na siku akiitambua thamani yake mutajuta hamtakua na hela yakumbakisha na atobakia bongo
Tatizo simba imeshakuwa tim ndogo kwa sasa....na sifa ya timu ndogo ni Kutoweza kuwashikilia wachezaji wazuri...sooon utaskia huyo mtu kakimbilia timu kubwa kama sio yanga,itakua azam,mwadui au stand united
Si Huyu.
Unasema si huyu Mkuu #sembo!!!!!!!!!!!!
Kwani hakuitwa huyu kwenye ile Squad ya Kilimanjaro stars!!! Mkuu hebu nikumbushe labda nimesahau
Halafu Tanzania ni kama Mungu ametupendelea kwa kutupatia vipaji vya kipekee ktk soka kuliko nchi nyingi Afrika na duniani. Tatizo shetani tuliyeamua kumkaribisha ktk maisha amezuia kabisa tukakosa akili ya kutunza na kuendeleza vipaji.
Huyu kijana Ajibu ni bonge la inside ten la miaka 2 ijayo. Farid Mussa ni winga wa kuchezea ligi kuu angalau ya Ureno ndani ya mwaka mmoja ujao! Ndemla yuko tayari isipokuwa ktk akili yake tu.
Tanzania kuwa na mseto wa wachezaji kama Aishi Manula Ajibu, Farid Mussa, Ndemla, Mwashiuya, Himid Mao, Tshabalala, Mudathir, Kapombe, Msuva, na akina Samaata ktk kipindi kimoja na kwa umri huu ni zaidi ya upendeleo. Tatizo ni nani anawandaa kutoka kucheza mpira wa shule walionao wengi wao sasa hadi kucheza mpira wa matokeo ndani ya miaka 2 ijayo? Nani anawekeza ktk kujenga miili yao, uvumilivu, saikolojia ya ushindi, na njaa ya mafanikio?
Hivi ni zaidi ya vipaji, lakni kwa kuwa sisi tumespecialize ktk saikolojia ya kufeli, itabaki stori
Narudia tena..
1. Hivi Wadau wa kandanda mnamuona kweli Ajibu?.
2. Hivi mna taarifa kua kwa sasa katika VPL hakuna deadly straika kama Ajibu?
Hebu imagine.. Kijana wa kitanzania [mwenye umri wa miaka 20 tu] anafanya haya katika ligi kuu ya Tanzania [miongoni mwa ligi ngumu ukanda kabisa huu wa CECAFA].
1. Katika misimu yake miwili tu katika VPL.. Ajibu ana hat-trick 2!!
2. Katika mechi 2 zilizopita za VPL.. Ajibu ana Goli 5!!
3. Katika mechi 3 zilizopita za VPL + 1 ya Kirafiki.. Ajibu ana goli 6!!
4. Leo kainyanyasa ipasavyo defence bora kabisa kwa sasa katika VPL.. inayoongozwa na beki bora kuwahi kushuhudiwa katika VPL.. Pascal Wawa!!
KWENU WADAU.
Tumekua tukilalamika Mara kibao kua hatuna "mtupiaji" katika Kikosi chetu cha Taifa.. Nadhani sasa upele umepata mkunaji, tena mkunaji haswaa.. Na mkunaji mwenyewe ni Ibrahim Ajibu.. Asante Mola kwa kutuletea huyu kijana katika wakati muafaka.
KWAKO Master MKWASA.
Najua ni kwa kiasi gani una kubali kipaji cha Ajibu.. na hii inajidhihirisha kwa kumjumuisha katika Kikosi chako kila Mara. Ila ni mda muafaka wa wa kumuamini zaidi na kumuweka moja kwa moja katika 1st eleven.
Ibrahim Ajibu ni kipaji adhimu kwa sasa katika ardhi yetu ya Tanzania.. Tunatakiwa Tukitunze na Tukilinde ili soon tuweze kujivunia kama tunavyofanya kwa Samata na Thomas.
Nakutakia mafanikio Mema, Ibrahim Ajibu a.k.a Mzee wa Ma Hat-Trick
Halafu Tanzania ni kama Mungu ametupendelea kwa kutupatia vipaji vya kipekee ktk soka kuliko nchi nyingi Afrika na duniani. Tatizo shetani tuliyeamua kumkaribisha ktk maisha amezuia kabisa tukakosa akili ya kutunza na kuendeleza vipaji.
Huyu kijana Ajibu ni bonge la inside ten la miaka 2 ijayo. Farid Mussa ni winga wa kuchezea ligi kuu angalau ya Ureno ndani ya mwaka mmoja ujao! Ndemla yuko tayari isipokuwa ktk akili yake tu.
Tanzania kuwa na mseto wa wachezaji kama Aishi Manula Ajibu, Farid Mussa, Ndemla, Mwashiuya, Himid Mao, Tshabalala, Mudathir, Kapombe, Msuva, na akina Samaata ktk kipindi kimoja na kwa umri huu ni zaidi ya upendeleo. Tatizo ni nani anawandaa kutoka kucheza mpira wa shule walionao wengi wao sasa hadi kucheza mpira wa matokeo ndani ya miaka 2 ijayo? Nani anawekeza ktk kujenga miili yao, uvumilivu, saikolojia ya ushindi, na njaa ya mafanikio?
Hivi ni zaidi ya vipaji, lakni kwa kuwa sisi tumespecialize ktk saikolojia ya kufeli, itabaki stori
Mkuu tukielekea kutimiza mwaka mmoja baada ya hii kauli yako nzito, Nadhani sasa sio story tena, ni suala la mda tu, Ibrahim Ajibu atakua akiwatesa mabeki wa ligi za Ulaya.
Ajibu Sasa kaiva kisawasawa.. Wachambuzi wa soka tunamuita "finished product".
Mechi 4.. Goli 7.. Go Ajibu, Sky is your Limit.
Mkuu nadhani, unamzungumzia "Fundi" Jonathan Pitroipa.Huyu kijana ni hatari sana. Ni Haruna Moshi aliyezaliwa upya. Ni kama somebody Pitroda wa Burkina Faso, aina ya wachezaji wa kipekee ktk soka na hutokea kwa nadra sana. Hatma yake iko mikononi mwake mwenyewe. Akitaka kuwa na ujasiri na nidhamu ya Samatta na Ulimwengu basi ligi za majuu zinamsubiri
Mkuu nadhani, unamzungumzia "Fundi" Jonathan Pitroipa.