Wadau wa uchumi inakuwaje mkoa wa Kilimanjaro unachangia pakubwa kwenye uchumi wa Tanzania kuzidi mkoa wa Geita?

Sasa ulisema hivyo watalii wanaotembelea Kenya ama Afrika ya kusini tunawafikia hata kwa kuwakaribia? Mlima Kilimanjaro hauwezi ukazidi mapato yatokanayo na sekta za madini na kilimo hata kidogo shida elimu yetu mbovu.
 
Sasa kiongozi kiuhalisia si ndio inakuwa haichangii kwenye uchumi wetu
Mchango ni mkubwa sekta ya madini kwa mwaka inachangia zaidi ya bilioni 400 za kitanzania lakini mapato ya mlima kilimamanjaro hayafikii hata bilioni mia moja kwa mwaka. Kilimo kinatoa ajira na kuingiza pesa nyingi sema kama nilivyotangulia kusema bidhaa za mashambani, kilimo na uvuvi TRA hawapo ndiyo maana kwenye data huwezi kuona mchango wake kwa takwimu za Kodi kutoka TRA.
 
Kingine mapato ya kilimo na madini unaona yanachimbwa mwanza ama Geita ila siku makampuni yanatoa mrahaba hauhesabiki unatolewa kwa mji wa Geita nop inapatiwa serikali moja kwa moja. Next please
 
Mapato ya kiutalii Arusha kama mkoa ni kwa wilaya chache sana almost wilaya tatu tu, Arumeru, Arusha na Karatu labda kwaudogo.
Hapo ndio na Mimi nimeshangaa..wanauchumi watusaidie ni vigezo gani vilivyotumika
 
Yale madini ya Geita yanaenda yuesei hapa mbabaki na michanga tu na wachimbaji wadogowadogo.

Pia wafanyakazi wale professional wa migodini asilimia kubwa ni wageni, wanawekeza makwao

Geita kuna uchawi sana, uchawi na maendeleo havikai pamoja
Du!!!
 
"Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) akitoa Tuzo kwa Mikoa mitatu iliyofanya vizuri kwenye majadiliano na kuchangia Ukuaji wa Uchumi. Mikoa hiyo ni Dodoma, Dar es Salaam na Kilimanjaro"

Zingatia maneno yaliyokolezwa wino. Mikoa hiyo ilifanya vizuri kwenye majadiliano na kuchangia ukuaji uchumi. Hiyo haina maana kuwa GDP yao ni kubwa. mikoa yenye uchumi wa juu ni Dsm, Mwanza na Mbeya.
 
Geita ni mkoa tajiri sana..Kwa maoni yangu ukiondoa Dar na Mwanza sioni mikoa ya Dodoma na Kilimanjaro unaweza kufikia Geita kwa uchangiaji kwenye uchumi wa Taifa...
Lakini ndiyo wanatuona wajinga, wakati tunachangia pakubwa sana kwenye pato la taifa.
 
Geita ni mkoa tajiri sana..Kwa maoni yangu ukiondoa Dar na Mwanza sioni mikoa ya Dodoma na Kilimanjaro unaweza kufikia Geita kwa uchangiaji kwenye uchumi wa Taifa...
Kipimo ni GDP na Kwa muktadha huo ,Geita imezidi Dodoma ila sio Kilimanjaro

Aidha kwenye ishu ya Kodi za TRA,Geita haipo hata top 15 ila Kilimanjaro Iko top 10
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…