Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kilimanjaro, imepokea zaidi ya maombi 650 kutoka kwa wafanyabiashara wakiomba kufunga biashara za maduka na hoteli za kitalii kutokana sababu mbalimbali.
Miongoni mwa sababu walizozieleza ni watalii kusitisha safari zao za kuja kutalii na kupanda Mlima Kilimanjaro.
Meneja wa TRA, Mkoa wa Kilimanjaro, Gabriel Mwangosi, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wanahabari, na kuongeza kuwa licha ya maombi ya wafanyabiashara hao, TRA imekusanya zadi ya Sh. bilioni kumi sawa na asilimia 85 ya makisio yake kwa mwezi Machi mwaka huu.
Alisema TRA kila siku kuanzia mwezi Januari mwaka huu imekuwa ikipokea wastani wa barua za maombi zaidi ya 30 kila siku kutoka kwa wafanyabiashara wakiomba kusimamisha biashara zao kwa muda, wengine moja kwa moja kutokana na mwenendo wa biashara zao.
Pia alisema tushio la maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa homa ya mapafu corona, nao ukichangia kwa kiasi kikubwa.
Gabriel alisema TRA kuanzia leo itafanya uhakiki maduka na biashara zote zilizoombewa kufungwa, na kwamba kama mfanyabiashara atabainika kuomba kufunga biashara yake huku akiendelea na biashara, mamlaka hiyo itawaburuza mahakamani na kuwatoza faini.
Alisema kuanzia leo maofisa wa TRA watazunguka mitaani kukagua biashara zilizozofungwa na kila mfanyabiashara atapaswa kuonyesha mali zilizobakia na endapo kutakuwapo na ulaghai, mamlaka hiyo itawaburuza mahakamani.
Alisema Machi mwaka huu, TRA ilikusanya zadi ya asilimia 85 ya makisio ya makusanyo ya mapato, na kwamba hatua hiyo imefikiwa baada ya wafanyabiashara mkoani hapa kuwa na mwamko wa kulipa kodi kutokana na elimu na mahusiano mazuri kati ya wafanyabiashara na watumishi wa mamlaka hiyo.
Alisema kwa siku mbili mfululizo Machi 30 na 31 mwaka huu, watumishi wa TRA mjini Moshi walikaa ofisini hadi saa nne za usiku wakiendelea kutoa huduma kwa wafanyabiashara waliojitokeza kwa wingi kulipa kodi kabla ya Machi 31 kumalizika.
Alitoa wito kwa wafanyabiashara kuacha tabia ya kujitokeza tarehe za mwisho za ulipaji wa kodi ili kuepuka kutozwa faini kwani hali hiyo inasababisha msongamano wa walipakodi na kiwakwamisha watumishi wa mamlaka hiyo kutoa huduma bora.
Gabriel alisema ili kuepuka misongamano isiyokuwa na ulazima na kuzuia kuenea kwa maambukizi ya corona katika ofisi za TRA na benki, wafanyabiashara hawanabudi kujenga utamaduni wa kulipa kodi kabla ya tarehe za mwisho.
Alisema TRA mkoani hapa imeendesha kampeni ya utoaji elimu na faida za ulipaji kodi na wafanyabiashara kuwa na mwamko wa kulipa kodi.
Gabriel alisema tishio la corona limesababisha kusitishwa kwa safari za watalii kuja kupanda Mlima Kilimanjaro na kutembelea hifadhi wanyamapori, hivyo kuathiri biashara ya utalii kwani hata hoteli za kitalii zimepunguza ama kuwaondoa wafanyakazi wanaotoa huduma kwa wageni wa utalii.
Alisema amefanya ukaguzi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na kubaini hakuna ndege yoyote kutoka mataifa ya nje wanaokuja kufanya utalii isipokuwa ndege zinaotoa huduma za kusafirisha abiria wa ndani.
NIPASHE
Miongoni mwa sababu walizozieleza ni watalii kusitisha safari zao za kuja kutalii na kupanda Mlima Kilimanjaro.
Meneja wa TRA, Mkoa wa Kilimanjaro, Gabriel Mwangosi, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wanahabari, na kuongeza kuwa licha ya maombi ya wafanyabiashara hao, TRA imekusanya zadi ya Sh. bilioni kumi sawa na asilimia 85 ya makisio yake kwa mwezi Machi mwaka huu.
Alisema TRA kila siku kuanzia mwezi Januari mwaka huu imekuwa ikipokea wastani wa barua za maombi zaidi ya 30 kila siku kutoka kwa wafanyabiashara wakiomba kusimamisha biashara zao kwa muda, wengine moja kwa moja kutokana na mwenendo wa biashara zao.
Pia alisema tushio la maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa homa ya mapafu corona, nao ukichangia kwa kiasi kikubwa.
Gabriel alisema TRA kuanzia leo itafanya uhakiki maduka na biashara zote zilizoombewa kufungwa, na kwamba kama mfanyabiashara atabainika kuomba kufunga biashara yake huku akiendelea na biashara, mamlaka hiyo itawaburuza mahakamani na kuwatoza faini.
Alisema kuanzia leo maofisa wa TRA watazunguka mitaani kukagua biashara zilizozofungwa na kila mfanyabiashara atapaswa kuonyesha mali zilizobakia na endapo kutakuwapo na ulaghai, mamlaka hiyo itawaburuza mahakamani.
Alisema Machi mwaka huu, TRA ilikusanya zadi ya asilimia 85 ya makisio ya makusanyo ya mapato, na kwamba hatua hiyo imefikiwa baada ya wafanyabiashara mkoani hapa kuwa na mwamko wa kulipa kodi kutokana na elimu na mahusiano mazuri kati ya wafanyabiashara na watumishi wa mamlaka hiyo.
Alisema kwa siku mbili mfululizo Machi 30 na 31 mwaka huu, watumishi wa TRA mjini Moshi walikaa ofisini hadi saa nne za usiku wakiendelea kutoa huduma kwa wafanyabiashara waliojitokeza kwa wingi kulipa kodi kabla ya Machi 31 kumalizika.
Alitoa wito kwa wafanyabiashara kuacha tabia ya kujitokeza tarehe za mwisho za ulipaji wa kodi ili kuepuka kutozwa faini kwani hali hiyo inasababisha msongamano wa walipakodi na kiwakwamisha watumishi wa mamlaka hiyo kutoa huduma bora.
Gabriel alisema ili kuepuka misongamano isiyokuwa na ulazima na kuzuia kuenea kwa maambukizi ya corona katika ofisi za TRA na benki, wafanyabiashara hawanabudi kujenga utamaduni wa kulipa kodi kabla ya tarehe za mwisho.
Alisema TRA mkoani hapa imeendesha kampeni ya utoaji elimu na faida za ulipaji kodi na wafanyabiashara kuwa na mwamko wa kulipa kodi.
Gabriel alisema tishio la corona limesababisha kusitishwa kwa safari za watalii kuja kupanda Mlima Kilimanjaro na kutembelea hifadhi wanyamapori, hivyo kuathiri biashara ya utalii kwani hata hoteli za kitalii zimepunguza ama kuwaondoa wafanyakazi wanaotoa huduma kwa wageni wa utalii.
Alisema amefanya ukaguzi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na kubaini hakuna ndege yoyote kutoka mataifa ya nje wanaokuja kufanya utalii isipokuwa ndege zinaotoa huduma za kusafirisha abiria wa ndani.
NIPASHE