Wafanya biashara/wakulima

Wafanya biashara/wakulima

Ismoo

JF-Expert Member
Joined
Apr 18, 2018
Posts
1,101
Reaction score
1,573
Wakuu leo nimekuja tena kwenu, kupata maujuzi. Natumai mko poa na tunaendelea kuisoma namba, mafuta bei juu...! Nchi ina zizima kwa kilio cha wengi.[emoji24]

Wa kubwa bila kuwapotezea muda wenu naomba kuwauliza kwa yeyote anaye fahamu ni utaratibu gani unao tumika kwa wale wafanya biashara/wakulima wenye mizigo mikubwa kutoka mikoani wanao leta kwenye majiji kama Dar es salaam.

Mfano mtu ana ndizi mikungu mfano 300/400 au mchele tani 5 nakueledea... wakisha fikisha kwenye masoko mfano kama hapa Dar es salaam Mabibo,Mwananyamala, Tandika, na Tandale.

Huwa wanawezaje kuuza? ikumbukwe wanakuwa hawana frem wala vibanda masokoni, ninachotaka kujua wana wezaje kusukuma mizigo yao kwa haraka wa malize na kufuata mizigo mingine?

Natanguliza shukrani za dhati kwa yeyote atakaye nisaidia kunifumbulia hili fumbo.[emoji120]
 
Mi navyojua Kile kitendo cha kushusha tani tano za mchele. Halafu bei yako ni affordable kwa mnunuzi wa jumla.
Lazma mchele uishe chapu, tena utagombaniwa.


Ila ngoja waje wajuzi


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna watu wanaitwa madalali wamejaa masoko yote tz.

Kama mgeni soko husika kuwakwepa ngumu.

Chamsingi ona utaratibu mzuri wa kula nao.

Suala la usafiri magari yako mengi sana bei ni maelewano tu ingawa mafuta yamepanda bei.

Chamsingi fanya survey kwa madalali na wasafirishaji zaidi ya mmoja ili uweze kufanya ulinganifu wa bei na faida utakayoipata.

Kila jema kwako.

#MaendeleoHayanaChama
 
Sijawahi kufanya hizi biashara ila Katika kupeleleza moja na Mbili nikwamba kubali kula na madalali.... !! Madalali ndio Kila kitu....!!!..!!! Usipeleke mzigo kabla yakwenda sokoni mwenyewe kuchunguza bei na kutafuta madalali wa uhakika
 
Hua kuna madalali lakini inahitaji kuwa makini zaidi ya umakini wenyewe. Hua ni wajanja janja sana. Labda umpate mwenye weledi.
Hua wana tabia ya kung'ang'ania mzigo af kukupa hela inakua story. Wanakupanga kua mteja washampigia sim af wanabaki na mzigo, mtu mwingine akishusha tu mzigo wanakuja kukuoangia bei nyingine ya chini usipoangalia unatoka na hasara kubwa
Kaa ukijua lazma wapate chochote kitu. Sasa hapo ni ujanja wako. Labda ukubaliane kushika hela yako mwenyewe af mwishoni uwape hicho cha juu chao. Cha muhimu usiwe na tamaa. Unaeza kuja unauza kilo moja 2000 ye akapandisha mpka buku 4 kwa mfano na akauza mzigo. Hyo ya juu mpe tu kukwepa matatizo.
Fanya research ujue scarcity iliopo, njoo na mzigo weka bei ambayo itakupa faida na kukufanya usikae sana pale maana kuna risk kibao
 
Kuna watu wanaitwa madalali wamejaa masoko yote tz.

Kama mgeni soko husika kuwakwepa ngumu.

Chamsingi ona utaratibu mzuri wa kula nao.

Suala la usafiri magari yako mengi sana bei ni maelewano tu ingawa mafuta yamepanda bei.

Chamsingi fanya survey kwa madalali na wasafirishaji zaidi ya mmoja ili uweze kufanya ulinganifu wa bei na faida utakayoipata.

Kila jema kwako.

#MaendeleoHayanaChama
Nashukuru sana
 
Hua kuna madalali lakini inahitaji kuwa makini zaidi ya umakini wenyewe. Hua ni wajanja janja sana. Labda umpate mwenye weledi.
Hua wana tabia ya kung'ang'ania mzigo af kukupa hela inakua story. Wanakupanga kua mteja washampigia sim af wanabaki na mzigo, mtu mwingine akishusha tu mzigo wanakuja kukuoangia bei nyingine ya chini usipoangalia unatoka na hasara kubwa
Kaa ukijua lazma wapate chochote kitu. Sasa hapo ni ujanja wako. Labda ukubaliane kushika hela yako mwenyewe af mwishoni uwape hicho cha juu chao. Cha muhimu usiwe na tamaa. Unaeza kuja unauza kilo moja 2000 ye akapandisha mpka buku 4 kwa mfano na akauza mzigo. Hyo ya juu mpe tu kukwepa matatizo.
Fanya research ujue scarcity iliopo, njoo na mzigo weka bei ambayo itakupa faida na kukufanya usikae sana pale maana kuna risk kibao
Nimekupata vipivyo mkubwa kongole
 
Back
Top Bottom