Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 590
- 1,648
Wadau walalamikia notisi ya kuanza kutumika kwa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi bila kutolewa kwa kipindi cha mpito kabla ya kuanza kutumika rasmi kwa sheria.
Notisi ya Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi imetolewa ikionesha tarehe 1 Mei, 2023 imeteuliwa kuwa tarehe ambayo Sheria ya Ulinzi wa Taarifa itaanza kutumika.
Vilevile, Sheria hii inalalamikiwa kuwa na mapungufu makubwa hususani kifungu cha 42 kinachoipa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi uwezo wa kufanya kazi bila kujali sheria nyingine yoyote ya nchi na pia kuipa nguvu tume hiyo kuweza kuingia kwenye jengo lolote linalomilikiwa na mkusanyaji au mchakataji wa taarifa binafsi na kuchukua kifaa chochote chenye taarifa binafsi bila kibali cha mahakama.
Kifungu cha 42(1) sehemu (c) na (d) ambako wadau wanapendekeza iwepo idhini ya Mahakama ili kuhakikisha haki inatendeka.
Kifungu cha 42(3) ambacho kinalalamikiwa na wadau kuwa kitapelekea sheria nyingine za nchi kuvunjwa
Pia, wadau wamesema Maoni yaliyotolewa kurekebisha Muswada kabla haujawa sheria hayaonekani kwenye sheria na huku Kanuni zinazosimamia utekelezaji wa sheria husika zikiwa hazipo wazi kwa umma.
Mdau mwingine amedokeza: “Sheria itasimamiwa na Tume….. sheria imeanza kabla ya tume kuundwa, hivyo sheria inatekelezwa bila mtekelezaji”
Huku mwingine akieleza “Sheria husimamiwa na kanuni na miongozo; miongozo ililetwa kwa wadau lakini hakuna mrejesho wala nakala ya kanuni husika”
Notisi ya Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi imetolewa ikionesha tarehe 1 Mei, 2023 imeteuliwa kuwa tarehe ambayo Sheria ya Ulinzi wa Taarifa itaanza kutumika.
Vilevile, Sheria hii inalalamikiwa kuwa na mapungufu makubwa hususani kifungu cha 42 kinachoipa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi uwezo wa kufanya kazi bila kujali sheria nyingine yoyote ya nchi na pia kuipa nguvu tume hiyo kuweza kuingia kwenye jengo lolote linalomilikiwa na mkusanyaji au mchakataji wa taarifa binafsi na kuchukua kifaa chochote chenye taarifa binafsi bila kibali cha mahakama.
Kifungu cha 42(3) ambacho kinalalamikiwa na wadau kuwa kitapelekea sheria nyingine za nchi kuvunjwa
Pia, wadau wamesema Maoni yaliyotolewa kurekebisha Muswada kabla haujawa sheria hayaonekani kwenye sheria na huku Kanuni zinazosimamia utekelezaji wa sheria husika zikiwa hazipo wazi kwa umma.
Mdau mwingine amedokeza: “Sheria itasimamiwa na Tume….. sheria imeanza kabla ya tume kuundwa, hivyo sheria inatekelezwa bila mtekelezaji”
Huku mwingine akieleza “Sheria husimamiwa na kanuni na miongozo; miongozo ililetwa kwa wadau lakini hakuna mrejesho wala nakala ya kanuni husika”