kucheza upatu ambao ni kinyume na sheria....
 
Jamaa yupo Kigamboni na hivyo usemavyo ni kweli na watu wengi wamewekeza pia anasema mradi ukiwekeza unakatia na bima kusudi kujikinga na hasara,wajumbe tusubiri walau walioanza watupe feedback...

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi NAMAINGO aliishia wapi? Nayo ilikuwa imesajiliwa na walikuwa wanawasajili watu mpka NSSF .
 
Kwa 'idea' ya Mr. Kuku ilivyo ni kama kitu kinachoitwa 'Crowdfunding'.. yaani anatokea mtu anakuja na 'idea' yake ya biashara halafu wanatafuta watu wengi(wawekezaji) ambao watatoa fedha ili kuiwezesha hiyo biashara na kunakuwa na 'platform' ya kuwaunganisha ambayo ni biashara ya kuku.
Ukishawekeza fedha zako na wao(Mr. Kuku) wataanza kufuga kuku na kuuza na wateja wakubwa wanakuwa hao hao waliowekeza pamoja na wengine. Kwa hiyo ijapokuwa umewekeza fedha lakini unalazimika kununua kuku, nyama ya kuku, mayai,vifaranga ili kuharakisha faida. Ina maana ikipatikana faida mtagawana lakini ikitokea hasara mtagawana pia.
Kwa nchi zilizoendelea inaaminika sana.

Hapa Tanzania ina changamoto sana hasa kwa wawekezaji kwani:
  1. Hupewi vitabu vya fedha('Income stat. & balance sheet') kujiridhisha kama faida inapatikana.
  2. Gharama ya uhakikisho ni kubwa('Due diligence costs').
  3. Gharama ya ufuatiliaji wa mradi('monitoring') siku kwa siku ni kubwa kwa mwekezaji.
  4. Taarifa zinazotolewa ni za kuvutia na za upande mmoja('information assymetry').
Kwa hiyo miradi kama hii ni rahisi sana kugeuka na kutumika kama vichochoro vya kutakatisha fedha au 'Ponzi Schemes' kama Serikali haitaingilia kwa kuweka kanuni zinazoeleweka ikiwemo kuweka sehemu ya fedha za uwekezaji kama dhamana Benki Kuu.
Hii Kitu tulishawahi kuonya...
 
Watu bana, yaani jambo linaonekana tu kwa macho ya kawaida kua hii ni Ponzi Scheme au Pyramid Scheme mtu bado unajiuliza maswali mara mbili mbili?

Hao wenye hiyo kuku farm kwa nini wasiuze kila walichonacho na wawashawishi ndugu zao wauze kila walichonacho wawekeze kwenye hiyo project wapige hela wawe familia tajiri zaidi? Au unadhani hao jamaa wa kuku farm wanawapenda sana kuliko wanavyowapenda ndugu zao? Kwamba waone fursa wasiwaambie ndugu zao waje kuwambia nyie? Uliwahi kuona wapi?

Kila siku humu tunatahadharisha kua ukiona unaitwa kwenye deal ujue wewe ndie deal, ukiona unaitwa kwenye fursa ujue wewe ndie fursa. Wazungu husema when the deal is too good think twice. Hakuna hela inapatikana kwa haraka hivyo.

Ilikuja D9, Deci, Qnet, One coin, sijui vitu gani watu wanapigwa kila siku lakini hawajifunzi.

Hao wa kuku farm wape muda mfupi utaona mada zao humu, ni jambo la muda tu.
Naona ulitabiri yametimia hii ndo raha ya jamii forum.Kupata information ni ww kuchanganya na za kwako kuona lipi linafaa
 
Ila watz sijui tutaacha lini hizi mentality za kuhisiana utapeli kila pale inapotokea nafasi ya kuitana kwenye fursa.Kwani ni wangapi wanaotapeliana kimya kimya???

Kuna watu wengi humu wanajibu kulingana na hisia zao na mitazamo yao lakini hawajawahi kwenda ktk huo mradi na wala hata hawajui kinachofanyika huko kina sura gani.

Hao jamaa wanakuruhusu kwenda na mwanasheria wako na muwahoji kila kinachowatia masgaka km vile wao wanapataje faida,uhalali wa kampuni,mkataba wako na kampuni na pia uzungukie mradi kujionea shughuli zinazofanyika na mengineyo.Sasa jiulize ni wangapi mmeshaenda hata kujuamradi unafanyaje kazi???

Km utaenda na mwanasheria mkashindwa kuelewa uhalali wa hao jamaa na mfumo mzima wa shughuli yao basi nitawaina hai jamaa ni magenious.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli mkuu watanzania wana mentality ya hisia za utapeli panapotokea fursa!! Kama hii Mr Kuku watu wanahisi ni utapeli wakati wanaruhusu kabisa uende na mwanasheria.
 
Ni kweli mkuu watanzania wana mentality ya hisia za utapeli panapotokea fursa!! Kama hii Mr Kuku watu wanahisi ni utapeli wakati wanaruhusu kabisa uende na mwanasheria.
Sidhani tatizo ni la kisheria. Tatizo ni financial zaidi.
Mi naona mzizi wa fitina ni wao kutoa vitabu vyao vya accounts kila mtu aone kama ni biashara ina-make sense au utapeli.
Kampuni zote ambazo zinauza hisa zinaweka wazi vitabu vyao kwa wanahisa.
 
KISUTU:Mr Kuku karudishwa tena Mahakamani, ulipofika upelelezi wa kesi yake

Upelelezi wa kesi ya Uhujumu Uchumi inayomkabili mfanyabiashara Tariq Machibya(29) maarufu Mr Kuku, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu bado haujakamilika. Kutokana na hatua hiyo, kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 7 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa. Katika hati ya mashtaka mshtakiwa anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 60/2020.

Miongoni mwa mashtaka yanayomkabili Mr.Kuki ni kusimamia na kuendesha biashara ya upatu; kupokea maingizo ya fedha kutoka kwa umma bila kuwa na leseni na mashtaka matano ni kutakatisha fedha. Inadaiwa kuwa kati ya Januari 2018 na Mei 2020, katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar Es Salaam, mshtakiwa anadaiwa kusimamia biashara ya upatu.

Pia Machibya anadaiwa alijihusisha na biashara ya upatu kwa kukubali na kukusanya fedha kutoka kwa umma, akijifanya kwamba watafanya ujasiliamali wa ufugaji wa kuku na wangepata faida ya asilimia 70 ya mtaji wa awali waliowekeza kwa miezi minne na asilimia 90 ya mtaji wa awali waliowekeza kwa kipindi cha miezi sita, kiasi ambacho ni kikubwa katika biashara kuliko mtaji uliokusanywa.

Inadaiwa kati ya April 26, 2019 na Januari 26, 2020 maeneo ya Jiji la Dar Es Salaam, alijihusisha na miamala ya Sh 6.4bilioni kwa kutoa fedha hizo kutoka katika akaunti inayosomeka kwa jina la Mr Kuku Farmers Ltd iliyopo katika benki ya CRDB, wakati akijua kuwa fedha hizo ni zao tangulizi la biashara haramu ya upatu. Pia anadaiwa kupokea fedha za maingizo ya umma kiasi cha Sh.Bil 17 bila kuwa na leseni.



Sasa tusubiri kesi iishe.

Source: MillardAyo
 
Waoni

Wao ni wauzaji, wafugaji na wanunuzi wa kuku. Halafu wanakuambia wewe utajirike bila kufuga. Hivi hayo yanaingia akilini kweli? Mtu una almasi yako, halafu anakuja jamaa anakwambia hiyo si almasi ni vipande vya chupa. Na kwamba yeye ndo ana almasi na anachukua almasi yako na kukupa vipande vya chupa. Na wewe kama zuzu unaondoka ukichekelea kupata hiyo almasi bandia. Tahadhari kabla ya hatari! Tamaa ya kupata utajiri wa haraka imewaponza wengi.
Kauli Ya Mwalimu Nyerere
 
yametimia kaka[emoji419]
Watu bana, yaani jambo linaonekana tu kwa macho ya kawaida kua hii ni Ponzi Scheme au Pyramid Scheme mtu bado unajiuliza maswali mara mbili mbili?

Hao wenye hiyo kuku farm kwa nini wasiuze kila walichonacho na wawashawishi ndugu zao wauze kila walichonacho wawekeze kwenye hiyo project wapige hela wawe familia tajiri zaidi? Au unadhani hao jamaa wa kuku farm wanawapenda sana kuliko wanavyowapenda ndugu zao? Kwamba waone fursa wasiwaambie ndugu zao waje kuwambia nyie? Uliwahi kuona wapi?

Kila siku humu tunatahadharisha kua ukiona unaitwa kwenye deal ujue wewe ndie deal, ukiona unaitwa kwenye fursa ujue wewe ndie fursa. Wazungu husema when the deal is too good think twice. Hakuna hela inapatikana kwa haraka hivyo.

Ilikuja D9, Deci, Qnet, One coin, sijui vitu gani watu wanapigwa kila siku lakini hawajifunzi.

Hao wa kuku farm wape muda mfupi utaona mada zao humu, ni jambo la muda tu.
 
hii hatari, muda haujawahi kudanganya
Ndiyo Ukweli Wenyewe
[emoji16][emoji23][emoji1787][emoji2][emoji1][emoji28][emoji28][emoji16][emoji3][emoji2][emoji2][emoji1]
 
Back
Top Bottom