Wafanyabiashara jifunzeni kuwa na kauli nzuri kwa wateja

Wafanyabiashara jifunzeni kuwa na kauli nzuri kwa wateja

Kwani hiyo good customer care mnayoitaka mnailipia?
Hatulipi lakini tusioneshane dharau basi pesa ni yangu mali ni zako wewe unauza unahitaji pesa na mimi nanunua nahitaji mali sasa kwanini tuleteane dharau. Na kama una hio mentality jitahidi kuacha hizo ni akili za kimaskini sana.
 
Hakuna mfanyabiashara anaweza fanya ivo,ukiona ivo ujue nae kaajiriwa mmiliki hayupo
 
Wafanya biashara wa Arusha some percent kauli nzuri kwa mteja hawana… tena wale wa sokoni akuone unachagua chagua sana, au ubonyezee parachichi [emoji23][emoji23]
Anakushushua bila aibu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ukita huduma au kauli nzuri kwa wahudumu wa sehemu za biashara Bongo utakwama. (nikiri hata mimi nakwazika sana na huwa siendi sehemu zanye huduma mbovu). Ajabu ni kuwa watanzania wenyewe walishazoea na kukubali kunyanyaswa.
Na ni vitu vidogo ndo vinakwamisha biashara nyingi. We kama una biashara Heshimu kila mtu ongea vizuri haikugharimu hata mia yako
 
Nini Arusha, Nenda Kusini Mtwara na Lindi ni shida, hawamjali mteja na hawamwogopi hata kdg, mshkaji wangu mmoja alikwenda Lindi mjini akafikia maeneo ya karibu na stendi, akahitaji kunyoa akaenda jirani kuna bonge ya salon, milango iko wazi, muziki mkubwa na hakuna mtu, akaingia akakaa weee hakuna mtu akaenda jirani kuuliza wakamwambia yupo around angojee kdg, akaamua kutoka mitaa kama miwili akakuta watu wanacheza pool table, akawasalimia akauliza kama kuna salon jirani, wakamjibu huko ulikotoka kuna salon, akasema ni kweli ila kinyozi hayupo, wakamwambia kinyozi si ndio huyu tunacheza naye pool table!! Alichoka jamaa akaondoka zake, ndio wabongo walivyo.
Huko kuna dogo mmoja alienda shule pale Tandahimba Asee tukaona kuliko kubebana na mizigo ni bora tukanunulie vitu hukohuko Asee walivyojua sisi ni wakuja MBN tulikoma
 
Hatulipi lakini tusioneshane dharau basi pesa ni yangu mali ni zako wewe unauza unahitaji pesa na mimi nanunua nahitaji mali sasa kwanini tuleteane dharau. Na kama una hio mentality jitahidi kuacha hizo ni akili za kimaskini sana.
Vipi kuhusu wateja wenye dharau? Hilo unaliongeleaje?
 
Good customer care ndo kila kitu kwnye biashara hawaelewi mwisho wa siku unatafuta mchawi Nani kumbe mwnyew..afu neno karibu Lina Nguvu Sana kwnye biashara [emoji4]
 
Kwani hiyo good customer care mnayoitaka mnailipia?
Hahaha,ujue sio wewe tu unaeuza au unaetoa huduma iyo pekee wapo wngine,why mteja aache duka lile aje kwako, good customer care ndo kila kitu kwnye biashara...Ni free service unatoa kwa mteja but Ina impact kubwa kwny business
 
Hahaha,ujue sio wewe tu unaeuza au unaetoa huduma iyo pekee wapo wngine,why mteja aache duka lile aje kwako, good customer care ndo kila kitu kwnye biashara...Ni free service unatoa kwa mteja but Ina impact kubwa kwny business
Maana yangu Kama hawailipii Sasa si wahame hapo wakaipate Tena bure tu.

Umeshaona unapewa huduma mbovu Sasa si Ni kuhama tu kwano shida iko wapi?
 
