Agrey998
JF-Expert Member
- Jul 8, 2019
- 417
- 550
Leo katika harakati zangu nimeingia kwenye moneyshop moja ndogo tu Arusha shida yangu ilikuwa ni kufanya miamala kadhaa, nimeingia nikakuta jamaa anapanga vitu nimefika pale hakuna cha karibu wala nini , ananiangalia AF kakunja sura nikauliza huduma ninayotaka hakujibu nikaona kaingia ndani basi nikamsubiri atoke , ametoka anauliza wewe una shida gani unanisimamia nje hapa, sikutaka kuongea zaidi nikaondoka.
Nimeenda kwingine nakuta jamaa anachati na simu tu namuuliza huduma ananiuliza ebu sema shida yako chap . Hapo pia nikaona hizi dharau nikaamua kwenda benki tu . Benki wamenuhudumia vizuri sana.
Wafanyabishara mtambue tu kitu kimoja kauli kwa wateja ni muhimu sana katika kumtunza mteja na kumfanya arudi siku nyingine hii itakusaidia sana hata kupandisha mauzo , kwa hao walionihudumia vibaya leo sidhani kama nitakuja kukanyaga tena kwenye biashara zao . Na msijidanganye kubwa mna wateja wengi tambueni kuna mtu ana ushawishi mkubwa anaweza akapeleka kundi kubwa la wateja au kuhamisha kundi kubwa la wateja kutoka kwako.
Na kingine pia ni kwamba hasira za nyumbani au mahali pengine usiziweke kwenye biashara yako , wateja wako ndio wanaokufanya wewe ukae pale wao wakuletee hela na Wewe uwape huduma nzuri utakuwa mwendawazimu kama utamnunia mtu anayekuletea pesa.
Jifunzeni kumsikiliza kila mtu na kutambua anataka nini msidharau wateja hata akiwa namna gani msikilize muhudumie kwa heshima akiridhika kesho atakuletea wengine au atakuwa mteja wa kudumu.
Nawasilisha
Nimeenda kwingine nakuta jamaa anachati na simu tu namuuliza huduma ananiuliza ebu sema shida yako chap . Hapo pia nikaona hizi dharau nikaamua kwenda benki tu . Benki wamenuhudumia vizuri sana.
Wafanyabishara mtambue tu kitu kimoja kauli kwa wateja ni muhimu sana katika kumtunza mteja na kumfanya arudi siku nyingine hii itakusaidia sana hata kupandisha mauzo , kwa hao walionihudumia vibaya leo sidhani kama nitakuja kukanyaga tena kwenye biashara zao . Na msijidanganye kubwa mna wateja wengi tambueni kuna mtu ana ushawishi mkubwa anaweza akapeleka kundi kubwa la wateja au kuhamisha kundi kubwa la wateja kutoka kwako.
Na kingine pia ni kwamba hasira za nyumbani au mahali pengine usiziweke kwenye biashara yako , wateja wako ndio wanaokufanya wewe ukae pale wao wakuletee hela na Wewe uwape huduma nzuri utakuwa mwendawazimu kama utamnunia mtu anayekuletea pesa.
Jifunzeni kumsikiliza kila mtu na kutambua anataka nini msidharau wateja hata akiwa namna gani msikilize muhudumie kwa heshima akiridhika kesho atakuletea wengine au atakuwa mteja wa kudumu.
Nawasilisha