Wadau yamenikuta, hawa Wanawake hawa…

Wadau yamenikuta, hawa Wanawake hawa…

Biisa

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2019
Posts
513
Reaction score
544
Habari ya usiku huu.

Kijana mwenzenu yamenikuta aisee. Ngoja niingie kwenye mada moja kwa moja.

Kuna binti nilikuwa nae na nilipanga kumuoa,lakini masiku ya hivi karibuni nimeona amebadilika hayuko kama zamani (hapa najua wakubwa wenzangu mmenielewa kwamba kitu kidogo anakasirika na kukuza mambo,nikajua hapa natafutiwa sababu ya kuachwa,machale yakanicheza mapema). Sababu binti namjua vilivyo,nikambana sana akaamua kufunguka hiyo ilikuwa juzi. Akasema ni kweli kuna mtu ameunganishiwa na ndugu zake yaani dada zake na wameanza kuwasiliana na kwa mujibu wake huyo muhusika hakumwambia kama ana mtu na binti amekubali kuolewa na huyo mtu.

Lakini katika kuunganisha doti nahisi huyo muhusika(yaani muoaji) nina mfahamu kabisa. Sasa nimekaa hapa najiuliza je nipotezee nikubali matokeo au nimfate mdau nimwambie ukweli ?

Ushauri wenu tafadhali.
 
Pole sana. Wa ku deal nae hapo ni mwanamke jamaa utamuonea bure hata ukimwambia. Pia hivi viumbe kama hakikutaki ni hakikutaki tu hata uki force. Kubaliana na hali ndani ya mwezi mmoja utapoa
Nakuelewa vizuri kaka ila inaonekana dogo ameshikwa masikio na ndugu zake.

Ngoja nivumilie yatapita tu najua.
 
Mimi nimekubali matokeo lakini namuona binti kama anataka tuendelee na kuwasiliana nikamwambia huo ujinga siufanyi aheshimu mawazo yake.

Ila katika kuwaza na kuwazua na kuunganisha nukta nikapa wazo au nimchane mdau nini ?!
Pole.. maamuzi ya kumuacha unayo mwenyewe maana wewe ndo unaemfahamu msichana wako ila kiufupi huna mke.
 
Muache aende zake piga zako kimya, mke mtarajiwa anashikiwa akili na dada zake like for real? Aisee muache
Kiukweli nimemuacha ila ameniomba msamaha nimemsamehe na anataka tuendelee na mawasiliano nikamwambia siwezi kuendelea na mawasiliano sababu nakuwa kama simfanyii fair jamaa yake. Nikampiga stop.

Kila muda kananitumia msg na kupiga simu.
 
Ukweli upi? Kwamba demu wako hakutaki wewe, anamtaka yeye?

Au kuna ukweli upi mwingine?
Kwamba huyo binti baada ya kumbana sana nilivyo hisi mabadiliko,akaniambia kwamba ndugu zake wamemtafutia mtu wa kumuoa,na mimi hanitaki tena.

Nikamwambia sawa ila katika kuunganisha matukio nahisi huyo muhusika namjua sasa wazo likaniijia kwamba nimchane mdau au nikaushe tu...?
 
Mwamba dem wangu aliunganishiwa jamaa akaanza tabia kama hizo. Nikambana akanichana na jamaa alikuja kwa gear ya ndoa fasta. Nikamsaundisha ikishindikana, miez 2 mbele akaolewa. Nikapiga moyo konde sio cmpo lakini. Miez 6 mbele ndoa chungu na ana mimba.

Demu kanitafuta avunje ndoa yake, nikamwambia pambana. Sasa katoroka na kila siku haishi kunitafuta.Ningekua mhuni ningekua kama nimeoa mimi.
Huyo demu ukimganda atakusumbua na jamaa atakua anamla. Ila mpaka hapo amini huyo jamaa anaoa, wew subiri akazinguliwe utakuja kuliliwa baadae with regrets.

Wanawake wanaamua mambo kwa hisia na sio logic,na huyo tayari kashatekwa hisia na ndio maana kakuanzia drama. I feel hali unayopitia lakini amini huyo sio wako tena lakini jiandae kumpokea baada ya muda flani baada ya mambo kuharikbika huko.Hapo huna mtu na hatarudi nyuma!
 
Back
Top Bottom