Wadau wa mchezo wa draft, Leo Kuna mpambano wa kukata na shoka Ronaldo vs Noel

Safi Mkuu, ingekuwa inafanyika Kitaifa ingekuwa poa sana mabingwa wa Mkoa wanakusanyika Mkoa fulani wanapiga gemu za kutosha theni tunapata bingwa wa Taifa
Kwa mabingwa wa draft na stori za kwenye draft ni kwamba tanzania kuna mabingwa 12 tu
 
Kivip Mkuu manake tunamikoa ya kutosha iweje 12 tu
Ronaldo, Noeli ,Nduli , Issa Mamba, Simba wa dodoma, Rama wa arusha, Mstaafu mangwezi,, dogo sisto, dogo janja, kwata mwivi , gaidi, na specialist wa vipande Godzilla...

Ni baadhi tu ya mafundi wa sasa kwa draft,, ukikutana nao wakataka kitu kitu waogope sana hao watu ....

Sent from my TECNO CX Air using JamiiForums mobile app
 
Hua najiulizaga hivi hawa walio master draft wanacheza draft hili hili lenye jumla ya vyumba 64 au lao linakua lina vyumba 6?

Haya madude ndio maana yalitaka kumuua mangwelele
Mkuu kama hutojali hebu tupe story ya mangwelele
 
Enzi hizo wakati nakula mingo kabla ya ujio wa simu ilikua nikikuta ninayemlia mingo maeneo ya kwao kuna kijiwe cha drafti basi mingo inaenda mororo kabisa.
 
Natamani ningekuwepo

Hawa woote wakae upande mmoja wachangie mawazo hafu tuwe kwenye time limit ya 30s


Huu mchezo ulishafanywa nikanyang'anywa pasopoti yangu namibia. Sito sahau
Hahahaha ilikuwaje
 
Mi napende bwebwe na maneno unaweza shangaa umefugwa kwa maneno tu Kuna mzee mmoja nilimkuta kavaa shati na kizibao kwa nje ati ananambia kijana usinione hivi hapa nimevaa mashati mawili hili la nje limeisha mikono kwa sababu ya kusukuma kete tu Sasa Mimi ntampatia wapi
 
Kivip Mkuu manake tunamikoa ya kutosha iweje 12 tu
Miko mingine haina mabingwa...

Ili uitwe bingwa Kuna factor zao wanaziangalia

Sheria moja ambayo hata mimi naijua, mabingwa kwa mabingwa wakikutana hua hawafungani mpaka waanzishiane.

Sio unaleta uhuni kama wa godzilla unawapingisha watu tuvipande halafu unajiita bingwa
 
Kuna mzee mmoja wa makamo ni mchungaji hua anapenda sana draf kuji-organize na vijana

Aliwekewa kete ngumu mchungaji kila akifurukuta kujidai anapiga hesabu ajinasue anaona ngoma bado ngumu.

Kijana baada ya kuona yule mchungaji anahangaika kutafuta suluhu akamuambia "mzee yesu anaponya lakini sio kwenye mabao"
 
Daa anyway nimeona hapo mtu katoka Dar kuja kucheza michezo 24 kwa 200,000 hatupo sierous kwa kweli vipi hakuna baraza la draft au taasisi inayosimamia hayo mchezo huo
Kwenye michezo kinachoangaliwa ni ubingwa mambo ya hela hayapewi kipaumbele kivile.
We hujiulizi timu zinasajili kwa mabilioni afu kombe ni milioni 80
 
Kwa Africa hayo mambo yapo ila mabara mengine money ndio factor kubwa kwao
Naamini na sie tunaelekea huko.
Mi nahisi wenzetu wameweza kwa sababu kipato cha watu wao kiko juu, ndo maana hata uwanjan viingilio vinakua juu still watu wanajaza uwanja.
Ila kwetu huku bado sana maana hali ya kiuchumi kwa watu wengi iko chini japo wanapenda sana michezo.
 
Huu mchezo toka udogoni niliukubali sana ulishawahi nifanya nikafinywa na mother..😂

I love draft sema tu silikazanii..
 
Huo mchezo niliachaga kuucheza baada yakuona unaniganda kichwani.yaani ilikua kila nikikaa naliona draft kichwani nikajisemea,kichwa chenyewe kidogo kwanini kufikiria maovyo ovyo.nikaacha kabisa kucheza.
 
Hizo ndo sheria za kimataifa za mchezo wa drft na nimewahi kushudia mpambano uliozihusisha nchi za Africa kuna watu kwenye huu mchezo wanacheza sijawahi ona.
ulikua unaanga;ia sehemu gan mkuu?
 
baba babaah Hugo Godzilla ni nyoko. Jamaal and mkono mmoja mlemavu, na anaongea kithembe.
Mzee baba hao uliowataja happy nimekuvulia kofia.

Ronaldo niliwahi kumwona miaka ya nyuma akicheza na marehemu Human mchafu.
 
Muwe mnaproje
Kwa bahati mbaya sipo eneo la tukio lakini mtanage wote utarekodiwa na Kama sijakosea huenda vedio hizo zikapakiwa Hadi U tube.Lakini nikiwahi nitatupia updates za kutosha.
Muwe mna project kwa ukuta na projector
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…