Leo katika harakati zangu nimeingia kwenye moneyshop moja ndogo tu Arusha shida yangu ilikuwa ni kufanya miamala kadhaa, nimeingia nikakuta jamaa anapanga vitu nimefika pale hakuna cha karibu wala nini , ananiangalia AF kakunja sura nikauliza huduma ninayotaka hakujibu nikaona kaingia ndani basi nikamsubiri atoke , ametoka anauliza wewe una shida gani unanisimamia nje hapa, sikutaka kuongea zaidi nikaondoka.

Nimeenda kwingine nakuta jamaa anachati na simu tu namuuliza huduma ananiuliza ebu sema shida yako chap . Hapo pia nikaona hizi dharau nikaamua kwenda benki tu . Benki wamenuhudumia vizuri sana.

Wafanyabishara mtambue tu kitu kimoja kauli kwa wateja ni muhimu sana katika kumtunza mteja na kumfanya arudi siku nyingine hii itakusaidia sana hata kupandisha mauzo , kwa hao walionihudumia vibaya leo sidhani kama nitakuja kukanyaga tena kwenye biashara zao . Na msijidanganye kubwa mna wateja wengi tambueni kuna mtu ana ushawishi mkubwa anaweza akapeleka kundi kubwa la wateja au kuhamisha kundi kubwa la wateja kutoka kwako.

Na kingine pia ni kwamba hasira za nyumbani au mahali pengine usiziweke kwenye biashara yako , wateja wako ndio wanaokufanya wewe ukae pale wao wakuletee hela na Wewe uwape huduma nzuri utakuwa mwendawazimu kama utamnunia mtu anayekuletea pesa.

Jifunzeni kumsikiliza kila mtu na kutambua anataka nini msidharau wateja hata akiwa namna gani msikilize muhudumie kwa heshima akiridhika kesho atakuletea wengine au atakuwa mteja wa kudumu.

Nawasilisha
Pesa uitafute kwa shida na kuitumia ni kwa shida pia.

Ukiachana na kauli za wafanyabiashara pia kuna mambo huwa yananifeshesha kwenye biashara.

Wafanyabishara wengi wanauza bidhaa wasizozijua kiundani anachojua tu ni kuzisifia. Kama mteja kaagizwa na mtu mwingine ataishia kuuziwa kitu kingine kabisa.

Wafanyabishara wengi sio waaminifu wanachojali ni kuuza bidhaa na kupata pesa tu hawajali kuhusu kesho. Kuna ndugu yangu aliwahi kuuziwa nyaya za umeme kumbe ule waya wa ndani sio imara unapukutika ukitoa lile ganda la juu, na aliuziwa dukani. Aliporudisha bidhaa ile aliambiwa auziwe nyingine ila hawabadilishi.

Mfanyabiashara akiona umekuwa mteja wake wa kudumu anakuwa ana uhakika na wewe mwishowe anaanza kukupa huduma mbovu. Na moja ya watu ambao sipendi kuhudumiwa nao ni wadada wa migahawani au hotelini bora wahudumu wa kiume.

Mwisho kabisa kuna wateja huwa ni wasumbufu balaa tena ukute mhudumu ni mwanamke kama siyo msitaarabu unaweza ukamfukuza.
 
Dawa yao kuongea kiinglish tu, utaona jinsi wanavyojigonga,
Hao ndi wabongo mteja kwao ni fala, ila ukipiga sleng wanakuchangamkia fasta
 
Mimi wakati nasimamia kibanda cha kuingiza miziki na muvi nilikua najitahidi kua rafiki kwa mteja matokeo yake stori zikasambaa kwamba natongoza wateja.

Bro akanitimua akamuweka best yake. Ofisi ikachechemea kwakua muvi na miziki ni huduma ipo kila mahali so ukimjeuria mtu kukutema siyo tatizo.

Bro akaniplease nirudi by the time narudi nikakuta kafunga ofisi imekufa. Kuna frame ipo maeneo ya Kopa kwa anayetaka

Ni mimi kabisa aisee[emoji23][emoji23]walini nunia wakawa wnakuja na wapenzi wao .mwisho wakasema nina ukimwi[emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom