Wadau na wajasiriamali, naomba kujuzwa kuhusu Mr. Kuku Farms na uhalisia wa aina ile ya biashara

Mkuu DECI na CCM wapi na wapi Mkuu? Btw watu wa DECI pesa zenu zipo Biotii

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaulizaje DECI na CCM wapi na wapi na unajua wazi ccm walichukua zile pesa na kuziingiza katika kampeni yao, easy money for them kutoka kwa waliowaota watuhumiwa wa kucheza upatu ambao ni kinyume na sheria....
 
Jamaa yupo Kigamboni na hivyo usemavyo ni kweli na watu wengi wamewekeza pia anasema mradi ukiwekeza unakatia na bima kusudi kujikinga na hasara,wajumbe tusubiri walau walioanza watupe feedback...

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi NAMAINGO aliishia wapi? Nayo ilikuwa imesajiliwa na walikuwa wanawasajili watu mpka NSSF .
 
Hii Kitu tulishawahi kuonya...
 
Naona ulitabiri yametimia hii ndo raha ya jamii forum.Kupata information ni ww kuchanganya na za kwako kuona lipi linafaa
 
Ni kweli mkuu watanzania wana mentality ya hisia za utapeli panapotokea fursa!! Kama hii Mr Kuku watu wanahisi ni utapeli wakati wanaruhusu kabisa uende na mwanasheria.
 
Ni kweli mkuu watanzania wana mentality ya hisia za utapeli panapotokea fursa!! Kama hii Mr Kuku watu wanahisi ni utapeli wakati wanaruhusu kabisa uende na mwanasheria.
Sidhani tatizo ni la kisheria. Tatizo ni financial zaidi.
Mi naona mzizi wa fitina ni wao kutoa vitabu vyao vya accounts kila mtu aone kama ni biashara ina-make sense au utapeli.
Kampuni zote ambazo zinauza hisa zinaweka wazi vitabu vyao kwa wanahisa.
 
KISUTU:Mr Kuku karudishwa tena Mahakamani, ulipofika upelelezi wa kesi yake

Upelelezi wa kesi ya Uhujumu Uchumi inayomkabili mfanyabiashara Tariq Machibya(29) maarufu Mr Kuku, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu bado haujakamilika. Kutokana na hatua hiyo, kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 7 mwaka huu kwa ajili ya kutajwa. Katika hati ya mashtaka mshtakiwa anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 60/2020.

Miongoni mwa mashtaka yanayomkabili Mr.Kuki ni kusimamia na kuendesha biashara ya upatu; kupokea maingizo ya fedha kutoka kwa umma bila kuwa na leseni na mashtaka matano ni kutakatisha fedha. Inadaiwa kuwa kati ya Januari 2018 na Mei 2020, katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar Es Salaam, mshtakiwa anadaiwa kusimamia biashara ya upatu.

Pia Machibya anadaiwa alijihusisha na biashara ya upatu kwa kukubali na kukusanya fedha kutoka kwa umma, akijifanya kwamba watafanya ujasiliamali wa ufugaji wa kuku na wangepata faida ya asilimia 70 ya mtaji wa awali waliowekeza kwa miezi minne na asilimia 90 ya mtaji wa awali waliowekeza kwa kipindi cha miezi sita, kiasi ambacho ni kikubwa katika biashara kuliko mtaji uliokusanywa.

Inadaiwa kati ya April 26, 2019 na Januari 26, 2020 maeneo ya Jiji la Dar Es Salaam, alijihusisha na miamala ya Sh 6.4bilioni kwa kutoa fedha hizo kutoka katika akaunti inayosomeka kwa jina la Mr Kuku Farmers Ltd iliyopo katika benki ya CRDB, wakati akijua kuwa fedha hizo ni zao tangulizi la biashara haramu ya upatu. Pia anadaiwa kupokea fedha za maingizo ya umma kiasi cha Sh.Bil 17 bila kuwa na leseni.


Sasa tusubiri kesi iishe.

Source: MillardAyo
 
Kauli Ya Mwalimu Nyerere
 
yametimia kaka[emoji419]
 
hii hatari, muda haujawahi kudanganya
Ndiyo Ukweli Wenyewe
[emoji16][emoji23][emoji1787][emoji2][emoji1][emoji28][emoji28][emoji16][emoji3][emoji2][emoji2][emoji1]
 
JF ni msaada kwa serikali kuna wakati inabidi serikali iipongeze JF.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…