Wadau naombeni msaada, nina kiungulia

Kama relcer gel haijakusaidia jaribu omeprazol...pia zingatia kuepuka vyakula vinavyoleta kiungulia kama viazi vitamu, ndizi aina zote mbichi na za kuiva, vwakula vya unga wa ngano,baadhi ya mboga za majani kama kisamvu, mboga kama dagaa nk..nk.....pia ukiwa umetoka kula unapolala pendelea kulalia upande wa kushoto na mwisho kabisa pata vijiko 2 vya asali mbichi usiku unapotaka kulala ambapo ndo kiwe kitu cha mwisho kutia tumboni, na vijiko 2 unapoamka kabla hujatia chochote mdomoni hata mswaki......zingatia hayo wiki tu utarudi kushukuru.
 
Sawa mkuu
 
Wewe una tatizo la acid tumboni ambalo ndilo linapelekea kukwangua na kupata hivyo vidonda.Bila kupata dawa ya kuondoa au kuneutralize hiyo acid utakuwa unapona na ugonjwa unajirudia.Unatakiwa kupata dawa ya kutibu acid reflux hapo ndiyo utapoma kabisa shida hiyo.Ukipata nafasi nitafute nukuelekeze cha kufanya
 
Pole sana,kiungulia ni ishara asidi inazalishwa tumboni kupita kiasi na kupanda hadi kooni (kiunganishi cha tumbo na mdomo tunaita oesophagus ,hali hiyo tunaita GERD.Nashauri utafute mmea jamii ya mkandandogowe (psorospermum febrifegum) kwa wiki 2 utakaa sawa.
 
Ukiwa na kiungulia maana yake una vidonda vya tumbo.

Zamani niliamini dawa za hospitali haziponyi kumbe ni hizo dawa za MSD sijuwi wanaziokotaka wapi.

Mzigo huu hapa wa Mnyamwezi siku tano utaanza kula pilau dagaa na Cocacola.
 

Attachments

  • IMG20240619144407.jpg
    2.3 MB · Views: 11
Umejaribu kulamba Jivu la mkaa. Inasaidia pia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…