Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Nimepita hapo stendi zaidi ya mara 50 lakini sikuwahi kununua chochote, hii ni kwa sababu si lazima abiria kununua kitu hapo stendi, sasa wanacholilia ni nini?
Hujanunua unamkomoa nani sasa we mbwiga,kuna siku hao wanauza wamekuja kuomba kula kwako?
Ununue,usinunue potelea pwete maskini jeuri wataishi.
We endelea kulamba mitako huko kwenye saccos yenu.
 
Naheshimu mitazamo yao,ila kwa akili ya kawaida swali analopaswa kujiuliza mtu mwenye akili ni kua abiria wamewafuata wao au huduma za usafiri? Wao ni kunifaika ni by product ya mchakato mzima wa usafiri.


Hata stand haikujengwa hapo ili iwanufaishe, wao wamefuata kwa kuzingatia kanuni ile ile ya mlishano wa kiuchumi ila ni as if wao wana athirika zaidi.. mtu anakaa magomeni mfano aache kupandia Katarama shekilango aendw mpaka mbezi mwisho? Au unakuja na gari la kutoka dodoma unaishi manzese ushukie mbezi mwisho badala ya Manzese argentina kwenye ofisi kuu ya gari.? Nawaza tu.


Wakumbuke hii kitu ilishashindikana mwanzo pamoja na nguvu kubwa iliyotumika kuwarudisha mabasi yasipakie ofisini kwao yaaanzie stand kuu mbezi.

Ngoja tuone busara itakavyoamua...
 
Wangejua haihitaji kuwa na gharama wangewaambia kuongeza nauli yote ile?? Mbona walikaza hd mkapandishiwa nauli leo ndo waje kuwaonea huruma eti tunakusogeza hd ofsini
nimesema hivi:-
pamoja na 1.kufanya biashara lakini pia 2.wanatoa huduma
Namba moja hakuna biashara ya hasara.

namba 2 kusogeza huduma karibu na mteja kunampunguzia garama za kuifuata mbali
 
Stendi inaitwa Magufuli mnategemea nini!

Ni sawa na watoto unawapa majina ya Sikudhani, Chaupepo, Masumbuko, Majuto nk.
 
kwamba gari ikitoka Ubungo hairuhusiwi kupakia tegeta?
 
Stendi inaitwa Magufuli mnategemea nini!

Ni sawa na watoto unawapa majina ya Sikudhani, Chaupepo, Masumbuko, Majuto nk.
😂️😂️😂️😂️😂️😂️ Kwamba ni mikosi tu kwa kwenda mbele 😂️😂️😂️
 
kwamba gari ikitoka Ubungo hairuhusiwi kupakia tegeta?
Hawa wanaopiga kelele wanataka watu wote walifuate gari Magufuli. Hata kama upo njia gari linapita lazima uje Magufuli kulifuta. Hapo ndo kizungumkuti kinapoanzia. Na kushika vivyo hivyo. Lengo mfike pale mlale gesti, mnunue chakula, mikate na maji. Hivyo tu wao watafurahi hata kama utapoteza 50,000 kwenye hiyo mitikasi wao ni furaha
 
Kwanza na ww umeona wapi mkoa mzima uwe na kituo kimoja cha mabasi
Mtumie akili basi wakati wa kuchangia
Yaani Dar yote stand ya mabasi ni mbagala na Magufuli si uchizi huo
 
Mbona ndege huwa hamuombi mshushwe kwenu mnakubali kwenda airport? Utaratibu wa vituo ni muhimu sana, mkifanya shaghala baghala msilalamikie mfumo na utaratibu wa serikali.

Sasa Stand ya bus ya nini kama unaweza panda na kushuka popote?
Wewe naye, ndege inaweza kushusha abiria popote? Ingewezekana hata ndege zingefanya hivyo. Wakati serikali inataka kujenga kule , wadau mbalimbali walishauri stendi ibaki ubungo sababu kunafikika kirahisi. Wakakaza fuvu, mtokeo ndio hayo.
 
Watu hamtaki utaratibu, Tukitaka tuendelee tufuate utaratibu. Kama kuna haja ya kuwa na Bus terminal /stand kila wilaya basi lifanyike, lakini vituo vilivyopo viheshimike.

Lakini hao wachache wanaotaka kupandisha na kushusha abiria nje ya vituo halali sio sawa.
 
Ulishatoa mada, jukwaa zima limetofautiana na wewe ungekuwa muungwana ungejitafakari lakini wewe michango ya kukomaa naiona unajibu kila mchango wa mwanajukwaa. Katafute biashara nyingine.
Sina kazi, nipo hapa kutoa stress zangu, au pia siruhusiwi?
 
Kwa hiyo na ndege zifuate abiria walipo? Kuna haja gani ya kutumia pesa nyingi kujenga stendi??
NB: Arusha mbaki na stendi yenu maana tumeona hazina umhimu.
Sio lazma biashara zenu ziwe stand yapo maeneo mengi sana dar yanahitaji hizo biashara

Mkishindwa fungeni milango watakuja wengine watakao weza

Gari hapo hata miambiwa zikae hapo zote hapatoshi makamapuni mawili tu yatajaza

Abooud
Shabiby
New force

Sema dar mnajikuta kama malast born wa taifa mamaee kazeni

Dodoma hatusikii kelele shabiby anaeneo lake na anaanzia hapo ndio stand kuu
Tangu enzi scandinavia alikuwa na stand yake champion pia

Acheni wivu wa kike
Sasa bus linalala kigamboni na kuna watu wa k8gamboni mnataka liende tupu hizo gharama mtawapa nyie
Huyu muislamu wa hovyo sana

Ndo anasababisha uislamu uonekane kitu kibaya
 
Unamawazo mepes sana, unatoa maboko sana

Kaza mtoto wa mama mkwe usijilemaze mwili kwa akili zako za we we nani alikwambia msafir anakuja kununua bidhaa stand kwan kariakoo karume magomeni posta kinondon makumbusho hawapajui? Mwenge hawapajui mliman city pale

Hapo ni kusafir tu
 
Dunia ya leo mfanyabiashara ndo anamfata mteja alipo na sio kinyume chake, nyinyi tokeni hapo mbezi mkatembeze bidhaa zenu Urafiki msindelee kupoteza muda.

Huo mradi kibiashara ni hasara
 
Mbona wa ubungo hawalalamiki biashara zao kufa au mnahis wao sio walipa kodi? Tafuteni kazi kuku nyie na tena tuliamua abiria hata maji tutakuwa tunanunua stand ya kibaha muone mambo yanavyoenda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…