Wadau wa mchezo wa draft, Leo Kuna mpambano wa kukata na shoka Ronaldo vs Noel

Wadau wa mchezo wa draft, Leo Kuna mpambano wa kukata na shoka Ronaldo vs Noel

dah nmemiss sana draft aisee halafu nilipo sasa hamna mafundi dah, hivi kuna app yeyote ya pc ambayo ni ngumu kweli maana app zote nazopataga naona km ni kwa wale wasiojiweza tu
At least dalmax ya playstore
 
Aah aisee 30s hapo si wanakomoana sasa
Hizo ndo sheria za kimataifa za mchezo wa drft na nimewahi kushudia mpambano uliozihusisha nchi za Africa kuna watu kwenye huu mchezo wanacheza sijawahi ona.
 
Hawa jamaa wana spirit moja hivi ambayo karibia kila bingwa anayo.

Yani mchezo aliofungwa hua hawasahau, yani akitoka hapo anaenda nyumbani anakupangia kete zote namna jinsi bao lilivyokua.

Halafu anaanza kuifikiria kila kete kwa kila angle ajue wapi alikosea. Akijua basi hapo hapo anaweza akarudi kwa yule aliyemfunga na kumuambia tucheze tena. Hata kama ilikua ni kama jamaa yuko radhi aweke bondi hata simu

Inawezekana kabisa huyu ronaldo ule mchezo aliofungwa na noel kule kitunda ameufanyia majaribio kila siku na kujiridhisha kua hawezi kufungwa tena au ameuboresha zaidi kiasi cha yeye kupata ushindi
Mkuu...
Kwa comment hii, naomba nikiri kwamba unaufahamu mchezo wa draft..[emoji1666]
 
Tatizo Hawa jamaa hawapendi Sana kucheza friend matches,wao NI mwendo wa kitukitu tu.
Wote wababe, na kila mmoja anjoona mwalimu wa mwingine...[emoji23][emoji23]
 
Tatizo Hawa jamaa hawapendi Sana kucheza friend matches,wao NI mwendo wa kitukitu tu.
Mkuu ivi hakuna wadhamini tuweze kucheki kwenye luninga. Sijui kuucheza ila naupenda huu mchezo hasa ukiwakuta mafundi na maneno yao ya shombo na pia hesabu zao kali sana ukisukuma kete moja tu tayari anakumbia limeisha
 
Mkuu ivi hakuna wadhamini tuweze kucheki kwenye luninga. Sijui kuucheza ila naupenda huu mchezo hasa ukiwakuta mafundi na maneno yao ya shombo na pia hesabu zao kali sana ukisukuma kete moja tu tayari anakumbia limeisha
Hakuna wadhamini mkuu.
 
Mkuu...
Kwa comment hii, naomba nikiri kwamba unaufahamu mchezo wa draft..[emoji1666]
Naufahamu kwa kiasi chake sijafikia ile level ya kumuambia mpinzani "umefungwa" baada ya mpinzani kusukuma kete mbili za mwanzo

Kiukweli mpaka hapa umri huu nimefikia nakiri kua hakuna mchezo nao upenda kama draft.

Kuna baadhi ya michezo inakupa radha pindi ambako wewe mwenyewe unaucheza.

Lakini kwa draft ni tofauti, unaweza usipate fursa ya kucheza lakini ukikuta mabingwa wanacheza hutatamani kuondoka. Mixer na maneno ya kwenye vijiwe vya draft ndo kabisa unajikuta siku yako imeenda vizuri.
 
Daa anyway nimeona hapo mtu katoka Dar kuja kucheza michezo 24 kwa 200,000 hatupo sierous kwa kweli vipi hakuna baraza la draft au taasisi inayosimamia hayo mchezo huo
Umenikumbusha Mwaka flani hivi nakumbika kuna mtu aliweka uzi humu heading ilisomeka hivi
"Draft mchezo unaodharaulika na jamii"
 
Daa anyway nimeona hapo mtu katoka Dar kuja kucheza michezo 24 kwa 200,000 hatupo sierous kwa kweli vipi hakuna baraza la draft au taasisi inayosimamia hayo mchezo huo
Miaka fulani hivi nadhani ziliwahi kuwepo hizi tetesi likiwemo na bao sasa mambo ya vijana yalipoingilia utu uzima basi ndio hivo tena

Kwani michezo kama
Bao
Draft
Karata
Nsimbi
N.k

Unaiona siku hizi?
 
Hizo ndo sheria za kimataifa za mchezo wa drft na nimewahi kushudia mpambano uliozihusisha nchi za Africa kuna watu kwenye huu mchezo wanacheza sijawahi ona.
Hua najiulizaga hivi hawa walio master draft wanacheza draft hili hili lenye jumla ya vyumba 64 au lao linakua lina vyumba 6?

Haya madude ndio maana yalitaka kumuua mangwelele
 
Umenikumbusha Mwaka flani hivi nakumbika kuna mtu aliweka uzi humu heading ilisomeka hivi
"Draft mchezo unaodharaulika na jamii"
Kwa kweli tupo wadau wengi tu ila hakuna platform nzuri ya huu mchezo sijui tufanyaje
 
Miaka fulani hivi nadhani ziliwahi kuwepo hizi tetesi likiwemo na bao sasa mambo ya vijana yalipoingilia utu uzima basi ndio hivo tena

Kwani michezo kama
Bao
Draft
Karata
Nsimbi
N.k

Unaiona siku hizi?
Mkuu acha tu zaizi tumebase kwenye michezo inayohamasisha ngono.
Lakini nitoe rai kwa Viongozi wetu wa huu mchezo waweke mikakati ya tunatokaje hapa
 
Mi hata nikifika ugenini labda mkoani hua natafuta kijiwe cha draft maana wale wadau wa draft karibia wote tuna falsafa moja.
Safi Mkuu, ingekuwa inafanyika Kitaifa ingekuwa poa sana mabingwa wa Mkoa wanakusanyika Mkoa fulani wanapiga gemu za kutosha theni tunapata bingwa wa Taifa
 
Daa anyway nimeona hapo mtu katoka Dar kuja kucheza michezo 24 kwa 200,000 hatupo sierous kwa kweli vipi hakuna baraza la draft au taasisi inayosimamia hayo mchezo huo
Binafsi sijawahi sikia uwepo was Baraza la draft huenda ukawa umeunganishwa kwenye michezo ya asili Kama bao vile
 
Back
Top Bottom